28 Jun 2014



                                                         

                   MAAJABU  YA  LUGHA  YA  KISWAHILI

          Lugha  ya  Kiswahili ni  lugha  ya  kibantu  yenye  asili  ya  mwambao  wa  pwani  ya  afrika  mashariki  yenye lahaja  mbalimbali na  ambayo  hutumiwa  na  watu  wengi  wa  afrika  mashariki na kati  mfano  Kenya ,Rwanda,Burundi,Congo na  hususani  Tanzania. Maajabu  ni  mambo  ya  kushangaza ,yasiyokuwa  ya  kawaida na  yenye  upekee  mkubwa  ukilinganisha  na  hali  ya  kawaida.


Maajabu  ya  lugha  ya  Kiswahili  ni upekee , hali  isiyokuwa  ya  kawaida ,ubunifu  na  umahili  ndani  ya  lugha  ya  Kiswahili  jinsi  inavyopendeza ,inavyovutia  na inavyotumika  ndani  ya  jamii  mbalimbali .Kuna  maajabu  mbalimbali  ndani  ya  lugha  ya  Kiswahili  lakini  yafuatayo ni maajabu  saba  ya  lugha  ya  Kiswahili :-
            Asili  ya  lugha  ya Kiswahili; lugha  ya  Kiswahili  asili  yake  ni  mwambao  wa  pwani  ya  afrika  mashariki  ambao  huhusisha  nchi  kama  Kenya  na  Tanzania .Asili  hii  ya  lugha  ya  Kiswahili  tunaweza  kusibitisha  kwa  sababu  mbalimbali  kwa  mfano  lahaja  nyingi  za  Kiswahili  zinapatikana  ndani  ya  afrika  mashariki, waongeaji  wazuri  wa  lugha  ya  Kiswahili  wanapatikana ndani  ya  afrika  mashariki na waandishi  wengi  wa  vitabu  vya  Kiswahili  bado  wanapatikana  ndani  ya  afrika  mashariki. Hivyo basi  hii  inathibitisha  kuwa  Kiswahili  kina maajabu  makubwa.
            Fasihi  ya  lugha  ya  lugha  ya  Kiswahili, fasihi ya  lugha  hii  ni  ya  pekee  sana  ukilinganisha  lugha  zingine  mfano katika  tanzu  kama  vile  Liwaya ,Tamthilia  na   Ushairi, kwa  kiasi  kikubwa  tanzu  hizi  zinaingiliana  na  kutofautana  mfana  tamthilia  ya  Nguzo  Mama  ya  Penina  Muhando  tunaona  anajaribu  kutumia  nyimbo  katika  kuisana  kazi  yake ambao  ni  kipera  cha  ushairi. Hivyo  basi  haya  ni  maajabu  ndani  ya  lugha  Kiswahili  katika  fasihi  ya  Kiswahili.
           Ukuaji  na  ueneaji  wa  lugha  ya  Kiswahili, hapa  tunaangalia  njia  mbalimbali  zinazotumika  kukuza  na  kueneza  lugha  hii  ya  Kiswahili  mfano  vyombo  vya  habari  kama  vile  Lungoya  (redio  japan  idhaa ya  Kiswahili) ,sauti  ya  amerika  kwa  lugha  ya  Kiswahili hii ni kwa  upande  wa  nje  ya  afrika  mashariki.pia  kuna  taasisi  pamoja  na  vyama  mbalimbali vinavyoshughulikia  na ukuzaji  na  uenezaji  wa  lugha  hii ndani  ya  afrika  mashariki  mfano  TUKI ,TAKILUKI ,CHAWAKAMA,BAKITA,UKUTA nakadhalika. Hivyo  basi  hii  inapelekea  idadi  ya  watumiaji  kuongezeka  na  kukifanya  Kiswahili  kuendelea  kuwa  na  maajabu  makubwa.
           Matumizi  ya  lugha  ya  Kiswahili  katika  muktadha  mbalimbali, mfano  elimu,siasa, uchumi, michezo,mikutano ,sherehe  na  mahubiri.kwa  kuanza  na  muktadha wa elimu Kiswahili  kimepandishwa  hadhi  mpaka  kufundishwa  ngazi  ya  chuo  kikuu, sekondari  kama somo  na  shule  za  msingi  kama  lugha  ya  kufundishia masomo  yote  isipokuwa  kiingereza tu ndani  ya  Tanzania pia  Kiswahili  kutumika  kwenye  mikutano  mikubwa  ndani  ya  afrika mfano  ya  jumuiya  wanachama  wa  afrika mashariki. hivyo  basi  hayo  ni  maajabu  makubwa  ndani  ya  lugha  hii.
           Uundaji  wa  msamiati  wa  lugha  ya  Kiswahili.  msamiati ni  maneno  yanayopatikana  katika  lugha  Fulani  hivyo  basi  msamiati  katika  lugha  ya  Kiswahili  ni maneno  yanayopatikana  ndani  ya  lugha  ya  Kiswahili. Lugha  hii  ina njia  nyingi  sana  zinazotumika  katika  kukuza  msamiati  wake  kama  vile  kutohoa  toka  lugha  za  kigeni, miambatano, kufananisha  umbo  sura  na  sauti, na  kubadilisha  mpangilio  wa  herufi.hizi  njia  zinazotumika  katika  kuundia  msamiati  wa  lugha  ya  Kiswahili.
           Utafutaji  na  upataji  wa  visawe  vipya  vya  lugha  ya  kiswahli. Visawe  ni  maneno  ndani  ya  lugha  mbalimbali  yanayofafanua kitu  au  jambo  moja  kwa  matamshi  ya  lugha  hizo. Katika  lugha  ya  Kiswahili  kuna  uhaba wa  visawe  vinavyotokana  na  maendeleo  ya  sayansi  na  teknolojia lakini  jitihada  zimefanyika  na  zinaendelea  kufanyika katika  kuhakikisha  visawe  vinapatikana  mfano  wa  visawe vipya ni  mnyange, nywila, kinuruweo, sasisha, talakilishi, talakilishi mpakato pamoja  na  kinyoni. Hivyo  basi  haya ni  maajabu  makubwa  sana yanayopatikana  ndani  ya  lugha  hii  ya  Kiswahili.
            Kasumba  na  uhaba  wa  wataalamu  wa  lugha  ya  Kiswahili. Kasumba  ni  hali  ya  kutothamini  kitu  chako  kwa  kung’ang’ania vitu  vya  kigeni.hili  ni  moja  ya  ajabu  katika  lugha  ya  Kiswahili  kwa   sababu  wazawa  wengi hususani  wasomi  wanakidharau  kiswahli japo  kuwa  ndio  lugha  yao  pia  licha  ya  kuwa  Kiswahili   asili   yake  ni  afrika  mashariki  ajabu  bado  kuna  uhaba  wa  wataalamu  wa  lugha  hii. Hivyo basi  hayo  yote  yanabaki  kama  maajabu  katika  mlongo  hasi.
         Hivyo basi  hayo  ndio  maaajabu  ya  lugha  ya  Kiswahili. Ili  kiswahili  kiweze  kuendelea  zaidi  na  zaidi  ni  lazima  elimu  itolewe  juu  ya  umuhimu  wa lugha  hii.pia  serikali  ni  lazima  itambue  kuwa  hii  ni  lasilimali hivyo  basi  ni  lazima iwekeze  vya  kutosha kwa  kushilikiana  na  vyombo  vyombo  vya  habari, wadau mbalimbali, mashirika  mbalimbali  , pamoja  na  taasisi na  vyama  mbalimbali  vya  kukuza  na  kuendelza  Kiswahili  ndani  na  nje   ya  nchi.




…>>>>>>>>>>>>>????MTILA BAHATI?????>>>>>>>>>>>>>>>>>>>

13 Jun 2014

Mtilabahati: ushairi mtamu: KIMOJA          i.             Nyumba hujengwa kwa mawe, Nawe umenijengea, Ukaipamba vigawe, Izidi kunivutia, Huduma zako na wewe, pe...
Powered by Blogger.

Wasiliana nami papo kwa papo

Name

Email *

Message *

Ads 468x60px

Breaking News

Top Featured

Featured Posts

Sample text

Sample Text

Recomended

Facebook

Advertise

Most Popular

Connect With Us

Followers

Social Icons

Pages

Pages

BTricks

Pages

Popular posts

Tafuta chochote ukiwa hapahapa

Kategori

Recent Comments

You can replace this text by going to "Layout" and then "Page Elements" section. Edit " About "

recent posts

Video Of Day

TRANSLATE

Instructions

Video

Flickr Images

FURAHIA UWEPO WAKO HAPA

Logo Design by FlamingText.com
Logo Design by FlamingText.com

Imetembelewa mara

TAKWIMU ZA WATEMBELEAJI

Popular Posts

SAJIRI

Definition List

premium-wordpress-themes.org