SURA
SITA ZA KITABU
Utangulizi
Haya
shime piga konde, mambo sasa kuandika,
Mithili
maji mbande, yanotaka kumwagika,
Natanguli….chondechonde,
sura sita bila shaka
Lengo
kinyume cha mwande, uwanja uje safika,
Tupambane
tuyashinde, ili tuje heshimika,
Sura
sita kila pande, zimenena bila shaka,
Sura
ya kwanza
Yarabi
nipe imani, sura hii kueleza,
Yanofanywa
sakafuni , mimi yananishangaza,
Na
vifo vya hadharani, albino wapoteza,
Ni
dhambi iso kifani, nchi twaitelekeza,
Tupambane
kwa yakini, kwa umoja tutaweza,
Tudumishe
na amani, na sifa kuendeleza,
Tuzidishe
ikisiri, tokomeza mauwaji.
Sura
ya pili
Sura
hii si sharifu, inaitwa “ugaidi”
Sura
hii si nadhifu, kueleza imebidi,
Nchi
wazifanya chafu, mwanadamu makusudi,
Kuua
kwa israfu, duniani kumezidi,
Afrika
sasa hofu, mashariki ni zaidi,
Tuwatoe
waarifu, tupambane kwa jihadi,
Afrika
iwe safi, iwe safi na nadhifu.
Sura
ya tatu
Haya
shime kwa salamu,hii sura ni makini,
Ina
mambo ya muhimu, yalo bora na thamani,
Haya
mambo ya kalamu, hayaitaji umbini,
Yanaitaji
nidhamu, pamoja na darubini,
Kutazama
kufahamu, tunapanda tupo chini,
Kwa
wadau na walimu, tufanye kazi nyanjani,
Tuiboreshe
elimu, vizazi visipotee.
Sura
ya nne
Jama
sili nikashiba, natafuta koti langu,
Koti
hilo ndio tiba, visiwani bara kwangu,
Kwa
famili ndio baba, binadamu moyo wangu,
nikilikosa
msiba, itazikwa nchi yangu,
kubwa
maoni ya huba, yatoke kwako na kwangu,
tuitetee
katiba, tutetee kwa uchungu,
bila
katiba ni sawa, gari bila mataili.
Sura
ya tano
Sura
hii ya vijana, wa rika lile shufufu,
Wavulana
wasichana, wahusika maarufu,
Mitandaoni
kwa sana, Kuperuzi picha chafu,
Matumizi
yaso mana, kutumia bila hofu,
Kuna
baadhi vijana, tumia kwa unadhifu,
Mambo
mema kupashana, na kukemea machafu,
Ya
jamii mitandao, tuitumie muluwa.
Sura
ya sita
Kuna
mapacha wawili, sasa wana jina moja,
Ukimuita
wa pili, wanaitika pamoja,
Waliungana
wawili, hivi sasa ni mmoja,
Wametoka
huko mbali, waliungana kwa hoja,
Na
mchanga wa halali, walichanganya pamoja,
Kulipinga
jambo hili, ni hoja si kubwabwaja,
Tudumishe
muungano, Tanzania songa mbele.
hitimisho
Hitimisho
langu leo, lina mambo kadharika,
Na
walio wengi wao, nahodha taka kushika,
Kutangaza
nia zao, lengo chombo kupeleka,
Wananchi
kazi yao, yupi safi kumuweka,
Bila
kujali wa kwao, au wapi anatoka,
Kiongozi
ndio ngao, ili bora imarika
Uchaguzi
ukifika, weka nia piga kura