Kusikiliza
mazungumzo
Dhana ya mazungumzo.
Mazungumzo ni
utaratibu ni maelezoya mdomo kwa lugha ya kawaida kuhusu suala lolote mbili au
zaidi ambapo kwa kawaida kwa kawaida wahusikawa mazungumzo hayo huwa ni watu
.Mazungumzo yanapofanyika huwakutanisha mzungumzaji na msikilizaji ,msikilizaji
huelewa vizuri mazungumzo kutokana na kusikilizakwa makini. Mazungumzoau habari
anayosomewa au kusimuliwa msikilizaji huhitaji umakini .Habari inaweza
kusimuliwa ana kwa ana au kutoka kwenye televisheni ,redio ,komyuta au simu ya
mkononi.
Mambo
ya kuzingatia katika kusikiliza mazungumzo
Ili kuelewa vizuri mazungumzoau habari
anayosikiliza,msikilizaji anatakiwa kuzingatia mambo yafuatayo,
·
Awe makini
kusikiliza kinachosimuliwa au kusomwa
·
Abainishe
mambo muhimu yanayoelezwa katika mazungumzo anayosikiliza.
·
Msikilizaji
amtazame usoni mzungumzaji iliaweze kupata taarifa za ziada ambazo mzungumzaji
anawe za kuzitoa kwa kutumia ishara za mwili.
·
Msikilizaji
awe makini na sarufi ya lugha inayozungumzwa na lafudhi ya mzungumzajia anaweza
kuzitoa kwa kutumia ishara za mwili
·
Msikilizaji
awe makini na sarufi ya lugha inayozungumzwa na lafudhi ya mzungumzaji
·
Msikilizaji
awe katika eneo lenye utulivu kuepuka kelele zinazoweza kufanya asisikie vyema
.
Sifa
za lugha ya mazungumzo.
Lugha ya mazungumzo huwa na sifa kadhaa kama
ifuatavyo;
·
Mzungumzaji na
msikilizaji kupeana nafasi wakati wa mazungumzo ili wweze kuelewana
·
Kutumia lugha
ya mkato kwalengo la kurahisisha mawasiliano na kuokoa muda
·
Huwa na
utaratibu wa kurudiana kwa maneno au sentensi kwa lengo la kusisitiza au
kufafanua jambo zaidi
·
Huwa na
matumizi ya lugha ya vionjo kwalengo la kupamba lugha . mfano, matumizi ya
semi.
·
Huhusiha stadi
kuu mbili za lugha ambazo ni kuzungumza
na kusikiliza kwa wakati mmoja.
·
Hutumia lugha
ya ishara na mijongeo ya viungo ya mwili .Mtu anapomzungumza huwezakucheka
kutikisa mabega ,kuguna,kuweka mkono usoni,kutikisa kichwa kuashiria kukubali
au kukataa jambo.
·
Mzungumzaji au
msemaji au msikilizaji wote kwa pamoja hutakiwa kuzingatia ufasaha wa maneno
yanayotolewa
Kusikiliza
mazungumzo changamani.
Mazungumzochangamani ni mazungumzo yale yanayohusu
masuala muhimu yanayozungumziwa katika mazungumzo.katika kusikiliza mazungumzo
changamani, msikiliza anatakiwa awe na kalamu na karatasi,kompyuta,simu au
tablet kwa ajili ya kuandika mambo hayo muhimu kutoka kwenye habari
anayoisikiliza.ikumbukwe kuwa mazungumzo changamani ni yale mazungumzo marefu
ambayo yanahitaji msikilizaji awe makini kuchambua ni kusikiliza mambo muhimu.
Mfano wa mazungumzo changamani ni hotuba za viongozi , kampeni za siasa, risala
na mazungumzo mengine yenye mada mchanganyiko,
Kufupisha
mazungumzo changamani.
Ufupisho ni taaluma inayohusu upunguaji wa maneno
katika habari au mazungumzo kwa kuzingatia maudhui ya habari au mazungumzo
husika . upunguzaji huo huyaondoa au kuyajumuisha maneneo yenye dhana moja bila
kuathiri ujumbe uliokusudiwa katika kufupisha mazungumzo changamani ,unapaswa
kuzingatia yafuatayo ;
·
Kufupisha
mazungumzo yawe mafupi kuliko ya mwanzo
·
Kubakiza maana
ileile katika mazungumzo uliyofupisha,usiondoe maneno ya msingi
·
Kuwa na
mtiririko mzuri wa mazungumzo yako nay awe na mantiki
·
Tumia maneno
yako mwenyewe
·
Zingatia
kutokpunguza ujumbe wa mazungumzo
·
Tafuta maneno
mengine yanayoweza kutumika badala ya fungu Fulani la maneno. Kwa mfano “kaka
wa mama yangu ni mgonjwa” inaweza kuwa mjomba ni mgonjwa.
Hatua
za kufuata katika kufupisha mazungumzo changamani
l Sikiliza
mazungumzo au habari yote kwa makini
l Bainisha
mawazo makuu kutoka kwenye habari au mazungumzo uliyoyasikiliza
l Mazungumzo
au habari uliyoisikiliza ina lugha fasaha na mtiririko mzuri wa mawazo
l Hakikisha
hujapunguza ujumbe wa mazungumzo
l Husianisha
mazungumzo muhimu na mazungumzo ya awali kama yanaendana.
Kushiriki
katika majadiliano ya muktadha mbalimbali.
Majadiliano
ni
kitendo cha kupeana mawazo chanya baina ya watu au pande mbili au zaidi ili
kufikia muafaka wenye manufaa kuhusu suala au jambo fulani.
Mara nyingi majadiliano hufanywa kwenye kikundi
cha watu wawili au zaidi ili kutatua jambo au kuonngeza ujuzi wa jambo Fulani.
Kwa mfano:majadiliano kuhusu umuhimu wa elimu .
Majadiliano huwa na mada moja au zaidi . Aidha,
majadiliano yanaweza kuwa rasmi au yasiyo rasmi . majadiliano rasmi huzingatia
mazingira rasmi na majadiliano yasiyo rasmi hufanyika katika mazingira yasiyo
rasmi mfano kijiweni,nyumbani au barabarani
Taratibu
na sifa za majadiliano
·
Huhusisha
pande mbili yaani wazungumzaji na wasikilizaji kwa wakati mmoja
·
Huwa na washiriki wawili au zaidi
·
Huwa na hoja au mada imayojadiliwa
·
Huandaliwa
katika mazingira rasmi au yasiyo rasmi
·
Huhusisha
utamkaji sahihi na matumizi ya Kiswahili fasaha
·
Huhitaji
utamkaji sahihi na matumizi ya Kiswahili fasaha
·
Huhitaji
usikivu mkubwa ili kuweza kuchangia hoja.
Zoezi la
Marudio
1. Chagua jibu sahihi katika
maswali yafuatayo
i) Malezo ya mdomo kwa lugha ya kawaida kuhusu jambo lolote
huitwaje?
A.Majadiliano
B.Mazungumzo
C.Mawasiliano
D.Ushirikiano
E.Makubaliano
ii) Ipi kati ya seti zifuatazo si sifa ya
mazungumzo?
A. Haifanyiki
bila kuzingatia aina za maneno
B. Kupeana
nafasi wakati wa mazungumzo
C. Kuna
matumizi ya vionjo vya mwili
D. Hutumia
lugha ya mkato ili kurahisisha mawasiliano
E. Hawana
urudiaji wa maneno au sentensi ili kusisitiza
iii) Zipi ni pande mbili zinazohusisha mazungumzo?
A. Mzungumzaji
ma msemaji
B. Msemaji
na msikilizaji
C. Msilikilizaji
na msemaji
D. Mzungumzaji
na msikilizaji
E. Msikilizaji
na Msomaji
iv)
Unaelewa nini kuhusu mazungumzo changamani?
A. Mazungumzo
ya watu wakubwa
B. Mazungumzo
yahusuyo masuala muhimu
C. Mazungumzo
yahusuyo familia tu
D. Mazungumzo
yaliyopitwa na wakati
E. Mazungumzo
yanayotumia lugha ya ishara.
v) Taaluma inayohusu upunguzaji wa maneno
katika habari au mazungumzo kwa kuzingatia maudhui ya habari au mazungumzo
husika huitwaje?
A. Mazungumzo
changamani
B. Ufupisho
C. Majadiliano
D. Mkazo
E. Ufahamu
2. Oanisha maana
ya dhana katika Orodha A na dhana zinahusika kutoka Orodha B kwa kuchagua
herufi ya jibu sahihi.
ORODHA A |
ORODHA B |
i.
Redio,televisheni,kompyuta,simu
ya mkononi na kinasa sauti |
A. Kupunga,kukunja
uso, kucheka |
ii.
Kueleza jambo kwa maneno
machache |
B. Vifaa
vinavyoweza kutumika katika maasiliano ya mzangumzo |
iii.
Ishara zitumikazo katika
mazungumzo |
C. Mzungumzaji
na msikilizaji |
iv.
Mazungumzo huhusisha pande
mbili |
D. Ufupisho |
v.
Hutambulisha jamii Fulani |
E. Lafudhi |
|
F. Mkazo |
|
G. Lugha
ya mazungumzo |
3. Eleza
mambo matano (5) yanayoweza kukusaidia kuelewa unaposikiliza mazungumzo
4. Fanya
majadiliano na wenzako darasani kuhusu chanzo cha mmomonyoko wa maadili kwa
vijana na kupendekeza nini kifanyike ili kuondoa hali hiyo . Kisha, andika
ufupisho na mjadala huo kwenye daftari lako kwa maneno yasiyozidi 150
5. Sikiliza
kifungu cha habari kifuatacho kinachosomwa na mwenzako, kisha kifupishe kwa
sentensi zisizozidi tano(5)
Maendeleo ya
Kiswahili nchini ni ya kutia moyo Lugha hii sasa imeingia katika uwanja wa
sayansi na teknolojia . Huu ni wakati muhimu sana katika maendeleo ya lugha hii
. kwanza ni wakati ambapo kunahitajika kuwapo na mikakati kabambe yenye upeo wa
mbali ya kuendeleza lugha hii kitaaluma. Sayansi na teknolojia ni uwanja wa
taaluma . Pili, tunahitajika kutumia utaalamu wa hali ya juu katika kuijenga
lugha hii ili iweze kubeba mahitaji katika mazingira hayo. Bila hiyo hatuwezi
kusonga mbele.
6. Fafanua
sifa za lugha ya mazungumzo na taratibu za majadiliano
7. Unapata
ujumbe gani unaposikiliza wimbo wa Taifa la Tanzania unakimbwa
8. Fafanua
sifa tano za majadiliano
9. Andika
tofauti tano kati ya mazungumzo na majadiliano
10.Fafanua
mambo matano(5) yanayoweza kusababish msikilizaji asiweze kuelewa
anachosikiliza.