Kuwasiliana
kwa njia ya maandishi
Dhana
ya mawasiliano kwa njia ya maandishi
Mawasiliano kwa njia ya maandishi ni aina ya
mawasiliano ambayo huhusisha matumizi ya
matini mbalimbali kama vile barua, hotuba, risala, kumbukumbu za vikao, kifungu
cha habari na insha.
Mambo yakuzingatia katika kufikisha
ujmbe wa maandishi
i.
Mwandishi
anapaswa kuzingatia ufasaha wa lugha anayotumia ili msomajia aweze kuelewa
ujumbe uliokusudiwa
ii.
Mwandishi
anapaswa kuzingatia matumizi ya lugha
fasaha kwani yatamsaidia msomaji
kuuelewa na kukuza lugha inayohusika kwa
ufasaha
iii. Mwandishi
anapaswa kutumia msamiati sahihi unaoendana na muktadha wa mada inayohusika
iv. Mwandishi
anapaswa kuzingatia uhusiano sahihi wa maneno ili kujenga sentesi zinazoeleweka
kwa msomaji
v.
Mwandishi
anapaswa kuzingatia matumizi sahihi ya viunganishi na tahajia
vi. Mwandishi
anapaswa kuzingatia alama za uandishi
vyema ili maudhui yaliyokusudiwa yaweze kumfikia msomaji.
Taratibu
za Uandishi
Taratibu za uandishi ni alama na mpangilio wa
maneno yanayo mwongoza mwandishi kuandika kwa usahihi. Ili habari iweze kuwa
nzuri, inayoeleweka vizuri kwa wasomaji, mwandishi hana budi kutumia alama.
Alama hizi humsaidia msomaji kujua wapi pa kupumzika, kuuliza swali, kushangaa,
n.k. Alama zifuatazo hutumiwa katika uandishi:
Nukta
(.)
(a) Hutumika
kukamilisha sentensi
Mfano:Mama anapika jikoni.
(b)Hutumika
kuonesha ufupisho wa maneno
Mfano:n.k (nakadhalika), k.m (kwa
mfano), S.L.P (sanduku la posta).
(c) Hutumika
kuonesha vipimo mbalimbali katika desimali
Mfano: saa 3.45, meta 92.3, kilogramu 8.2
Mkato (,)
(a) Hutumika
kuweka pumziko fupi katika sentensi
Mfano: Alipofika
shuleni alipokelewa na Ashura, Musa na Mwalimu Tino.
(b)Hutumika
kutenga maneno yaliyo katika orodha
Mfano: Ninunulie kalamu, kitabu, ufutio na karatasi
(c) Hutumika
kuonesha sehemu mbili za sentensi zilizo kinyume
Mfano: Aliye juu, mngoje chini
Umoja
ni nguvu, utengano ni udhaifu.
(d)Hutumika
kabla ya alama za mtajo.
Mfano: Mwalimu Sawaka alisema, “leo nitawafundisha”
(e) Hutumika
kuonesha vyeo, anuani au maskani baada ya jina la mtajwa.
Mfano: Moses Okelo , Mkurugenzi wa Halmashauri-Nzega.
(f) Hutumika
badala ya viunganishi
Mfano: Unacheza au huchezi?
Usipotaka
kutumia kiunganishi au unaweza kuandika
Unacheza,
huchezi?
(g) Hutumika
kabla na baada ya vifungu vya maneno vielezavyo maneno yaliyotangulia.
Mifano: Helasita, shule ya mfano Tanzania, huwezi kuifananisha.
Mihambo,
mwalimu pekee wa somo la Kiswahili, aliyekutana na Rais Trump Marekani.
(h)
Hutumika mbele
ya vifungu vya vielezi vinavyokaa mwanzoni mwa sentensi.
Mifano: Kimyakimya, aliingia ndani huku akilia.
Kwa
mbwembwe nyingi, alianza kupigana.
Nukta mbili/Nukta pacha (:)
(a) Hutumika
kuashiria vitu vilivyo katika mfululizo au orodha.
Mfano: Nilimletea mama: nguo, viatu, gauni na kitenge.
(b)Hutumika
katika maandishi ya kitamthiliya.
Mifano: Mwalimu Masawe: (kwa upole)hamjambo wanafunzi
Wanafunzi:
Hatujambo shikamoo mwalimu.
Mwalimu
Masawe: Marahaba! Kaeni.
(c) Hutumika
kutenganisha saa, dakika na sekunde.
Mifano: Saa 9:45, saa 2:28:10
Saa
2:20:10, saa 12:00 n.k.
(d)Hutumika
kuonesha uwiano baina ya namba.
Mfano: 8:7, 26:20, 7:6
(e) Hutumika
kutenganisha tarakimu kama vile za maandiko matakatifu.
Mifano: Yohana 3:16-19
Matendo
ya Mitume 8:1-3
Nukta Mkato (;)
(a) Hutumika
kuunga tungo mbili zenye sifa zinazolingana lakini zisizo na kiunganishi.
Mfano: Wengine wanacheka; Wengine wanalia.
Jackline
Tiganga anasoma;Ghati anaandika
(b)Hutumika
ili kuonesha pumziko la muda mrefu zaidi katika kusoma kuliko unapotumia mkato.
Mifano: Mwalimu Neema anafundisha vizuri; anatamani kutuona tukifaulu
vizuri.
Triphonia
anapenda sana kuchora; inaonyesha jinsi atakavyokuwa mchoraji wa kimataifa.
Kistari (-)
(a) Hutumika
kuonesha neno limekatwa kwa kuwa limefika ukingoni mwa karatasi wakati bado
linaendelea katika mstari unaofuata. Kwa kawaida neno lenye silabi moja
halikatwi, huandikwa lote mwishoni mwa mstari au kama nafasi haitoshi, mwanzoni
mwa mstari unaofuata.
Mifano: Alipofika hapa ali-
pewa zawadi
(b)Hutumika
kuunga maneno mawili.
Mfano: Askari –kanzu, Idd-el-fitri
Kipima-pembe
Dar-es-Salaam
(c) Hutumika
kuendeleza sauti
Mfano: A-a-a-a-a
Lo-o-o-o
(d)Hutumika
kuunga sentensi mbili, sentensi ya pili ikiwa ni ufafanuzi wa sentensi ya
kwanza.
Mfano: Kulikuwa
na kusanyiko kubwa sana uwanjani- wanaume, wanawake na watoto walihudhuria.
(e) Hutumika
badala ya nukta mbili.
Mfano: Nichukulie- shati, gauni na koti.
Mabano( )
(a) Hutumika
kuonesha maana ya ziada katika sentensi.
Mfano: Rais
Mstaafu wa awamu ya nne(Jakaya Kikwete) ni mtu hodari.
Nchi
yangu (Tanzania) ina demokrasia makini.
Alama ya kuuliza (?)
(a) Hutumika
badala ya nukta au alama ya kushangaa ili kufunga sentensi zinazouliza maswali.
Baada ya alama hii, sentensi inayofuata huanza kwa herufi kubwa.
Mfano Mama yuko wapi? Mbona
haonekani?
(b)Hutumika
kuuliza swali
Mfano: Wewe unaitwa nani?
Alama ya kushangaa (!)
(a) Hutumika
baada ya neno au usemi wa kushangaa, kushtuka, huzuni au uchungu. Baada ya
alama hii kutumika, sentensi inayoanza huanza kwa herufi kubwa.
Mfano: Loo! Mtoto wewe huna adabu
Kumbe
amefariki!
(b)Hutumika
wakati wa kusisitiza jambo kama vile kero, kubeza, utani n.k.
Mfano: Ona ulivyo mjinga!, Ondoka hapa wewe kima!
Alama za mtajo (“…..”)
(a) Hutumika
katika kukariri maneno yaliyosemwa au kuandikwa na mtu mwingine.
Mfano: Mwalimu alisema, “Wote mnastahili zawadi nono”
Juma
alijibu, “Hata mimi ninastahili zawadi nono”
(b)Hutumika
kuonesha maneno ya lugha ya kigeni
Mfano: Hilda Fundi ni “Intelligent”
Mwalimu
hakufanya “fair”
(c) Hutumika
kubainisha misimu, maneno yasiyokubalika katika lugha inayoandikwa.
Mifano: Amekutwa akitumia “ngada” chooni.
Timu
ya Simba “walitoswa” na wenyeji wao huko Manungu.
Ritifaa (‘) Kibainishi
(a) Hutumika
kutofautisha ng na ng’ katika maneno.
Mfano ng’ombe, ng’arisha,
ng’ang’ania, ng’aa n.k.
(b)Hutumika
kuonesha kwamba herufi fulani imeachwa hasa katika ushairi.
Mfano: ‘mejaribu jongea ndege awe mkononi.
Nimejaribu jongea ndege awe mkononi.
Mstari wa mshazari ( /
)
(a) Hutumika
katika nambari ya kumbukumbu
Mfano: NA: PT / BT / 60
(b)Hutumika
katika kutenga tarehe, mwezi na mwaka.
Mfano: 6/8/2022
(c) Hutumika
badala ya neno au.
Mfano: Bw/Bi
Dawa/chakula
Nyeusi/nyekundu
Asubuhi/jioni
Herufi kubwa
(a) Hutumiwa
mwanzoni mwa sentensi, baada ya nukta, baada ya alama ya kushangaa au alama ya
kuuliza.
Mfano: Tanga
ni mkoa ulioko Kaskazini mwa nchi yetu. Mkoa huo unasifika kwa jambo gani?
Jambo la kwanza ni kilimo cha mazao ya biashara.
(b)Hutumika
katika kuandika nomino za pekee kama majina ya watu, miji, vyeo na Mungu.
Mfano: Kajuna – jina la mtu
Arusha
– jina la mji
Rais-jina la cheo au wadhifa
(c) Hutumika
katika kuandika herufi ya kwanza ya kauli iliyokaririwa.
Mfano: “Nitawaadhibu wote,” Mwalimu Lugome alisema.
(d)Hutumika
katika kuandika vifupi vya majina ya watu, vyama au kampuni.
Mfano: J.K. T – Jeshi la Kujenga Taifa.
(e) Hutumika
kutaja majina ya sikukuu, sayari, siku, miezi, pande, dira, majina ya vitabu na
mada.
Nukta katishi (…….)
(a) Hutumika
kubainisha mdokezo
Mfano: Anatuongoza vizuri lakini ………
(b)Hutumika
kuonesha kuwa kuna maneno yaliyotangulia katika tungo.
Mfano: …………ndio waliochaguliwa na Rais
Aya
Ni
jumla ya sentensi zinazoeleza wazo moja. Hivyo, mkusanyiko wa sentensi zenye
wazo kuu au sentensi zinazolifafanua wazo hilo huitwa aya.
Aya
hueleza au kufafanua wazo maalumu, pia hurahisisha kazi ya msomaji kwa kuwa na
mawazo yenye mantiki. Aya hupunguza au kuondoa marudio ya mawazo kwa sababu
kila aya hubeba wazo moja linalojitosheleza.
Mambo
ya kuzingaitia katiika uandishi
i.
Hakikisha
unalielewa vyema jambo unaloliandikia. Hii itakusaidia kuandika jambo hilo kwa
upana na kufikisha ujumbe kamili kwa jamii iliyokusudiwa
ii.
Fuata
mtiririko mzuri wa mawazo ili kupangalia
maudhui vizuri na kufanya yaeleweke kwa msomaji
iii. Tumia
lugha fasaha
iv. Zingatia
alama za uandishi
v.
Hakikisha
unamsamiati wa kutosha utakaokuwezesha kuandika na kujieleza vizuri
vi. Akikisha
unamifano ya kutosha
Kazi
1. Andika
tena sentensi zifuatazo, ukitumia alama za uandishi zifaazo.
(a) tanga
kuna machungwa mengi
(b)unataka
kufanya nini
(c) Nilikwambiaje
(d)leo
ni tarehe 29 agosti 2022
(e) Mimi
ni mwenyeji wa dodoma
(f) hassani
ni bondia mzuri
(g) nenda
dukani ukaninunulie mafuta ya kula mafuta ya kupaka na mafuta ya nywele
2. Tumia
ritifaa kusahihisha maneno yafuatayo.
(a) Ngoa
(b)Ngatuka
(c) Ngombe
(d)Ngoka
(e) Ngamua
3. Tumia
herufi kubwa kusahihisha uandishi wa nomino hizi za kipekee.
(a) tanzania
(b)mihambo
(c) ashura
(d)dodoma
(e) holoma
4. Tunga
sentensi tano zenye kukata maneno zinapofikia ukingoni mwa karatasi.
5. Tumia
alama za uandishi zifaazo kurekebisha kifungu kifuatacho.
namjua mkurugenzi wa shule ya sekondari helasita
kwa moyo wake mzuri anapenda kuona sisi wanafunzi tukifanya vizuri kwenye
masomo yetu siku moja alipotutembelea shuleni alituuliza je tunataka atuongezee
walimu wa somo gani mimi nilijibu pasi kuwatazama wenzangu kiswahili mwezi
mmoja baadaye alimleta mwalimu wa somo la kiswahili kutoka jiji la arusha
ambaye amekuwa chachu ya mafanikio ya shule ya helasita.
6. Fafanua
dhima tatu za aya.
7. Tumia
alama za uandishi zifaazo kusahihisha sentensi zifuatazo.
(a) nilijitahidi
kuwa mpole kwa wote mwalimu alisema
(b)
niombee ruhusa kwa mwalimu wa zamu joan alisema
(c) titi la mama ni tamu hata likiwa la mbwa ni
shairi zuri sana
(d)
mimi napenda kula ugali maharage na nyama
(e) ninapenda sana kipindi cha azam sports arena
Kazi
Chunguza picha ifuatayo kisha jibu maswali yanayofuata.
Picha ya mwanafunzi akiandika
insha huku karatasi yake ikionesha kichwa cha insha ni umuhimu wa sensa.
Maswali
1. Mwanafunzi
katika picha anafanya nini?
2. Kipi
ni kichwa cha insha anayoiandika mwanafunzi?
3. Andika
majina ya vifaa vyote anavyotumia mwanafunzi kuandika insha.
Dhana
ya insha
Insha
ni utungo wa maneno kuhusu jambo fulani. Ni mfululizo wa sentensi zinazohusiana
na mada inayozungumziwa au kuandikwa. Insha inaweza kuwa ndefu au fupi
kutegemeana na kusudi la mwandishi na mada anayoiandika. Insha hugawanywa
kwenye vifungu vya maneno vinavyoitwa aya. Kwa kawaida, aya hubeba wazo
maalumu.
Muundo
wa insha
Muundo wa insha umegawanyika katika sehemu
zifuatazo:
1. Kichwa cha
insha
Huandikwa kwa herufi kubwa juu ya karatasi ya
kuandikia, huwa katikati juu ya insha. Huandikwa kwa ufasaha na kwa kifupi
(muhtasari). Kichwa cha insha hakitakiwi kuwa na maneno mengi, kinatakiwa
kisizidi maneno matano(5) wakati mwingine hupigiwa mstari.Kichwa cha insha
wakati mwingine pia hujitokeza kikiwa katika wino mzito au uliokoza kwenye
baadhi ya maandiko kama vile magazeti.
2. Utangulizi /
Mwanzo wa insha
Sehemu hii huzingatia fasiri au
ufafanuzi wa jambo linalozungumziwa, uhusiano wake au muhtasari wa insha
inayotungwa. Kwa kawaida utangulizi hauzidi aya moja.
3. Kiini cha
insha
Hii ndiyo sehemu kuu ya insha. Huzingatia mawazo
makuu ambayo hupangwa katika aya zenye mtiririko wa mawazo. Huonesha kwa undani
maana ya jambo linalotungwa, kuenea kwake na uthibitisho wake.Sehemu hii
huandikwa aya zilizosheheni hoja mbalimbali kuhusu jambo linaloandikiwa insha.
4. Mwisho wa
insha (hitimisho)
Ni aya ya mwisho katika insha
ambayo huwa na maoni na mapendekezo ya mwandishi kuhusu jambo linalotungiwa
insha. Mwisho wa insha hautakiwi kuzidi aya moja.
Aina za insha
Kuna
aina mbili za insha ambazo ni:
(a) Insha
za wasifu
(b)Insha
za hoja
Katika
hatua hii ya kidato cha kwanza tutazungumzia insha za wasifu peke yake na aina
nyingine tutajifunza katika madarasa mengine.
Mambo
ya kuzingatia katika kutunga insha
Yapo mambo ya msingi ya kuzingatia wakati wa
utungaji insha. Mambo hayo ni haya yafuatayo:
1. Kuandika
kichwa cha insha na maelezo yote kama yapo.
2. Kuandika
kwa kufuata taratibu za uandishi na lugha ambayo ni fasaha. Mfano epuka kutumia
lugha ya mkato, yaani vifupisho kama vile n.k badala ya nakadhalika, k.m badala
ya kwa mfano, k.v badala ya kama vile, ktk badala ya katika. Andika neno lote
kama lilivyo, lakini pia unapoandika insha epuka kuandika nambari kwa tarakimu,
kwa mfano, kuandika 12 badala ya kumi na mbili. Andika nambari kwa maneno.
3. Andika
utangulizi unaovutia makini ya wasomaji au wasikilizaji. Utangulizi ambao
hauvutii humfanya msomaji au msikilizaji kuchoka na kutopenda kuendelea kusoma
au kusikiliza insha yako.
4. Andika
kiini cha insha yako kwa mpangilio unaofaa. Kila wazo kuu liandikwe kwenye aya
yake. Mawazo ya aya zote yahusiane.
5. Andika
mwisho wa insha unaovutia ili wasomaji wapende kurudia kusoma insha hiyo.
Insha
za wasifu
Ni aina za insha ambazo huelezea sifa nzuri au
mbaya za viumbe mbalimbali kama vile watu, wanyama, ndege, wadudu, mimea,
majengo, mahali na kadhalika.
Kazi
Tunga insha ya maneno mia tatu (300) kuhusu picha
hiyo hapo chini.
Picha
ya Mlima Kilimanjaro
Aina
za insha za wasifu
Kuna aina mbili za insha za wasifu.
(a) Insha
za wasifu za kisanaa
(b)Insha
za wasifu zisizo za kisanaa
(a)
Insha
za wasifu za kisanaa
Hizi
ni aina za insha ambazo hueleza kwa upana kuhusu sifa za watu, wanyama, mahali
na vitu kwa kutumia lugha ya kisanaa iliyosheheni tamathali za semi, mbinu
nyingine ya kisanaa, taswira, lugha ya kuvutia na matumizi ya semi kama vile
methali, nahau, mafumbo, vitendawili na misemo.
Mfano
wa insha ya wasifu ya kisanaa
MALAIKA SHULE YA MFANO TANZANIA
Helasita ni shule ya mfano Tanzania.
Hapa ni mahali ambapo wataalamu mbalimbali na magwiji wa kuunganisha mwili wa
binadamu hutengenezwa. Kila anayeingia Malaika hutoka akiwa ubongo wake
umenolewa kisawasawa.
Kuna shule nyingi sana nchini Tanzania,
lakini hii ni bora zaidi. Madarasa yake ni makubwa, mithili ya hekalu la Mfalme
Suleimani. Ndani ya madarasa kuna vibao vikubwa vilivyo nakshiwa maandishi
yanayotoa mwongozo na kanuni za shule, viti vya kukalia ni kama vile
wanavyokalia wageni wanaoingia Ikulu pale Magogoni. Upepo ukivuma kila darasa
humeza hewa ya kutosha kutoka kwenye maua na miti inayoizunguka shule hii.
Achilia hewa safi iingiayo kwenye madarasa, nje ya madarasa yetu kuna bustani
maridadi kuliko bustani ya Edeni.
Katika shule yangu Malaika, tunajivunia
uwepo wa walimu mahiri wa masomo mbalimbali, hakika walimu na wafanyakazi wa
shule hii ni werevu sana kwani hutuelimisha bila kukata tamaa wakiongozwa na
jemedari nambari moja ambaye ni Meneja wa shule yetu. Hakika kila mwanafunzi
anajisikia faraja maishani kwani hakuna mwanafunzi ambaye ni mbumbumbu.
Wanafunzi wa shule hii ni mafundi wa kutumia ubongo katika kutatua masahibu
mbalimbali yanayojitokeza.
Mambo mengine muhimu ya kujipigia kifua
katika shule hii ni majengo matakatifu yaliyotulia kama nguzo zibebazo Msalaba
wa Vatikani. Majengo mazuri yaliyokaa kama uyoga hupendezesha shule na kuifanya
shule kuwa kitovu cha maarifa. Maabara za kisasa na chumba cha wale wenye
kudonoa chombo cha kuandikia huvutia sana, bwawa la kuogelea nalo ni kivutio
kikubwa cha watu kutoka Ughaibuni.
Hata ningepewa mwaka mzima kuielezea
shule hii siwezi kumaliza. Nimeangalia afya za walimu, namna wanavyovaa, ngozi
zao zilivyo na vinyweleo vya manyunyumanyunyu ni ishara tosha kuwa Mkurugenzi
anaupiga mwingi kwenye kuwajali walimu na wafanyakazi wengine. Hii ndiyo Malaika,
shule ambayo inapatikana katika jiji la Dar es Salaam, wilaya ya Kigamboni .
(b)
Insha
za wasifu zisizo za kisanaa
Ni aina ya insha
ambazo hutumia lugha ya kawaida na rahisi na ya kueleweka. Insha za aina hii
hazina mahadhi ya kisanaa, matumizi ya lugha ya mjazo hayapo kwani mwandishi
hutumia lugha nyepesi na kutoa mifano halisi.
Mfano
wa insha ya wasifu isiyo ya kisanaa.
NYERERE KIONGOZI WA DUNIA
Mwalimu Julius Kambarage Nyerere anabaki
kuwa kiongozi wa kipekee sana Tanzania, Afrika na duniani kwa ujumla. Japo
alizaliwa kwenye familia ya Uchifu huko Mkoa wa Mara kwa Wazanaki, lakini
hakupenda kujikweza.
Mwalimu aliishi maisha ya kawaida,
hakuwa na ulinzi mkali, hakutembelea magari ya thamani na hata hakuwahi kujenga
nyumba ya thamani. Kumbuka nyumba yake ya kule Mwitongo, Butiama Mkoa wa Mara
alijengewa na serikali baada ya kuomba msaada.
Aprili kumi na tatu mwaka elfu moja mia
tisa na ishirini na mbili ndio mwaka aliozaliwa na mwaka elfu moja mia tisa
hamsini na tatu, akiwa kijana wa miaka thelathini na moja, wazee wapigania
uhuru wakati huo walimuamini na kumchagua kuwa mwenyekiti wa chama cha siasa
cha Tanganyika African Association (TAA).
Mwaka mmoja baadaye, yaani mwaka elfu
moja mia tisa hamsini na nne kwa kushirikiana na vijana wenzake akina Rashidi
Kawawa, Kambona, watoto wa Kleist Sykes, Dossa Aziz na John Rupia ambaye
inasadikika ndiye alikuwa anaongoza kwa utajiri kati ya Watanganyika wote wa
wakati huo, walipambana kwelikweli na serikali ya Mwingereza.
Walipambana mpaka waliposhinda kwenye
uchaguzi ambao ulisababisha Mwalimu Nyerere kuwa Waziri Mkuu Kiongozi wa kwanza
mweusi nafasi aliyoihudumu tangu Septemba mbili, mwaka elfu moja mia tisa na
sitini mpaka Mei moja, mwaka elfu moja mia tisa sitini na moja alipoamua
kung’atuka baada ya kuona yupo kwenye mfumo wa serikali ya Waingereza.
Mwaka huo huo, elfu moja mia tisa na
sitini na moja, Nyerere alifanikiwa kuongoza mapambano kwa nguvu zaidi na
kuudai uhuru kamili wa Tanganyika ambapo Desemba tisa, mwaka elfu moja mia tisa
sitini na moja Tanganyika ikawa huru. Bendera ya Uingereza ikashushwa Desemba
nane, mwaka elfu moja mia tisa sitini na moja saa tano na dakika hamsini na
tisa na bendera ya Tanganyika ikapandishwa Desemba tisa, mwaka elfu moja mia
tisa na sitini na moja saa sita kamili usiku
Baada ya kupata uhuru mwaka elfu moja
mia tisa na sitini na moja, Mwalimu Nyerere aliunda Baraza lake la mawaziri
lenye mawaziri kumi na moja tu, idadi ndogo kuliko serikali zote zilizofuata.
Mawaziri hao walikuwa vijana tupu wenye umri chini ya miaka thelathini na tisa
huku Nyerere mwenyewe akiwa na miaka thelathini na tisa.
Mwalimu Nyerere aliamini sana kuwekeza
kwa vijana ukiachilia mbali Baraza lake la Mawaziri kujaa vijana kwa asilimia
tisini na tisa, alisukumwa zaidi kwa sababu yeye mwenyewe alianza harakati za
kupigania uhuru wa nchi yake akiwa kijana. Huyu ndiye Mwalimu Julius Kambarage
Nyerere ambaye dunia nzima inamkumbuka kwa ujasiri wake na uongozi ulio bora.
Uandishi wa barua
Picha
ya mwanafunzi anaandika barua
Barua ni mojawapo ya njia ya mawasiliano kama
ilivyo simu, kadi nakadhalika. Kuna aina nyingi za barua. Baadhi yake ni hizi
zifuatazo: Barua za kirafiki, barua rasmi, barua za magazeti, barua za mialiko nakadhalika.
Barua
za kirafiki
Hizi ni barua ambazo huandikwa kwa marafiki,
wazazi na ndugu wengine. Barua hizi humpa uhuru mwandishi kuandika barua yake
akitumia lugha isiyo rasmi (kama anavyopenda). Uhuru huu humpa mwandishi wa
barua ruhusa ya kuandika barua yenye urefu anaotaka. Mwandishi wa barua hii na
anayeandikiwa huwa wanajuana vizuri kiasi cha kuandikiana barua wakitumia lugha
ya kawaida waliyoizoea.
Kazi
Utajuaje kuwa barua
uliyoandikiwa / uliyoandika ni barua ya kirafiki? Fafanua.
Mambo
ya kuzingatia wakati wa kuandika barua za kirafiki
1. Anwani ya
mwandishi
Huandikwa
juu upande wa kulia wa karatasi. Huwa na muundo wa mshazari, wakati mwingine
huwa wima, mkato, kituo na taratibu nyingine za uandishi huzingatiwa.
Mfano
Shule ya sekondari Helasita, S.L.P 11639, Dar es salaam.
Mkao
wima.
au
Shule ya sekondari
Helasita,
S.L.P 11639, Mkao mshazari
Dar es salaam.
2. Tarehe ya
kuandika barua
Huandikwa
chini ya anwani ya mwandishi wa barua . Lengo
ni kumjulisha mwandikiwa lini barua iliandikwa. Tarehe huweza kuandikwa kwa
mitindo mbalimbali kama vile:
24 Septemba 2022
24 – 9 – 2022
24 . 9 .2022
24 / 9 / 2022
Septemba 24, 2022
Baada
ya tarehe kuandikwa, mwandishi wa barua aruke mstari mmoja.
3. Mwanzo wa
barua
Huanzia upande wa kushoto karibu
kabisa na mstari wa pambizo. Maneno yanayoweza kutumika mwanzoni mwa barua ni
kama vile; mpenzi baba, mama mpendwa, ndugu mpendwa, shangazi mpenzi, kwako
kaka, dada yangu mpendwa. Baada ya mwanzo, aya fupi ya salamu hufuata.
4. Kiini cha
barua
Hii ni sehemu muhimu sana katika
barua kwani ndio sehemu ambayo mwandishi hueleza lengo lake la kuandika barua.
Katika sehemu hii mwandishi huweza kueleza kusudi lake. Mfano kusalimia, kuomba
msaada, kutoa pongezi na kadhalika. Kiini kinaweza kuwa na aya moja au zaidi
ambayo mwandishi angependa kuwasilisha kwenye barua yake.
5. Mwisho wa
barua
Sehemu hii huwa na salamu za
maagano. Salamu hizi hutegemea pia uhusiano uliopo baina ya mwandishi na
mwandikiwa. Maneno ambayo mara nyingi hutumiwa wakati wa kumaliza barua ni kama
yafuatayo:
Wasaalamu
Wako akupendaye
Wako wa moyoni
Kwa heri
Rafiki yako akupendaye
Leo naishia hapa, na
kadhalika.
6. Jina la
mwandishi
Sehemu hii ni muhimu sana kwani
humsaidia yule anayepelekewa barua kufahamu barua imetoka kwa nani. Iwapo barua
imechapwa kwa mashine (taipureta au kompyuta), mwandishi huandika jina lake
kamili, kama imeandikwa kwa mkono mwandishi ataandika jina lake kamili au jina
moja tu. Endapo barua itazidi ukurasa mmoja, kurasa hizo itabidi zipewe
namba.Ikumbukwe kuwa barua za kirafiki hazina kipengele cha Saini ya mwandishi
wa barua.
Kielelezo cha muundo wa barua ya
kirafiki
Anuani ya mwandishi Tarehe Salamu Mwanzo wa barua
Kiini
cha barua Mwisho wa barua Jina la mwandishi
Mfano wa barua ya
kirafiki / kindugu
Shule ya
Sekondari Azimio, S.L.P 284, Arusha. 26/09/2022. Baba mpendwa, Salamu
sana. Habari za siku nyingi? Abigael hajambo? Mama naye hajambo? Mimi ni
mzima kabisa na ninaendelea vizuri na masomo yangu hapa shuleni. Dhumuni
la barua hii ni kutaka kukujulisha kuwa mimi ni mzima na ninaendelea vizuri
na masomo yangu japo najisikia mpweke sana kutokana na kwamba sikuzoea
kukaa mbali nanyi wazazi wangu. Baba,
naomba umwambie mama, asisahau kuniombea kwa Mungu ili nifaulu vizuri
katika mitihani yangu yote. Naomba pia usisahau kunitumia pesa ya matumizi
ili niweze kununua mboga mboga na dagaa kantini hasa siku ya ugali na
maharage. Kwa
leo naishia hapa, wasalimie wote wanaonifahamu hasa majirani zetu wote. Ni mimi mwanao Triphonia.
Kazi
1. Wewe
ni mwanafunzi wa kidato cha kwanza katika shule ya sekondari Mawasiliano, S.L.P
145, Morogoro. Mwandikie barua shangazi yako ambaye ni Mkuu wa shule katika
shule ya sekondari Mawenzi S.L.P 342 Singida ukimwomba akutumie pesa ya
matumizi. Jina lako ni Furaha Falisha.
2. Chora
kielelezo cha muundo wa barua ya kirafiki kisha ufafanue umuhimu wa kila
kipengele.
3. Andika
barua kwa mlezi/mzazi wako ili umweleze siku utakayowasili nyumbani baada ya
kumaliza mtihani wako wa mwisho wa mwaka. Jina lako liwe Seba Bwiri, jina la
mlezi/mzazi wako liwe George Bwiri Mahaba wa S.L.P 280 Musoma. Anuani yako iwe
S.L.P 25458 Dar es salaam.
Uandishi
wa anuani juu ya bahasha
Mwandishi
wa barua amalizapo kuandika barua, huikunja na kuiingiza kwenye bahasha na
kuipeleka posta tayari kwa kuituma kwa mlengwa. Mara nyingi juu ya bahasha ni
lazima kuwekwe stempu ambayo ndio hubeba gharama ya kuisafirisha barua hiyo
kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine. Stempu hubandikwa juu ya bahasha
upande wa kulia juu nchani mwa bahasha. Anuani inayoandikwa juu ya bahasha huwa
na muundo maalumu kama ifuatavyo:
STEMPU SEPHANIA
KAZUMBA, S.L.P
23, BUKENE – NZEGA.
Zoezi la Mada
1. Chagua
herufi ya jibu sahihi katika vipengele (i) hadi (v) kisha andika herufi ya jibu
hilo katika sehemu ya kujibia.
i)
Ni sehemu gani
katika muundo wa insha za wasifu huonesha mapendekezo ya mwandishi kuhusiana na
jambo linalojadiliwa?
A. Kichwa
cha insha
B. Hitimisho
C. Kiini
cha insha
D. Utangulizi
E. Hoja
za insha
ii)
Ipi ni hatua
ya mwisho ya kuzingatia katika kuandika ufupisho wa habari uliyosoma?
A. Kuhesabu
idadi ya maneno
B. Kutambua
mawazo makuu
C. Kusoma
kwa makini
D. Kuandika
idadi ya maneno
E. Kuandika
kichwa cha habari
iii)
Ipi ni alama
ya uandishi inayotumika kuonesha sehemu mbili za sentensi zilizo kinyume?
A. Nukta
pacha
B. Mkato
C. Nukta
mbili
D. Nukta
mkato
E. Nukta
mtajo
iv)
“Nitawaadhibu wote”, Mwalimu
Gudilla alisema. Ni alama ipi ya
uandishi imetumika katika sentensi nitawaadhibu wote?
A. Alama
ya mshangao
B. Alama
ya ritifaa
C. Alama
ya mtajo
D. Alama
ya mjalizo
E. Alama
ya kushangaa
v)
Lipi kati ya
maneno yafuatayo huandikwa mwanzoni mwa barua ya kirafiki?
A. Saini
ya mwandishi
B. Dada
yangu mpendwa
C. Tarehe
D. Anwani
ya mwandishi
E. Jina
la mwandishi
2. Oanisha
maana za dhana za alama za uandishi zilizo katika Safu A kwa kuchagua herufi ya dhana husika katika Safu B kasha andika herufi husika katika
sehemu ya kujibia.
Safu A |
Safu B |
i)
Huonesha vipimo mbalimbali
katika desimali ii)
Hutumika ili kupumzika katika
sentensi iliyo ndefu sana iii)
Huonesha uwiano baina ya
namba iv)
Hutumika badala ya nukta
mbili v)
Huonesha maana ya ziada
katika sentensi |
A. (:) B. (-) C. (;) D. (.) E. (
) F. (?) G. (!) |
3. Panga
vipengele vifuatavyo kwa kufuata muundo wa barua ya kirafiki.
i)
Salamu za
awali
ii)
Tarehe
iii)
Furaha Amani
iv)
Shule ya
Sekondari Kifungilo, S.L.P 248 Tanga
v)
Barua yenyewe
4. Andika
maneno matano (5) kutokana na jedwali lifuatalo na ueleze umuhimu wa maneno
hayo kama yanavyoweza kutumika katika barua ya kirafiki.
A |
M |
W |
A |
N |
Z |
O |
W |
A |
B |
M |
N |
A |
M |
A |
E |
E |
A |
U |
A |
A |
U |
U |
L |
A |
S |
A |
S |
Y |
R |
T |
L |
A |
A |
S |
P |
T |
L |
N |
U |
A |
K |
J |
I |
N |
A |
B |
P |
N |
A |
N |
Z |
A |
I |
E |
I |
B |
E |
D |
E |
O |
O |
K |
L |
N |
E |
T |
I |
O |
A |
T |
A |
R |
E |
H |
E |
E |
I |
N |
A |
5. Tumia
vipengele vilivyomo kwenye kisanduku kujaza muundo wa barua ya kirafiki
uliyopewa.
Anwani ya mwandishi, Jina la
mwandishi, Tarehe ya kuandika barua, Mwanzo wa barua, Mwisho wa barua,
Barua yenyewe
6. Tia
alama za uandishi zifaazo kusahihisha sentensi zifuatazo.
(a) Wanafunzi
walisema kwa pamoja tutashinda
(b)Daudi
alikuwa kibaraka cha wazungu
(c) Rebeka
George Kyamba aliwaeleza wanafunzi wamesema tutasoma kwa bidii
(d)Endelea
twasikiliza hivyo basi Meneja aliendelea.
7. Andika
insha yenye maneno yasiyopungua mia mbili (200) na yasiyozidi mia mbili na
hamsini (250) juu ya mada moja kati ya zifuatazo.
(a) Ajali
za barabarani
(b)Nilipomaliza
darasa la saba
(c) Umuhimu
wa kujisomea
(d)Madhara
ya ajira kwa watoto
(e) Unyanyasaji
wa kijinsia.
8. Badilisha
kadi ya mwaliko ifuatayo iwe barua ya kirafiki.
MWALIKO
WA HARUSI Familia
ya Mzee Charles Swai wa Dar es salaam, wanayo furaha kubwa sana
kukualika/kuwaalika Prof/Dkt/Shekhe/Padri/Bw/Bi Bi
Asha Kizuki Kwenye
harusi ya kijana wao mpendwa Godson Swai Itakayofanyika
katika Ukumbi wa diamond jubilee siku ya Jumamosi tarehe 6/8/2022 kuanzia
saa moja jioni. Kufika
kwako ndiyo mafanikio ya shughuli hii Majibu
( kwa wasiofika tu) Gloria
Swai. Simu
na. 0684 224 944
9. Fafanua
mambo matano ya kuzingatia unapoandika insha ya wasifu.
10. Chunguza picha ifuatayo kisha
tunga insha isiyopungua maneno mia moja.
Picha
ya vijana wakitumia sindano za dawa za kulevya
0 maoni:
Post a Comment