19 Jul 2023


Usanifishaji wa Kiswahili Afrika Mashariki: Changamoto na namna ya kukabiliana nazo Mussa M. Hans University of Dar es Salaam Abstract The process of standardizing Kiswahili language started before East African countries attained independence. Despite adopting different objectives and methods, the process has been ongoing even after independence of the East African countries. When discussing this process, it is of paramount importance to take into consideration the growth of terminologies, especially scientific and technological terms, which are created almost on a daily basis. It is also important to take cognizance of an increase in the number of universities in this region in which Kiswahili is one of the subjects studied by many students. Taking into consideration the fact that Kiswahili is the medium of the subject’s instructions these universities, students need sufficient textbooks and reference books written in Kiswahili, among other things. As such, East African Community member states need standard terms in various sectors, including research. This being the case, it is important to carefully coordinate the process of standardizing Kiswahili terms for use in various domains of the East African Community. The main objective of this article, therefore, is to examine the challenges of standardizing Kiswahili in the new East African Community. The article also provides recommendations on what can be done best to facilitate effective use of Kiswahili language among East African Community member states. Key words: standardization, east Africa, Kiswahili, challenges Ikisiri Mchakato wa usanifishaji wa lugha ya Kiswahili ulianza siku nyingi, hata kabla nchi za Afrika Mashariki hazijapata uhuru. Baada ya nchi hizi kupata uhuru bado mchakato huo umeendelea japo kwa malengo na mbinu tofauti. Wakati tukiwa tunajadili kuhusu mchakato wa usanifishaji wa lugha ya Kiswahili katika nchi za Afrika Mashariki, 101 ni vema tukatilia maanani kuhusu mfumuko wa istilahi, hasa istilahi zinazohusu maendeleo ya sayansi na teknolojia ambazo huibuka kila uchao. Aidha, tukumbuke pia kwamba hivi sasa kuna mfumuko wa vyuo vikuu na Kiswahili ni miongoni mwa masomo yanayosomwa na wanafunzi wengi katika vyuo hivyo. Wanafunzi hao kwa yakini wanahitaji vitabu vya kutosha vya marejeo tena vilivyoandikwa kwa lugha ya Kiswahili. Wanajumuiya hawa pia wanahitaji kuwa na istilahi kubalifu katika nyanja mbalimbali ikiwa ni pamoja istilahi za utafiti hasa ukitilia maanani kwamba lugha ya mawasiliano katika ufundishaji wa somo hili ni Kiswahili. Katika mazingira kama haya kuna umuhimu wa kusimamia kwa makini mchakato wa usanifishaji wa istilahi za Kiswahili katika nyanja mbalimbali ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki. Lengo la makala haya ni kujadili changamoto zinazolikabili zoezi la usanifishaji wa Kiswahili katika jumuiya mpya ya Afrika Mashariki. Makala haya pia yatatoa mapendekezo ya nini kifanyike ili kuwa na matumizi bora ya lugha ya Kiswahili miongoni mwa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. Maneno ya msingi: usanifishaji, Afrika mashariki, changamoto, Kiswahili Utangulizi Hivi sasa nchi za Afrika Mashariki ziko katika mwendelezo wa kuunda upya Jumuiya yao ambayo ilivunjika zaidi ya miaka ishirini iliyopita. Idadi ya nchi wanachama nayo imeongezeka ambapo nchi za Rwanda na Burundi na hivi karibuni Sudani ya kusini zimejiunga katika Jumuiya hii. Miongoni mwa mambo ya msingi yanayojadiliwa katika Jumuiya hii ni lugha moja itakayorahisisha mawasiliano miongoni mwa nchi zote wanachama. Lugha ya Kiswahili imepewa fursa hii adhimu ya kutumika katika mawasiliano miongoni mwa nchi wanachama.1 Wakati haya yote yakifanyika, ile Kamati ya Lugha iliyokuwa na uwakilishi kutoka nchi zote wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, hivi sasa haipo tena. Badala yake kuna Taasisi ya Taaluma za Kiswahili ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambayo ilirithi baadhi ya kazi za Kamati. Aidha, hivi karibuni imeanzishwa 1 Hivi karibuni tumeshuhudia Bunge la Afrika Mashariki likipitisha pendekezo la kukitambua Kiswahili kuwa miongoni mwa lugha rasmi sambamba na Kiingerezakatika Jumuiya ya Afrika Mashariki. 102 Kamisheni ya Kiswahili ya Afrika Mashariki ambayo ingawa bado haijawa na watendaji wa kutosha imekwishaanza kazi ikiwa ni pamoja na kuandaa mpango mkakati wa Kamisheni. Kamisheni hii inatarajiwa kuendeleza majukumu yaliyokuwa yakifanywa na Kamati ya Lugha. Hata hivyo ni vema ikafahamika kuwa ili lugha hii iweze kutekeleza jukumu lake la kufanikisha mawasiliano miongoni mwa wanajumuiya, kuna haja ya kuandaa namna bora itakayowawezesha wanajumuiya kuwasiliana bila kikwazo. Namna mojawapo ni kuwa na njia muafaka ya kusanifisha lugha ya Kiswahili kama ilivyokuwa wakati wa utawala wa Mwingereza na pengine kupiga hatua zaidi ya ilivyokuwa wakati wa utawala wa Mwingireza. Hii ndiyo sababu makala haya yanalenga kujadili mchakato wa usanifishaji katika Jumuiya mpya ya Afrika Mashariki, changamoto zake na namna ya kukabiliana na changamoto hizo. Kabla ya kuanza mjadala huu makala yanaanza kwa kutoa usuli kuhusu mchakato wa usaninifishaji katika Jumuiya ya Afrika Mashariki kabla ya nchi hizi kupata uhuru. Makala haya yanalenga kujadili kuhusu mchakato wa usanifishaji katika jumuiya ya Afrika Mashariki iliyoanzishwa miaka kadhaa iliyopita. Makala yanajikita katika kuainisha changamoto zinazoukabili mchakato wa usanifishaji na namna ya kukabiliana na changamoto hizo. Makala yanaanza kwa kutoa usuli wa mchakato wa usanifishaji uliokuwa ukifanywa wakati wa utawala wa Mwingireza katika nchi za Afrika Mashariki Usuli kuhusu Usanifishaji wa Kiswahili Wakati wa utawala wa wakoloni katika nchi za Afrika Mashariki, paliibuka haja ya kuwa na lugha moja itakayotumika katika elimu na mawasiliano miongoni mwa wananchi wa nchi zote za makoloni ya Mwingereza wakati ule, yaani Tanganyika, Kenya, Uganda na Zanzibar. Lengo lilikuwa ni kuwaandaa wananchi ambao wangewasaidia wakoloni hasa katika masuala ya utawala (Kiango, 2002; Massamba, 1989, 2005). Mjadala ukaanza juu ya lugha itakayoweza kutumiwa na wakazi wengi waishio katika ukanda wa Afrika Mashariki hasusan katika sekta rasmi kama vile elimu na utawala. Kwa kuwa lugha ya Kiswahili ilikuwa imeenea sehemu kubwa ya Afrika Mashariki, lugha hii ikapewa jukumu hili adhimu la kufanikisha mawasiliano miongoni mwa wananchi wa nchi hizi. 103 Hata hivyo, kuteuliwa kwa lugha ya Kiswahili kutumika katika shughuli za mawasiliano kwa wakazi wa Afrika Mashariki bado kulikabiliwa na changamoto nyingi. Miongoni mwa changamoto hizo ni lugha ya Kiswahili kuwa na lahaja2 nyingi na kila lahaja ikawa na kundi la watu walioishabikia na kuitumia. Nyingi ya lahaja hizi zinapatikana Pwani ya Afrika Mashariki. Lahaja hizi ni pamoja na Chimiini, Kipate, Kitikuu, Kishela, Kiamu, Kimvita, Chichifundi, Kibajuni, Kimafia, Kivumba, Kimtang’ata, Kinzwani, Shingazija, Kipemba, Kitumbatu, Kihadimu3 , na Kiunguja (Mkude, 2005; Nurse na Spear, 1985; Whiteley, 1969).4 Miongoni mwa lahaja hizo, lahaja ya Kiunguja (lahaja ya Zanzibar mjini) na Kimvita (lahaja ya Mombasa) ndizo zilikuwa katika ushindani mkubwa, kwani kila moja ilionekana kuwa na mashabiki wengi. Mashabiki hawa hawakuwa wazawa tu bali hata wageni ambao wengi wao walikuwa Wamisionari waliokuwa wakifanya kazi ya kueneza dini (Chiraghdin na Mnyampala, 1977; Massamba, 2005). Hatimaye, kwenye miaka ya 1920 ubishi huu ukafikia ukomo na lahaja ya Kiunguja ikateuliwa kuwa msingi wa Kiswahili sanifu. Baada ya uteuzi wa lahaja ya Kiunguja, mnamo mwezi Januari, 1930 iliundwa Kamati ya Lugha ya Afrika Mashariki. Kamati ilikuwa na wajumbe kumi na saba, wajumbe wanne kutoka kila nchi pamoja na Katibu wa Kamati.5 (Chiraghdin na Mnyampala, 1977; Massamba, 2005; Mulokozi, 2005; Whiteley, 1969). Miongoni mwa wajumbe hao wanne kutoka kwenye kila nchi ni Mkurugenzi wa elimu,6 afisa mmoja wa serikali na wajumbe wengine wawili ambao si maafisa wa serikali. Kuanzia mwaka 1939 ilishauriwa kwamba 2 Kwa mujibu wa TUKI (2013:282) lahaja ni tofauti katika matamshi, maumbo na matumizi ya maneno katika maeneo mbalimbali kwa lugha yenye asili moja. 3 Kwa mujibu wa makala haya , jina la Hadimu kwa sasa halitumiki tena badala yake jina la Makunduchi hutumika. Hivyo lahaja hii inaitwa Kimakunduchi. 4 Majina na idadi ya lahaja za Kiswahili yamekuwa yakitofautiana baina ya mwandishi mmoja na mwingine. 5 Katibu wa kwanza wa Kamati alikuwa Fredrick Johnson. 6 Nchini Tanzania, afisa huyu kwa sasa anajulikana kama Kamishna wa elimu. Huyu ni mjumbe muhimu sana kwani ndiye msimamizi mkuu wa masuala ya elimu na ofisi yake ndiyo inayopaswa kuidhinisha vitabu vinavyopaswa kutumika kufundishia hasa katika ngazi ya shule za msingi na sekondari. 104 pawe na mjumbe mmoja ambaye ni mzawa wa lugha ya Kiswahili kutoka katika kila nchi. Yafuatayo yalikuwa majukumu ya Kamati ya lugha: i. Kusanifisha maandishi yote ya Kiswahili na kuhakikisha kwamba nchi zote nne za Afrika Mashariki zinakuwa na mtindo mmoja wa uandishi. ii Kwa kadiri inavyowezekana kuhakikisha kwamba kunakuwa na mfanano wa kimsamiati kwenye vitabu na kamusi zinazotumika katika shule zote za Afrika Mashariki. iii. Kusimamia uchapishaji wa vitabu vya sarufi kwa lengo la kuhakikisha kwamba kuna uwiano wa sarufi kwa nchi zote za Afrika Mashariki. iv. Kuwatia moyo na kuwasaidia waandishi ambao Kiswahili ni lugha yao ya kwanza. v. Kutoa ushauri kwa waandishi tarajali kuhusu vitabu wanavyokusudia kuviandika. vi. Kupitia lugha ya vitabu vilivyokwisha kupata ithibati na vitabu vingine vilivyokwishachapishwa pale itakaoonekana kuna umuhimu wa kufanya hivyo. vii. Kuandaa orodha ya vitabu vya kiada na vya ziada vinavyopaswa kutumika kila mwaka. viii. Kuweka mkakati wa kutafsiri katika lugha ya Kiswahili vitabu vya kiada na vile vya ziada. ix. Kupitia na pale itakapobidi kusahihisha vitabu vilivyotafsiriwa katika lugha ya Kiswahili. x. Kupitia na kutoa ushauri juu ya vitabu vyote vinavyoshughulikiwa na Kamati. xi. Kuwapa taarifa waandishi wa vitabu kuhusu mbinu ya kufundishia katika nchi za Afrika Mashariki. xii. Kutoa majibu juu ya hoja zinazohusu lugha ya Kiswahili na maandishi yake. xiii. Kufanya jambo lolote litakalosaidia kufanikisha utekelezaji wa malengo ya Kamati. (ILC Bulletin Na. 16, pp. 5-6) Ukifuatilia mjadala huu mbali na mambo mengine kuna mambo mawili muhimu sana katika makala haya. Jambo la kwanza ni uwakilishi wa wajumbe wanaounda Kamati ya Lugha kwamba kuna uwakilishi sawa kutoka katika kila nchi mwanachama. Aidha, ingawa wawakilishi hawa wote walikuwa ni wageni kulikuwa na 105 uwakilishi wa makundi mbalimbali ikiwa ni pamoja na wizara yenye dhamana ya maendeleo ya lugha na elimu kwa ujumla. Jambo la pili ni kwamba miongoni mwa majukumu zaidi ya kumi yaliyoelekezwa kwenye kamati, jukumu la kwanza lilikuwa kusanifisha maandishi yote ya Kiswahili na kuhakikisha kwamba nchi zote nne za Afrika Mashariki zinakuwa na mtindo mmoja wa uandishi. Hali ilivyo sasa kama itakavyofafanuliwa katika sehemu zinazofuata ni tofauti kabisa kwani hakuna mtindo unaofanana sio tu katika Jumuiya ya Afrika Mashariki bali hata ndani ya nchi wanachama wa jumuiya hii. Sehemu inayofuata inajadili kwa mifano changamoto zinazoukabili mchakato wa usanifishaji wa Kiswahili katika Jumuiya ya Afrika Mashariki. Changamoto zinazoukabili usanifishaji wa Kiswahili Baada ya nchi za Afrika Mashariki kupata uhuru na kila nchi kuwa na sera zake kuhusu mchakato wa kukuza na kuendeleza lugha ya Kiswahili, umoja uliokuwepo katika usanifishaji wa lugha hii ukaanza kutetereka. Baada ya kutetereka kwa umoja uliokuwepo, usanifishaji wa Kiswahili katika Jumuiya ya Afrika Mashariki ukaanza kukabiliwa na changamoto nyingi. Katika sehemu hii tumejadili baadhi ya changamoto hizo. Hata hivyo mifano mingi imetolewa kutoka katika nchi ya Tanzania kutokana na tajriba aliyonayo mwandishi wa makala haya kuhusu asasi zinazohusika na ukuzaji wa Kiswahili nchini Tanzania. Zifuatazo ni baadhi ya changamoto hizo: Kwanza, kutokuwa na Asasi moja inayowaunganisha wataalamu wote wa lugha ya Kiswahili na kusimamia usanifishaji kwa nchi zote za Afrika Mashariki. Hali hii ni tofauti na ilivyokuwa wakati wa Kamati ya Lugha ya Afrika Mashariki, amabako Kamati ilikuwa na wajumbe ambao idadi yao ilikuwa na uwiano sawa kutoka katika nchi zote za Afrika Mashariki. Wajumbe hawa pia walipatikana kwa utaratibu unaofanana. Palikuwa na Mkurugenzi wa elimu, afisa mmoja wa Serikali na watu wengine wawili ambao si maafisa wa serikali. Katika mazingira kama haya lilikuwa jambo rahisi kwa msamiati unaosanifishwa kuwa na uwakilishi wa nchi zote. Vilevile ilikuwa rahisi kusimamia utekelezaji wa maazimio ya kamati, hasa maazimio yanayohusu uandishi wa vitabu pamoja na ufundishaji wa lugha ya Kiswahili. Urahisi huu ulitokana na kamati kuwa na mjumbe ambaye ndiye msimamizi mkuu wa masuala ya elimu na ambaye ofisi yake ndiyo inahusika na utoaji wa ithibati kwa vitabu vya kufundishia. 106 Mwaka 1939 lilitolewa pendekezo kwamba mjumbe mmoja kutoka katika kila nchi awe mtu ambaye lugha yake ya kwanza ni Kiswahili. Lengo ni kuwashirikisha wazungumzaji wazawa wa lugha ya Kiswahili katika usanifishaji kunarahisisha ukubalifu wa msamiati unaosanifishwa katika mazingira halisi ya matumizi ya lugha. Jambo hili lilifanyika kwa kuwa hapo awali wajumbe wote wa Kamati hawakuwa wazungumzaji wa lugha ya Kiswahili. Tunatambua kwamba kuwa hivi sasa kuna Kamisheni ya Kiswahili ya Afrika Mashariki. Hata hivyo, kamisheni hii ina majukumu lukuki ilihali watendaji ni wachache sana. Aidha, kamisheni hii haina uwakilishi unaofanana kama ilivyokuwa wakati wa Kamati ya Lugha ya Afrika Mashariki. Tunatambua pia kwamba kuna baadhi ya asasi zinazojishughulisha na ukuzaji na usanifishaji wa Kiswahili. Asasi hizo ni pamoja na Taasisi ya Taaluma za Kiswahili (TATAKI), Taasisi ya Kiswahili na Lugha za Kigeni (TAKILUKI), Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA) na Baraza la Kiswahili Zanzibar (BAKIZA). Hata hivyo majukumu ya asasi hizi katika ukuzaji wa Kiswahili ni ya Kitaifa zaidi na siyo ya Kimataifa kama ilivyokuwa wakati wa Kamati ya Lugha ya Afrika Mashariki. Taasisi ya Taaluma za Kiswahili inayosemekana kuwa ndiye mrithi wa kazi nyingi za iliyokuwa Kamati ya Lugha, haijaajiri watu kutoka nje ya Tanzania, japo katika baadhi ya majopo yake imekuwa ikiwashirikisha baadhi ya wataalamu kutoka nje ya Tanzania. Hoja ya kuziona shughuli za TATAKI kuwa ni za kitaifa zaidi kuliko kimataifa iliwahi kuelezwa pia na Mbaabu (2007) pale aliposema: ...shughuli za Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili7 , ambazo zinaendelea sana au zile zilizopangwa zinafanana sana na shughuli za Kamati ya Lugha iliyovunjika, isipokuwa kwamba ni za kitaifa zaidi kuliko kimataifa (uk. 131). Suala la kuzingatia hapa ni kwamba TATAKI ni Taasisi ambayo iko chini ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, hivyo hata uendeshaji wa shughuli zake likiwemo suala la ajira unatakiwa ufanyike kwa mujibu wa taratibu za Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Tatizo jingine linaloifanya TATAKI ishindwe kufanya majopo yanayowashirikisha 7 Kwa sasa Taasisi hii inaitwa Taasisi ya Taaluma za Kiswahili ( TATAKI) 107 wajumbe kutoka nje ya Tanzania kama ilivyokuwa ikifanya awali ni ukosefu wa fedha. Pili, ni kukinzana kimsimamo kwa wataalamu wa lugha kuhusu istilahi za Kiswahili. Mfano mmojawapo ni istilahi za utafiti. Baada ya TATAKI kuanzisha programu za Kiswahili, hasa programu za uzamili, kumeibuka mjadala kuhusu istilahi zinazopaswa kutumika katika uandishi wa tasnifu. Ukipitia tasnifu za wanafunzi wa uzamivu na umahiri8 utaona kuwa kuna visawe vingi katika matumizi ya istilahi kutokana na kila msimamizi kuwa na msimamo wake kuhusu istilahi ya Kiswahili inayopaswa kutumika. Ifuatayo ni mifano ya istilahi hizo na visawe vyake vya Kiingereza vimewekwa katika mabano. ikisiri/ufupisho(abstract),uthibitisho/ idhini (certification), marejeo/rejea/marejeleo (references), tatizo la utafiti/tamko la utafiti/tatizo la tamko la utafiti (statement of the problem), mapitio ya maandiko/mapitio na maandiko/pitio la maandiko/mapitio ya nyaraka mbalimbali (literature review). Suala la kuzingatia hapa ni kwamba, neno moja la Kiingereza kuwa na kisawe zaidi ya kimoja katika Kiswahili siyo jambo baya ila litakuwa jambo jema endapo kutakuwa na muafaka katika matumizi ya istilahi hizo. Pamekuwa pia na mjadala kuhusu matumizi ya neno shahada na digirii katika tasnifu za wanafunzi. Katika mjadala huu paliibuka (huenda mpaka sasa bado yako) makundi mawili ya wanataaluma. Kundi la kwanza ni wanataaluma waliodai kuwa neno digrii ndilo linalopaswa kutumika. Wanataaluma hawa wanajikita katika hoja kuu mbili. Hoja ya kwanza ni kuwa neno shahada tayari linatumiwa kwa maana ya cheti, wametoa mfano wa shahada ya ndoa, shahada ya mpiga kura n.k. Hivyo kwa mtazamo wa waumini wa kundi hili, kuendelea kulitumia neno hili kwa maana ya neno la Kiingereza “degree” ni sawa na kulibebesha majukumu mazito zaidi neno hili. Hoja ya pili wanayoitoa waumini wa kundi hili ni kwamba, kwa kuwa kwa muda mrefu kumekuwa na dhana kwamba Kiswahili ni Kiarabu kwa kuwa lugha hii ina matumizi makubwa ya maneno yenye asili ya Kiarabu, ni vema kadiri inavyowezekana tukapunguza matumizi 8 Neno hili linatumika kwa maana ya shahada ya pili. Mwandishi wa makala haya anatambua kwamba baadhi ya wataalamu hasa kutoka Kenya shahada hii wanaiita Uzamili 108 ya maneno yenye asili ya Kiarabu. Kwa minajili hiyo basi, wao wanaona kwamba ni vizuri tukatumia neno digrii badala ya shahada. Mwandishi wa makala haya anakubaliana na hoja ya waumini wa kundi la kwanza kwamba kadiri inavyowezekana ni vema tukapunguza matumizi ya maneno yenye asili ya kigeni katika lugha ya Kiswahili. Hata hivyo inamuwia vigumu kukubaliana nao katika uamuzi wa kuacha kutumia neno lenye asili ya lugha ya kigeni ( shahada) na kuamua kutumia neno jingine (diggrii) ambalo nalo pia asili yake ni lugha ya kigeni. Maneno haya yote mawili; digrii na shahada yanatokana na lugha za kigeni ambazo ni Kiingereza na Kiarabu. Kundi la pili, ni wanataaluma waliodai kuwa neno shahada ndilo linalopaswa kutumika, kwa hoja kuu mbili. Hoja ya kwanza ni kwamba tayari kuna neno stashahada lenye maana ya ngazi ya elimu iliyo chini ya shahada lakini kubwa kuliko cheti na ambalo tayari limo katika kamusi ya Kiswahili sanifu na tayari limekwishazoeleka. Hoja ya pili wanayoitoa waumini wa kundi hili ni kwamba hivi sasa lugha inayopambanishwa na Kiswahili katika nyanja mbalimbali ni Kiingereza. Miongoni mwa hoja wanazotumia watu wanaotetea matumizi ya Kiingereza dhidi ya Kiswahili ni kuwa lugha hii haina msamiati wa kutosha na kuwa msamiati mwingi unaotumika katika lugha ya Kiswahili umetoholewa kutoka katika lugha ya Kiingereza. Hivyo waumini wa kundi hili wanaona kuwa kuendelea kusisitiza matumizi ya maneno yenye asili ya Kiingereza ni sawa na kuendelea kuwapa nguvu wapinzani wa lugha ya Kiswahili. Waumini wa kundi la pili wanapingana na wenzao wa kundi la kwanza waliodai kwamba neno shahada halistahili kutumika kwa maana ya msingi ya cheti cha kitaaluma kwa kuwa tayari linatumiwa kwa maana nyingine kama shahada ya ndoa, shahada ya mpigakura nk. Badala yake wao wanaamini kwamba neno kuwa na manaa pana siyo sababu pekee ya kutufanya tuache kulitumia neno hilo. Wanaendelea kueleza kwamba hata neno digrii ukiliangalia katika kamusi ya Kiswahili sanifu, utabaini kwamba maana ya kwanza haihusu cheti cha kitaaluma bali inahusu masuala ya vipimo katika hesabu za maumbo au hali ya joto. Wakati mwingine wataalamu wa lugha wanatofautiana juu ya namna ya kushughulikia tahajia ya maneno yaliyotoholewa kutoka 109 katika lugha za kigeni. Kuna wanaodai kwamba ni vema maneno hayo yakaandikwa kwa kuzingatia namna yanavyotamkwa, na wengine msimamo wao ni kwamba maneno hayo sharti yaandikwe kwa kuzingatia namna yanavyoandikwa. Wanaojikita katika kundi la pili wanadai kwamba ni vigumu kuzingatia kigezo cha namna neno linavyotamkwa kwani kunaweza kuwa na tofauti ya utamkaji baina ya mtu mmoja na mwingine au watu wa taifa moja na jingine. Mwandishi wa makala haya alifanya mahojiano na mwanataaluma mmoja aliyeshiriki kikamilifu katika utunzi wa kamusi ya Biolojia, Fizikia, na Kemia ambaye alieleza kwamba wakati wa uandishi wa kamusi hii, wao walizingatia zaidi namna neno linavyotamkwa katika lugha ya asili. Hata hivyo alisisitiza kwamba, kwa kuwa walikuwa na wataalamu wa nyanja zote tatu, matamshi yaliyozingatiwa hapa ni yale ya lugha ya asili ambako neno hilo limetokea. Ukifuatilia kwa kina mjadala tulioueleza hasa kuhusu matumizi ya neno shahada na digrii utabaini kuwa kuna sababu mbalimbali zinazowafanya wakuzaji wa istilahi za Kiswahili kutoafikiana katika matumizi ya baadhi ya istilahi. Miongoni mwa sababu hizo ni raghba waliyonayo kuhusu lugha za kigeni hasa Kiingereza na Kiarabu. Katika mfano wa neno digrii na shahada tulioutoa hapo juu, ni dhahiri shahiri kwamba kila kundi limekuwa na msimamo wa kutetea neno lake pamoja na mambo mengine kwa kueleza kwamba neno jingine halifai kwa kuwa kulikubali neno hilo kutaifanya lugha ya Kiswahili iwe na maneno mengi yenye asili ya lugha hiyo. Mvutano huo unaashiria wazi kwamba wataalamu hawa kila mmoja ana utashi na lugha mojawapo kati ya Kiingereza au Kiarabu. Hata hivyo mwandishi wa makala haya anatambua kwamba katika Taasisi ya Taaluma za Kiswahili, juhudi za kuunda na hatimaye kusanifisha istilahi za utafiti zimekwishaanza, matokeo ya juhudi hizi huenda yakasaidia katika kutatua tatizo la kukosekana kwa muafaka katika matumizi ya istilahi katika uwanja huu. Hoja ya msingi ya kuzingatia hapa ni kwamba ingawa mchakato huu unaratibiwa na TATAKI kuna umuhimu wa kufikiria namna ya kushirikisha wataalamu wengine sio tu nje ya TATAKI bali nje ya Tanzania ambao kwa namna moja ama nyingine istilahi hizi zinaweza kuwahusu. Ikumbukwe kwamba tasnifu za wanafunzi wa TATAKI kama zilivyo tasnifu za wanafunzi wengine, baada ya kumalizika hupelekwa kwa watahini wa nje ambao aghalabu wanatoka nje ya Tanzania. Hivyo 110 kukosekana kwa muafaka wa pamoja katika matumizi ya istilahi kunaweza kukasababisha mpishano mkubwa wa kimtazamo kati ya wanafunzi, watahini wa ndani na watahini wa nje. Tatu, ni changamoto ya kutokushirikishwa kwa wazungumzaji wa lahaja za Kiswahili. Baada ya kuanzishwa kwa Kamati ya lugha na kupewa pamoja na mambo mengine jukumu la kusimamia usanifishaji wa lugha ya Kiswahili, wajumbe wa Kamati walijiwekea mikakati ya kutekeleza majukumu yake ikiwa ni pamoja na kupokea maoni kutoka kwa wadau wa lugha ya Kiswahili. Katika kutekeleza majukumu yake, Kamati ilishauriwa kuzitumia ipasavyo lahaja nyingine za Kiswahili ili kuhakikisha kuwa usanifishaji na ukuzaji wa Kiswahili unawashirikisha wazungumzaji wengi wa Kiswahili kadiri inavyowezekana. Kutokana na hali hiyo, utafiti katika lahaja za Kiswahili ulitakiwa kupewa msisitizo wa hali ya juu (Whiteley, 1969). Akiunga mkono hoja ya kufanya utafiti katika lahaja za Kiswahili, Temu, (1980) anasema Kwa kuchunguza kwa makini lahaja za Kiswahili tunagundua maneno mengi ambayo hayatumiki katika Kiswahili sanifu na ambayo hayamo katika orodha ya msamiati na wala hayamo katika kamusi (uk. 7). Pamoja na kutolewa mapendekezo juu ya namna ya kukuza Kiswahili sanifu kwa kutumia lahaja nyinginezo za Kiswahili, baada ya nchi za Afrika Mashariki kupata uhuru, kila nchi ikawa na sera zake kuhusu lugha ya Kiswahili. Nchini Tanzania, mbali na kuwa na Chuo cha Uchunguzi wa Lugha ya Kiswahili,9 liliundwa pia Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA) kwa Sheria ya Bunge na. 27 ya mwaka 1967. Baraza hili lilipewa jukumu la kusimamia na kuhakiki shughuli zote za ukuzaji, uendelezaji na usanifishaji wa lugha ya Kiswahili nchini Tanzania. Baraza pia lilipewa mamlaka ya kutoa muhuri wa ithibati kwa kazi mbalimbali zilizoandikwa kwa Kiswahili nchini Tanzania. 9 Chuo hiki ni matokeo ya mabadiliko ya jina la iliyokuwa Kamati ya Lugha ya Afrika Mashariki yaliyofanyika mwaka 1964. Baada miaka sita, (yaani mwaka 1970), Chuo hiki kikabadili tena jina na kuwa Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili (TUKI), na mnamo mwaka 2009 Taasisi hii ikaungana na iliyokuwa Idara ya Kiswahili ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na kuitwa Taasisi ya Taaluma za Kiswahili (TATAKI). 111 Katika kutekeleza jukumu la kukuza msamiati wa Kiswahili sanifu, Chiraghdin na Mnyampala (1977, p. 64) wakashauri kuwa ingefaa msamiati wa Kiswahili sanifu ukuzwe kwanza kwa kutafutiwa maneno kutoka kwenye Kiswahili chenyewe, yaani lahaja mbalimbali za Kiswahili, kisha ndipo utafutwe kutoka kwenye lugha nyingine za Kibantu, lugha za Kiafrika kwa ujumla, na baadaye lugha nyingine nje ya Afrika. Likitoa maelekezo ya namna ya kuunda msamiati na istilahi za Kiswahili, BAKITA (1982) liliweka bayana misingi ambayo ilifuata mapendekezo yaliyotolewa na Chiraghdin na Mnyampala (1977, p. 64) (taz. KAKULU, 1982, p. 16). Misingi hiyo ni: a) kuanza kwa kuchunguza lahaja mbalimbali za Kiswahili, b) kuangalia lugha za Kibantu, c) kuchunguza lugha za Kiafrika, na kama itakuwa imeshindikana, d) kuangalia lugha nyingine nje ya Afrika. Pamoja na mapendekezo yaliyotolewa na Chiraghdin na Mnyampala (1977, p. 64) na misingi iliyobainishwa na BAKITA kuhusu uundaji wa msamiati na istilahi za Kiswahili, bado lahaja za Kiswahili hazijatumika ipasavyo katika mchakato huu. Wakithibitisha hoja hii, Mwansoko na Masabo (1992, p. 22) wanaeleza kuwa, licha ya kuwa na mwongozo wa namna bora ya kuunda istilahi za Kiswahili, lahaja za Kiswahili hazijatumiwa kikamilifu kama ilivyoelekezwa, kwa kuwa msamiati mwingi uliomo katika lahaja hizi haujafanyiwa utafiti wa kina. Matokeo yake ni kuwa msamiati mwingi uliomo katika Kiswahili sanifu unatoholewa kutoka katika lugha za kigeni ilihali Kiswahili chenyewe kinaweza kujiimarisha kimsamiati kupitia katika lahaja zake anuwai. Nne, kasi ya usanifishaji kutoendana na mfumuko wa istilahi. Pamoja na tatizo la kutokuwa na asasi ya pamoja ya kimataifa inayoratibu usanifishaji wa Kiswahili Afrika Mashariki, bado kuna tatizo hata katika hizi asasi za kitaifa kushindwa kufanya kazi zake kulingana na kasi ya ukuaji wa istilahi. Katika Taasisi ya Taaluma za Kiswahili kwa mfano, kuna kituo cha Istilahi, Tafsiri na Ukalimani na katika Baraza la Kiswahili la Taifa, kuna Kamati ya Kusanifisha Lugha. Tulitegemea kwamba vitengo hivi vifanye kazi ya kuunda istilahi kwa kasi hasa tukizingatia kwamba kuna mfumuko mkubwa wa istilahi hasa istilahi zinazotokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia. 112 Hata hivyo hali ni tofauti kabisa kwani kwa muda mrefu sasa hapajawa na mchakato wowote wa kusanifisha istilahi za Kiswahili, hususani kwa BAKITA lenye mamlaka ya kusimamia maendeleo ya lugha ya Kiswahili nchini Tanzania. Tatizo kubwa linaloelezewa kuwa ni sababu ya kutofanikiwa kwa majukumu haya ni uhaba wa fedha. Matokeo yake ni kwamba wazungumzaji wa lugha huamua kutumia istilahi kama zinavyotumika katika lugha za kigeni hasa Kiingereza. Unapofika wakati wataalamu wa asasi za kukuza lugha wakakaa na kuunda istilahi mbadala huwa vigumu kwa istilahi hizo kukubalika kwa watumiaji wake, hivyo istilahi hizo hubakia kuhifadhiwa katika mashubaka. Mfano wa istilahi hizo ambazo istilahi mbadala ziko kwenye mabano ni televisheni(runinga), kalkuleta(kikokotozi), feni(pangaboi), friji(jokofu) es-em-es(sms) (ujumbe mfupi) n.k. Miezi kadhaa iliyopita paliibuka majadala kuhusu matumizi ya neno king’amuzi kwa maana ya “ decorder” ambalo lilikwishazoeleka kwa watumiaji wengi wa Kiswahili. Baada ya BAKIZA wakatoa hoja kuwa neno muafaka ni kisimbuzi kutokana na hoja kwamba kifaa hiki kinafanya kazi ya kusimbua. Pamoja na hoja nzuri inayotolewa na BAKITA kuhusu matumizi ya neno kisimbuzi, hoja hii haikuja wakati muafaka kwani wazungumzaji wameachwa kwa muda mrefu wakitumia neno king’amuzi hadi likazoeleka kwa wazungumzaji wengi wa Kiswahili. Tukiruhusu hali hii iendelee, utafika wakati utaibuka mjadala mwingine kwamba Kiswahili asili yake ni Kiingereza kwa kuwa kitakuwa kimesheheni istilahi za Kiingereza. Baadhi ya watu pia wanaweza kuja na hoja kwamba lugha hii ni lugha isiyo na wenyewe kwani msamiati wake kwa kiasi kikubwa umetokana na lugha za kigeni. Tano, kuna tofauti ya matumizi ya lugha baina ya jamii moja na nyingine. Licha ya tofauti ya mitazamo ya wataalamu wa Kiswahili kuhusu usanifishaji wa Kiswahili kama tulivyoeleza hapo juu, kuna tofauti pia ya matumizi ya lugha baina ya nchi moja na nyingine au jamii moja na nyingine ndani ya nchi moja. Hivi sasa kumekuwa na juhudi kubwa ya kuchapisha vitabu vya lugha ya Kiswahili pamoja na kamusi za jumla na zile za nyanja maalumu. Hili ni jambo jema kabisa ambalo linahitaji pongezi. Hata hivyo, ukipitia kwa mfano, vitabu na kamusi zilizochapishwa Kenya na Tanzania unaweza kujionea tofauti za kiistilahi baina ya waandishi wa nchi hizi. Ikumbukwe kwamba vitabu hivi vinatumiwa na wanafunzi wetu wa shule za msingi, sekondari na vyuo vikuu. Hivyo kuna umuhimu wa 113 kuwa na namna bora ya kusanifisha istilahi hizi ili tuweze kuwasaidia wanafunzi wetu. Nchini Tanzania pia kuna tofauti ya matumizi ya baadhi ya maneno kati ya Tanzania bara na Zanzibar. Ukichunguza matumizi ya maneno kama mfereji, tungule, hoho, nyanyamshumaa na mengine mengi utagundua kwamba maana za maneno hayo ni tofauti kati ya Tanzania bara na Zanzibar. Mara nyingi wataalamu wa Kiswahili wa Tanzania bara hukuza Kiswahili kwa kutumia lugha za Kibantu kwani wengi wao hizo ndizo lugha zao za kwanza. Kwa upande wa Zanzibar, kwa kuwa watu wanaohusika na ukuzaji wa Kiswahili walio wengi lugha zao za kwanza ndio hizi tunazoziita lahaja za Kiswahili, msamiati wao mwingi unatokana na lahaja hizi. Aidha, kuanzishwa kwa Baraza la Kiswahili Zanzibar licha ya kuwa na Baraza la Kiswahili la Taifa, ni ishara kwamba kuna tofauti ya kimtazamo kati ya Kiswahili cha Tanzania bara na Zanzibar. Hoja ya msingi inayoelezwa kuwa ni sababu mojawapo ya kuwa na mabaraza mawili ndani ya nchi moja ni kuwa utamaduni, siyo sehemu ya masuala ya Muungano. Hata hivyo kuanzishwa kwa Baraza la Kiswahili Zanzibar kumeibua hamasa katika utafiti wa lahaja, hasa lahaja zilizoko katika kisiwa cha Zanzibar. Hivi sasa BAKIZA wamekwishafanya utafiti na kuandika kamusi katika lahaja za Kimakunduchi, Kipemba na Kitumbatu. Huu ni mfano mzuri wa kuigwa na asasi nyingine zinazojihusisha na ukuzaji wa lugha ya Kiswahili. Sita, asasi nyingi zinazohusika na usanifishaji wa Kiswahili ziko mijini. Ukuzaji na Usanifishaji wa lugha yoyote ni jambo linalowahusu watu wote, wakiwemo watu wanaoishi maeneo ya vijijini. Hata hivyo, vyombo vingi vinavyohusika na ukuzaji na usanifishaji wa lugha ya Kiswahili viko mijini. Ni mara chache sana wataalamu wa lugha kutoka katika asasi hizi wanawatembelea watu wanaoishi vijijini. Wakati mwingine hata matokeo ya kazi za utafiti wa asasi hizi huishia mijini. Nchini Tanzania kwa mfano ni watu wachache sana waishio vijijini walio na welewa wa asasi zinazojishughulisha na ukuzaji na uendelezaji wa lugha ya Kiswahili. Mfano mzuri ni Taasisi ya Taaluma za Kiswahili, ambayo ni matokeo ya muungano wa iliyokuwa Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili na Idara ya Kiswahili. Katika shule nyingi za vijijini alizozitembelea 114 mwandishi wa makala haya bado kuna wanafunzi wengi na baadhi ya walimu hawana welewa kuhusu muundo mpya wa Taasisi hii. Mwandishi ameshuhudia baadhi ya walimu wakiwafundisha wanafunzi kuhusu asasi zinazohusika na ukuzaji na uendelezaji wa Kiswahili kuwa ni pamoja na TUKI na Idara ya Kiswahili ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Walimu hawa walipoulizwa endapo wana taarifa yoyote kuhusu muunganiko wa asasi hizi na kuunda Taasisi moja, wengi wao walionesha kutokuwa na taarifa. Tukumbuke kwamba TATAKI hivi sasa imeshatimiza miaka mitatu, na hawa ni walimu wa Kiswahili lakini bado taarifa za kuundwa kwake hazijawafikia, vipi kuhusu watu wengine ambao hawako katika sekta ya elimu? Vilevile, Baraza la Kiswahili la Taifa ambalo lina jukumu la kuratibu na kusimamia maendeleo ya kiswahili nchi nzima nalo shughuli zake kwa kiasi kikubwa zinafanyikia mjini. Hata hivyo, ingawa asasi zinazojishughulisha na ukuzaji wa Kiswahili ziko mijini na shughuli zake kama semina na makongamano vyote vinafanyikia mijini, bado pia kuna idadi kubwa ya wakazi wa mijini ambao hawana welewa wa michango ya asasi hizi. Kwa mfano (Nchimbi 2005, p. 205) anaeleza kwamba asilimia sabini (70%) ya wafanyakazi aliowafanyia mahojiano kutoka shirika la Posta na hospitali za Dar es Salaam, walionesha kwamba hawafahamu mchango wa TUKI katika ukuzaji na uendelezaji wa lugha ya Kiswahili. Kwa maelezo haya ni dhahiri kwamba watu hawa hawana welewa wowote juu ya Taasisi hii na majukumu yake. Saba, kuna changamoto nyingine ya asasi za Kiswahili kutokuwa na nguvu za Kisheria. Ni jambo la kawaida kwa wanajamii kufanya kazi kwa mujibu wa sheria hasa ikiwa wanafahamu wazi kwamba kutokuzingatia sheria hizo kunaweza kuwaingiza hatiani. Nchini Tanzania kwa mfano, kuna Baraza la Sanaa (BASATA) lililoanzishwa kwa sheria Na. 23 ya mwaka 1984 ambalo pamoja na mambo mengine limepewa mamlaka ya kisheria ya kusimamia ubora wa filamu nchini Tanzania. Kwa mamlaka waliyopewa BASATA wana uwezo wa kuzifungia filamu ambazo zinaonekana kwenda kinyume na maadili ya mtanzania. Kwa upande wa lugha ya Kiswahili, hali ni tofauti kabisa kwani licha ya kuanzishwa kwa Baraza la Kiswahili la Taifa kwa sheria ya bunge 115 Na. 27 ya mwaka 1977, bado Baraza halina nguvu ya kisheria ya kuvifungia vyombo vinavyobananga matumizi ya Kiswahili sanifu. Jambo la kusikitisha zaidi ni kwamba hata katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tuliyonayo hivi sasa haisemi chochote kuhusu nafasi ya lugha ya Kiswahili Tanzania. Mwandishi wa makala haya anakiri kwamba yametolewa matamko mengi na viongozi waandamizi wa serikali yenye lengo la kuhakikisha kwamba matumizi bora ya lugha ya Kiswahili yanazingatiwa katika sekta mbalimbali nchini Tanzania. Mfano mmojawapo ni tamko la Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Mh. George Mkuchika alilolitoa tarehe 19/04/2010. Katika tamko hilo, mbali na mambo mengine, Mh. Waziri alivitaka vyombo vya habari vinavyotumia lugha ya Kiswahili vihakikishe kwamba vinatumia Kiswahili sanifu na mwanana, huku vikizingatia kwa dhati sarufi ya Kiswahili. Pamoja maelekezo mazuri na yenye kutia faraja yaliyotolewa na waziri Mkuchika kuhusu lugha ya Kiswahili, bado maelekezo hayo yanabaki katika maandishi kwa kuwa hakuna chombo chenye mamlaka ya kisheria ya kusimamia matumizi ya lugha ya Kiswahili ambacho kinaweza kuwachukulia hatua za kisheria watu watakaokiuka maelekezo hayo. Hivi sasa kuna vyombo vingi vya habari vinavyobananga matumizi ya Kiswahili sanifu na wanachotakiwa kufanya watu wa BAKITA ni kuviandikia barua na kuvishauri kuhusu matumizi bora ya Kiswahili sanifu. Hata hivyo BAKITA hawana mamlaka ya kuvichukulia hatua vyombo vya habari vitakavyokwenda kinyume na maelekezo wanayopewa kuhusu matumizi ya Kiswahili sanifu. Ni katika mazingira kama hayo ndipo unapokuta magazeti ya Kiswahili yakiandikwa kwa sarufi ya Kiingereza. Mfano mmojawapo ni sentensi inayotaja kiwango cha fedha kama vile 10 milioni, 50 elfu n.k. Jambo la ajabu ni kwamba katika uanishaji mwingine wa namba hawafuati kanuni hii. Si rahisi kwa mfano kukuta gazeti limeandika 10 watu, 500 watoto n.k. Wakati mwingine waandishi wa habari hufanya tafsiri sissi katika kazi zao na hivyo kupotosha maana ya msingi. Mfano maneno kituo cha kati cha polisi badala ya kituo kikuu cha polisi yaliyotafsiriwa kutoka katika maneno ya Kiingereza Central police station. 116 Mapendekezo ya namna ya kukabiliana na changamoto Baada ya kuainisha baadhi ya matatizo yanayolikabili zoezi la usanifishaji wa Kiswahili katika nchi za Afrika Mashariki, mwandishi wa makala haya anaamini kwamba itakuwa ni vizuri zaidi ikiwa atapendekeza baadhi ya mbinu zinazoweza kutumika ili kutatua matatizo yaliyoainishwa hapo juu. Zifuatazo ni baadhi ya mbinu hizo: Kwanza, kuundwe chombo kimoja kitakachosimamia jukumu la kukuza na kusanifisha lugha ya Kiswahili, kwa nchi zote za Afrika Mashariki. Chombo hiki kiwe na uwakilishi kutoka katika kila nchi. Wajumbe hawa ni vema pia wakazingatia uwakilishi wa sekta mbalimbali ikiwemo sekta inayohusika na utungaji wa sera. Kama ilivyopendekezwa mwaka 1939 wakati wa Kamati ya Lugha ya Afrika Mashariki, ni vema pia Kamati ikawa na wajumbe ambao ni wazawa wa lugha ya Kiswahili watakaopatikana kupitia katika lahaja anwai za Kiswahili. Wajumbe wa chombo hiki wawe wanakutana mara kwa mara ili kuunda istilahi mpya na kuzisanifisha ili kuendana na kasi ya uibukaji wa istilahi unaotokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia. Tunatambua kwamba kuna Kamisheni ya Kiswahili ya Afrika Mashariki, hata hivyo kama ilivyokwishaelezwa katika sehemu iliyotangulia kamisheni hii ina majukumu mengi sana ilihali watendaji wake ni wachache sana. Aidha, kamisheni haina uwakilishi kama ilivyokuwa wakati wa Kamati ya Lugha. Hivyo, sisi kama wataalamu wa lugha ya Kiswahili tuna dhima ya kuhakikisha kwamba Kamisheni hii pamoja na mambo mengine inasimamia kwa dhati jukumu la ukuzaji na usanifishaji wa lugha ya Kiswahili. Hata hivyo, kwa kuwa kila nchi ina sera zake kuhusu lugha ya Kiswahili ni vema pakawa na chombo kitakachosimamia ukuzaji na usanifishaji wa lugha ya Kiswahili katika nchi hiyo. Wajumbe kutoka katika vyombo hivi ndio waungane na kuunda chombo kimoja kitakachosimamia usanifishaji wa pamoja katika nchi zote za Afrika Mashariki. Pili, kwa kuwa katiba inayopendekezwa inakitambua Kiswahili kuwa ni lugha na tunu ya taifa ni vema mabaraza yaliyopewa jukumu la kusimamia maendeleo ya Kiswahili yakapewa nguvu ya kisheria ya kusimamia matumizi ya Kiswahili nchini Tanzania. 117 Juhudi kama hizi zifanywe pia katika nchi nyingine za Afrika Mashariki ili kuwe na usawa katika ukuzaji na usanifishaji wa lugha ya Kiswahili. Tunatambua kwamba katiba mpya ya nchi ya Kenya imetamka wazi kwamba Kiswahili ni lugha ya Taifa katika nchi hiyo. Tunatambua pia kwamba serikali ya Rwanda imetangaza Kiswahili kuwa miongoni mwa lugha rasmi nchini Rwanda. Tatu, uudaji na usanifishaji wa istilahi katika lugha ya Kiswahili ni vema ukafanywa kwa kufuata mapendekezo yaliyotolewa na wataalamu na wadau wa lugha ya Kiswahili na kusisitiza kuanza kwa kuchunguza lahaja za Kiswahili, lugha ya Kibantu, lugha za Kiafrika na kama itakuwa imeshindikana ndipo tutohoe maneno kutoka katika lugha za kigeni. Ili utaratibu huu uweze kufuatwa, utafiti katika lahaja za Kiswahili unatakiwa kufanywa kuwa ni zoezi endelevu. Kwa mujibu wa utafiti alioufanya mwandishi wa makala haya katika lahaja za Kiswahili zilizoko katika kisiwa cha Zanzibar, lugha ya Kiswahili bado ina fursa kubwa sana ya kuendelea endapo lahaja hizi zitatumika ipasavyo. Kwa kufanya hivyo, tutaondoa dhana kwamba lugha hii ni tegemezi kwa lugha za kigeni hasa katika kipengele cha msamiati. Mwandishi wa makala haya anatambua kwamba kuna orodha kubwa ya msamiati uliokusanywa katika utafiti wa lugha za Tanzania hususani lugha za Kibantu, ulioratibiwa na Mradi wa Lugha za Tanzania. Msamiati huo unaweza kutumiwa pia wakati wa kukusanya na kusanifisha istilahi za Kiswahili ili kuhakikisha kwamba lugha hii inakuwa kwa kuzingatia misingi ya lugha za Kibatu na lugha nyinginezo za Kiafrika kabla ya kukimbilia katika lugha za kigeni. Nne, asasi zinazojishughulisha na ukuzaji na usanifishaji wa lugha ya Kiswahili zinatakiwa zibuni mbinu mbadala za kujipatia vipato ili ziweze kufanya kazi zake kwa ufanisi, kwani tatizo kubwa linalizikabili asasi hizi ni uhaba wa fedha. Vitengo vinavyohusika na ukuzaji na usanifishaji wa istilahi katika asasi hizi ni vema pia vikakaa pamoja na kujadiliana namna ya kufanya shughuli hii kwa pamoja na kwa ufanisi. Mfano mzuri ni Taasisi ya Taaluma za Kiswahili ambayo kwa kiasi kikubwa gharama za uendeshaji wake zinategemea kazi zinazofanywa na wanataaluma na waendeshaji wa Taasisi. Baadhi yetu tunafahamu kwamba, licha ya hali ngumu 118 ya kifedha lakini TATAKI wamekuwa wakifadhili shughuli mbalimbali zinazofanywa kwa lengo la kukuza na kuendeleza Kiswahili ndani na nje ya nchi ya Tanzania. Licha ya hali ngumu ya kifedha inayozikabili asasi za kukuza Kiswahili, ni vema asasi hizi zikashirikisha mashirika mbalimbali ya ndani na nje ya nchi kuandaa makongamano kwa wadau wa lugha ya Kiswahili hasa waandishi wa habari kwa lengo la kuelimishana juu ya umuhimu wa kuzingatia matumizi ya Kiswahili sanifu. Fursa ya makongamano hayo pia itumike kwa ajili ya kutangaza istilahi zinazoundwa na kusanifishwa na asasi hizi. Tano, Mwandishi wa makala haya anatambua kwamba kuna tofauti za kimtazamo kuhusu istilahi za Kiswahili zinazopaswa kutumika katika nyanja mbalimbali. Hata hivyo ufike wakati kwa wadau wote wa Kiswahili kukaa pamoja na kuafikiana kwa hoja kuntu kuhusu istilahi zinazopaswa kutumika katika nyanja hizo. Pale itakapobidi baadhi ya istilahi zinaweza kuwa na kisawe zaidi ya kimoja ili kuhakikisha kwamba istilahi zinazosanifishwa zinaakisi vema dhana iliyokusudiwa. Sita, asasi zilizoundwa na kupewa majukumu ya Kitaifa ya kusimamia maendeleo ya Kiswahili ni vema zikatafuta namna ya kushirikiana na wizara zinazohusika katika kusimamia utekelezaji wa matamko yanayotolewa na viongozi waandamizi wa serikali kuhusu matumizi ya lugha ya Kiswahili nchini. Saba, kadiri inavyowezekana uandishi wa kazi na hasa kamusi mbalimbali zinazotumika kufundishia katika shule zetu ni vema ukawashirikisha wataalamu wa lugha na nyanja zinazohusika ikiwa ni kamusi ya uwanja maalumu kutoka katika nchi zote za Afrika mashariki. Mfano mzuri ni kamusi ya Kiswahili sanifu na kamusi ya Biolojia, Fizikia na Kemia ambazo zimewashirikishwa wataalamu kutoka ndani na nje ya Tanzania. Hitimisho Makala haya yamejadili kwa muhtasari kuhusu usanifishaji wa lugha ya Kiswahili Afrika Mashariki, na matatizo yake na kupendekeza mbinu za utatuzi wa matatizo hayo. Kwa kiasi kikubwa asasi zilizojadiliwa na mifano iliyotolewa imetoka katika nchi ya Tanzania. Hata hivyo tunatambua kwa dhati juhudi zinazofanywa na asasi 119 zinazosimamia matumizi ya Kiswahili ndani na nje ya nchi ya Tanzania. Ili kushadidia hoja hii nitataja japo kwa muhtasari mafanikio ya asasi tatu zinazosimamia maendeleo ya Kiswahili nchini Tanzania. Asasi hizo ni TATAKI, BAKITA na BAKIZA. Tukianza na TATAKI, Taasisi hii hadi sasa imefanya mambo mengi na makubwa katika maendeleo ya lugha ya Kiswahili, imeendesha makongamano mbalimbali na hivi sasa Taasisi inaandaa wataalamu katika ngazi za shahada ya kwanza, umahiri na uzamivu. Taasisi pia inaandika na kuchapisha vitabu na kamusi mbalimbali. Hizi ni juhudi kubwa zinazostahili pongezi. Baraza la Kiswahili la Taifa, kwa upande wake limeandika vitabu mbalimbali kikiwemo kitabu cha Istilahi za Kiswahili na kitabu cha mwongozo kwa waandishi wa Kiswahili. Tunatambua kwamba hivi sasa, Baraza lina miswada ya kazi mbalimbali ikiwemo kamusi ya diplomasia na kitabu cha ufundishaji wa Kiswahili kwa wageni ambavyo viko mbioni kuchapishwa. Baada ya kukaa katika majengo ya kukodi kwa muda mrefu, majengo ambayo hayaendani na hadhi yake, Baraza limefanikiwa kupata majengo yake, yenye nafasi ya kutosha ambapo sasa litaweza kubuni miradi ya kujiendeleza na kujipanua. Hizi pia ni juhudi za aina yake ambazo haziwezi kubezwa hata kidogo. Kwa upande wa Baraza la Kiswahili Zanzibar, nalo pia limefanya mambo mengi na makubwa yenye lengo la kukuza na kuendeleza lugha ya Kiswahili. Miongoni mwa mambo hayo ni uandishi wa “Kamusi la Kiswahili Fasaha” Kamusi hii imeibua hamasa kwa wanataaluma na watafiti wa lugha kujifunza tofauti zilizopo kati ya Kiswahili cha Zanzibar na Kiswahili cha Tanzania bara. Baraza pia limefanya utafiti na kuandika kamusi za lahaja ya Kipemba, Kimakunduchi na Kitumbatu. Hivyo ile hofu kwamba lahaja haziwezi kushirikishwa kwa kuwa hazijafanyiwa utafiti wa kina hivi sasa imekwishapata ufumbuzi. 120 Marejeo Chiraghdin, N. & M. Mnyampala (1977). Historia ya Kiswahili. Nairobi: Oxford University Press KAKULU. ( 1982). Kamati ya Kusanifu Lugha: Misingi ya Uundaji wa Istilahi za Kiswahili. Dar es Salaam: Baraza la Kiswahili la Taifa Kiango, J. G. (2002), “Nafasi ya Kiswahili Katika Ujenzi wa Jamii Mpya ya Afrika Mashariki”, Nordic Journal of African Studies, 11(2) 185-197 Massamba, D. P. B (1989b). An assessment of the development and modernization of the Kiswahili language in Tanzania. Language Adaptation. Cambridge, UK: Cambridge University Press Massamba, D. P. B (2005). Ushirikiano: Muhimili wa TUKI katika Kukuza na Kuendeleza Kiswahili. Kiswahili: Jarida la Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili. Massamba, D. P. B (2007). Kiswahili origins and the Bantu divergence – Convergence theory. Dar es Salaam: Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili, 68, 29-41 Mkude, D. J. (2005). The passive construction in Swahili. Tokyo: Research Institute for Languages and Cultures of Asia and Africa Mulokozi, M. M. (2005). Miaka 75 ya Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili (1930-2005). Kiswahili: Jarida la Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili, 68, 1-28 Mwansoko, H. na Z. Masabo ( 1992). Kiongozi cha Uundaji wa Istilahi za Kiswahili, Dar es Salaam: Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili Nchimbi, F.A (2005). Mchango wa TUKI katika ukuzaji na Uendelezaji wa Kiswahili Tanzania na Mustakabali wake: Mtazamo wa watumiaji wa Kiswahili. Kiswahili: Jarida la Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili. 121 Nurse, D na T. Spear (1985), The Swahili: Reconstructing the history and language of an African society, 800-1500, Philadelphia: University of Pennsylvania Press Temu, C. W. (1980), Lahaja za Kiswahili: Muswada wa Ripoti ya Mwanzo ya Mradi wa Lahaja, Dar es Salaam: Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili. TUKI, (2013), Kamusi ya Kiswahili Sanifu (Toleo la Tatu). Nairobi: Oxford University Press. Whiteley, W. (1969), Swahili: The rise of a national language, London: Methuen & Co. Ltd


18 Jul 2023

8 Jul 2023

29 Jun 2022

14 Jun 2022

20 Apr 2022

 

 

SSP HIGH SCHOOL

MTIHANI WA MWEZI – KIDATO CHA PILI

KISWAHILI

Muda: Masaa 2:30                                               Tuesday 15 Feb 2022.

MAAGIZO KWA WATAHANIWA

1.   Mtihani huu una sehemu kuu TANO (5), A, B, C, D na E.

2.   Jibu maswali YOTE kutoka kila sehemu.

3.   Zingatia maelekezo ya kila swali.

4.   Simu za mkononi haziruhusiwi katika chumba cha mtihani.

5.   Andika jina lako  katika kila ukurasa wa kijitabu chako cha kujibia.

 

KWA MATUMIZI YA USAHIHISHAJI

NAMBARI YA SWALI

ALAMA

SAINI

1.    

 

 

2.    

 

 

3.    

 

 

4.    

 

 

5.    

 

 

6.    

 

 

JUMLA

 

 

 

 

Mtihani huu una kurasa 10 zenye maandishi.

 

SEHEMU A (Alama 25)

 UFAHAMU NA UFUPISHO

1.    Soma habari ifuatayo kisha jibu maswali yanayofuata.

Miti ina faida nyingi sana kwa binadamu. Miti husitiri nchi kama vile nguo inavyomsitiri binadamu. Nchi isiyokuwa na miti ni sawa na mtu ambaye amevuliwa nguo.

 

Kuongezeka kwa idadi ya watu na kutokuwepo kwa nishati mbadala kama vile gesi na umeme mijini na vijijini kumesababisha kuwepo kwa matumizi lukuki ya kuni na mikaa katika shughuli za binadamu za kujikimu. Hali hii imesababisha baadhi ya sehemu za nchi kugeuka jangwa. Matukio ya uhaba wa mvua na upungufu wa maji kwenye mito na mabwawa yamejitokeza miaka ya hivi karibuni.

 

Viongozi wa nchi yetu waliliona hili mapema ndio maana walianzisha kampeni za kuhimiza upandaji miti kwa kupitia vyombo vya habari. Kulikuwa na: “kata mti panda mti mmoja, panda miti miwili na hata kukataza kabisa ukataji wa miti”. Lakini utekelezaji haujawahi kuwa na mafanikio kwa asilimia mia moja.

 

Hata hivyo ni muhimu kuendelea kuelimisha umma kuhusu umuhimu wa utunzaji wa mazingira kwani kama wasemavyo waswahili: “usipoziba ufa utajenga ukuta”. Ni muhimu ifike mahali mmoja wetu atambue kuwa miti au misitu ni roho ya taifa.

 

Binadamu hunufaika na miti kwa njia nyingi. Watu wengine hupikia kuni au mikaa na wengine hujengea miti. Watu wengine hupasua miti mikubwa na kupata mbao ambazo zinatumika kutengeneza samani kama meza, viti, kabati, madawati, rafu nk. Mbao nyingine hutumika kupaulia nyumba kutengeneza milango na vifaa vingine vya nyumbani.

 

Pia miti hutupatia matunda mbalimbali ambayo ni matamu na mazuri kwa afya ya mwili kama vile malimao, machungwa, maembe, zambarau nk. Nyuki pia hutumia maua ya miti kama malighafi ya kutengeneza  asali.

 

Faida nyingine ya miti au misitu ni kurekebisha hali ya hewa.  Nchi isiyo na miti ya kutosha haipati mvua za kutosha kwani sehemu zenye misitu ndizo zipatazo mvua nyingi na za kutosha. Tatizo la mgao wa umeme lililolikumba nchi yetu kwa kiasi kikubwa limetokana na uharibifu wa uoto wa asili ikiwemo miti, vichaka, nyasi na mimea mingine. Miti au mimea ikiharibika ardhi hukauka, vyanzo vya mito au chemchem hukauka na kina cha maji kwenye mabwawa hupungua. Miti pia humfaa binadamu kwa kumpatia dawa asili kwenye majani yake, maua, magome au hata mizizi.

 

Faida zote hizi zinadhihirisha kuwa miti ni rafiki mkubwa wa binadamu ambaye hajatendewa haki kwa kukatwa ovyo na kuchomwa moto. Ikumbukwe kuwa tukiangamiza miti na sisi tunaangamia.

 

Maswali:

a)   Andika kichwa cha habari uliyosoma kwa maneno yasiyozidi matano.

_________________________________________________________________

b)   Mwandishi ana maana gani anaposema “usipoziba ufa utajenga ukuta”?

________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________

c)    Taja faida tatu za miti au misitu.

(i)           ____________________________________________________________

(ii)          ____________________________________________________________

(iii)         ____________________________________________________________

d)   Eleza kwa kifupi maana ya maneno yaliyopigiwa mstari kama yalivyotumika

kwenye habari uliyosoma.

______________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________

2.    Fupisha habari hii kwa maneneo yasiyozidi 150.

________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________

 

 

SEHEMU C (Alama 25)

SARUFI

3.    a) Toa maana ya mofimu na aina zake.

________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________

b) Eleza dhima za mofimu zilizopigiwa mstari katika yafuatayo:

(i)             Wamejipiga

____________________________________________________________

(ii)            Umesoma

____________________________________________________________

(iii)           Tumemchezesha

____________________________________________________________

(iv)          Sijaw aona

____________________________________________________________

(v)            Limia

____________________________________________________________

 

 

 

 

 

 

 

c)  Chagua kifungu cha maneno kutoka ORODHA B kinachotoa maelezo sahihi ya

     maneno/neno katika ORODHA A kasha andika herufi ya jibu sahihi katika

     jadweli.

ORODHA A

ORODHA B

(i)   Nyanya

(ii)  A, E, I, O, U   

(iii) Angewahi angenikuta                                     

(iv)Idadi ya fonimu za Kiswahili

(v)  Fonolojia

A.    Insha

B.    Starehe 

C.    Sarufi matamshi

D.   Irabu/fonimu

E.    Shina/mzizi

F.    Sentensi shurutia

G.   Sentensi

H.   Thelathini

I.     Ishirini na tano

J.    Bibi

K.    Sarufi maana                                                                            

 

Jibu:

i

ii

iii

iv

v

 

 

 

 

 

 

SEHEMU D: (Alama 25)

FASIHI SIMULIZI

4.    a)  (i)      Fasihi simulizi ni

________________________________________________________________________________________________________________________

(ii)      Taja tanzu nne za fasihi simulizi.

·         _________________________________________________________

·         _________________________________________________________

·         _________________________________________________________

·         _________________________________________________________

 

 

 

5.    a)  Kifuatacho ni kielelezo kinachoonesha mchoro wa Fasihi simulizi, tanzu na vipera

vyake. Jaza nafasi zilizoachwa wazi.

 

FASIHI SIMULIZI

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 


b)   Taja dhima tatu za fasihi katika jamii.

(i)   ______________________________________________________________

(ii)  ______________________________________________________________

(iii) ______________________________________________________________

c)   Malizia methali zifuatazo:

(i)   Asiyesikia la mkuu  ___________________________________.

(ii)  ________________________________ humaliza buyu la asali.

(iii) ________________________________ hujaza kibaba.

 

SEHEMU E: (Alama 20)

UTUNGAJI

6.    a)  toa maana ya barua na aina zake          

___________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________

b)  Andika barua kwa mwalimu mkuu ukimuomba urejee kidato cha kwanza mwaka huu kwa sababu mwaka jana hujasoma vizuri. Jina lako liwe masumbuko sijaona. Shule unayosoma SSP secondari S.L.P 897 ZANZIBAR

____________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________________            

 

Powered by Blogger.

Wasiliana nami papo kwa papo

Name

Email *

Message *

Ads 468x60px

Breaking News

Top Featured

Featured Posts

Sample text

Sample Text

Recomended

Mtila

Facebook

Advertise

Most Popular

Connect With Us

Followers

Social Icons

Pages

Pages

BTricks

Pages

Popular posts

Tafuta chochote ukiwa hapahapa

Kategori

Recent Comments

You can replace this text by going to "Layout" and then "Page Elements" section. Edit " About "

recent posts

Video Of Day

TRANSLATE

Instructions

Video

Flickr Images

FURAHIA UWEPO WAKO HAPA

Logo Design by FlamingText.com
Logo Design by FlamingText.com

Imetembelewa mara

TAKWIMU ZA WATEMBELEAJI

Popular Posts

SAJIRI

Definition List

premium-wordpress-themes.org