MAAJABU YA
LUGHA YA KISWAHILI
Lugha
ya Kiswahili ni lugha
ya kibantu yenye
asili ya mwambao
wa pwani ya
afrika mashariki yenye lahaja
mbalimbali na ambayo hutumiwa
na watu wengi
wa afrika mashariki na kati mfano
Kenya ,Rwanda,Burundi,Congo na
hususani Tanzania. Maajabu ni
mambo ya kushangaza ,yasiyokuwa ya
kawaida na yenye upekee
mkubwa ukilinganisha na
hali ya kawaida.
Maajabu ya lugha ya
Kiswahili ni upekee , hali isiyokuwa
ya kawaida ,ubunifu na
umahili ndani ya
lugha ya Kiswahili
jinsi inavyopendeza ,inavyovutia na inavyotumika ndani
ya jamii mbalimbali .Kuna maajabu
mbalimbali ndani ya
lugha ya Kiswahili
lakini yafuatayo ni maajabu saba
ya lugha ya
Kiswahili :-
Asili ya lugha
ya Kiswahili; lugha ya Kiswahili
asili yake ni
mwambao wa pwani
ya afrika mashariki
ambao huhusisha nchi
kama Kenya na
Tanzania .Asili hii ya
lugha ya Kiswahili
tunaweza kusibitisha kwa
sababu mbalimbali kwa
mfano lahaja nyingi
za Kiswahili zinapatikana
ndani ya afrika
mashariki, waongeaji wazuri wa
lugha ya Kiswahili
wanapatikana ndani ya afrika
mashariki na waandishi wengi wa
vitabu vya Kiswahili
bado wanapatikana ndani
ya afrika mashariki. Hivyo basi hii
inathibitisha kuwa Kiswahili
kina maajabu makubwa.
Fasihi ya lugha
ya lugha ya
Kiswahili, fasihi ya
lugha hii ni ya
pekee sana ukilinganisha
lugha zingine mfano katika
tanzu kama vile
Liwaya ,Tamthilia na Ushairi, kwa
kiasi kikubwa tanzu
hizi zinaingiliana na
kutofautana mfana tamthilia
ya Nguzo Mama
ya Penina Muhando
tunaona anajaribu kutumia
nyimbo katika kuisana
kazi yake ambao ni
kipera cha ushairi. Hivyo basi
haya ni maajabu
ndani ya lugha
Kiswahili katika fasihi
ya Kiswahili.
Ukuaji na
ueneaji wa lugha
ya Kiswahili, hapa tunaangalia
njia mbalimbali zinazotumika
kukuza na kueneza
lugha hii ya
Kiswahili mfano vyombo
vya habari kama
vile Lungoya (redio
japan idhaa ya Kiswahili) ,sauti ya
amerika kwa lugha
ya Kiswahili hii ni kwa upande
wa nje ya
afrika mashariki.pia kuna
taasisi pamoja na
vyama mbalimbali
vinavyoshughulikia na ukuzaji na
uenezaji wa lugha
hii ndani ya afrika
mashariki mfano TUKI ,TAKILUKI ,CHAWAKAMA,BAKITA,UKUTA
nakadhalika. Hivyo basi hii
inapelekea idadi ya
watumiaji kuongezeka na
kukifanya Kiswahili kuendelea
kuwa na maajabu
makubwa.
Matumizi ya
lugha ya Kiswahili
katika muktadha mbalimbali, mfano elimu,siasa, uchumi, michezo,mikutano
,sherehe na mahubiri.kwa
kuanza na muktadha wa elimu Kiswahili kimepandishwa
hadhi mpaka kufundishwa
ngazi ya chuo kikuu, sekondari kama somo
na shule za
msingi kama lugha
ya kufundishia masomo yote
isipokuwa kiingereza tu
ndani ya
Tanzania pia Kiswahili kutumika
kwenye mikutano mikubwa
ndani ya afrika mfano
ya jumuiya wanachama
wa afrika mashariki. hivyo basi
hayo ni maajabu
makubwa ndani ya
lugha hii.
Uundaji wa
msamiati wa lugha
ya Kiswahili. msamiati ni maneno
yanayopatikana katika lugha
Fulani hivyo basi
msamiati katika lugha
ya Kiswahili ni maneno
yanayopatikana ndani ya
lugha ya Kiswahili. Lugha hii
ina njia nyingi sana zinazotumika
katika kukuza msamiati
wake kama vile
kutohoa toka lugha
za kigeni, miambatano,
kufananisha umbo sura
na sauti, na kubadilisha
mpangilio wa herufi.hizi
njia zinazotumika katika
kuundia msamiati wa
lugha ya Kiswahili.
Utafutaji na
upataji wa visawe
vipya vya lugha
ya kiswahli. Visawe ni
maneno ndani ya
lugha mbalimbali yanayofafanua kitu au
jambo moja kwa
matamshi ya lugha
hizo. Katika lugha ya
Kiswahili kuna uhaba wa
visawe vinavyotokana na
maendeleo ya sayansi
na teknolojia lakini jitihada
zimefanyika na zinaendelea
kufanyika katika kuhakikisha visawe
vinapatikana mfano wa
visawe vipya ni mnyange, nywila, kinuruweo,
sasisha, talakilishi, talakilishi mpakato pamoja na
kinyoni. Hivyo basi haya ni
maajabu makubwa sana yanayopatikana ndani
ya lugha hii
ya Kiswahili.
Kasumba na uhaba
wa wataalamu wa
lugha ya Kiswahili. Kasumba ni
hali ya kutothamini
kitu chako kwa
kung’ang’ania vitu vya kigeni.hili
ni moja ya
ajabu katika lugha ya Kiswahili
kwa sababu wazawa
wengi hususani wasomi wanakidharau
kiswahli japo kuwa ndio
lugha yao pia
licha ya kuwa
Kiswahili asili yake
ni afrika mashariki
ajabu bado kuna
uhaba wa wataalamu
wa lugha hii. Hivyo basi hayo
yote yanabaki kama
maajabu katika mlongo
hasi.
Hivyo basi hayo
ndio maaajabu ya
lugha ya Kiswahili. Ili kiswahili
kiweze kuendelea zaidi
na zaidi ni
lazima elimu itolewe
juu ya umuhimu
wa lugha hii.pia serikali
ni lazima itambue
kuwa hii ni lasilimali
hivyo basi ni
lazima iwekeze vya kutosha kwa
kushilikiana na vyombo
vyombo vya habari, wadau mbalimbali, mashirika mbalimbali
, pamoja na taasisi na
vyama mbalimbali vya
kukuza na kuendelza
Kiswahili ndani na
nje ya nchi.
…>>>>>>>>>>>>>????MTILA
BAHATI?????>>>>>>>>>>>>>>>>>>>