14 Jul 2025

 

Kuwasiliana kwa njia ya mazungumzo

Dhana ya Mazungumzo.

Mazungumzo ni utaratibu wa kuongea baina ya pande mbili ambapo wahusika wa mazungumzo hayo huwa ni watu. Kwa kawaida mazungumzo huwasilishwa kwa njia ya mdomo na huweza kuambatana na ishara za viungo vya mwili. Chanzo cha mazungumzo huwa ni mzungumzaji na kikomo chake huwa ni msikilizaji.

Mzungumzaji huwa ni mtu anayeanzisha uneni, huyu kifasihi huitwa fanani. Uneni ni utoaji wa matamko yenye maana katika lugha fulani ilihali kitendo ni dhana ya utendaji . Msikilizaji huwa ni mtu anayepokea uneni kutoka kwa mzungumzaji huyu kifasihi huitwa hadhira.

Misingi ya Mazungumzo

Ili watu waweze kuelewana vizuri wanapozungumza ni lazima wazingatie mambo makuu yafuatayo,Pia mambo hayo yasipozingatiwa yanaweza kuathiri mazungumzo ya wazungumzaj

(i)           Uhusiano wa wazungumzaji

Unaweza kuelewa na kutambua uhusiano wa watu wanaozungumza kama ni marafiki , wapenzi, baba na mtoto au mwalimu na mwanafunzi watu au wazungumzaji ni maadui kwa kuangalia msamiati wanayotumia katika mazungumzo yao. Msamiati wanayotumia katika mazungumzo yao. Msamiati anayotumia mwalimu na mwanafunzi wake ni tofauti sana na msamiati anayotumia mtoto na wazazi wake kwa sababu , msamiati utakaotumika na mwalimu na mwanafunzi  wake hutawaliwa na heshima busara na ulezi zaidi tofauti na msamiati utakaotumika na mtoto na wazazi wake kwani yenyewe hatawaliwa na madoido, madokezo na mabembelezo zaidi.

(ii)         Mada inayozungumzwa

Mazungumzo hutawaliwa na mada , mazunguzumo huhusisha mada inayozungumzwa ambayo pia huamua msamiati kwa kutumia katika mazungumzo husika. Kwa mfano mada inaweza kuwa siasa, masomo, sherehe au muziki. Wazungumziaji wana takiwa kuchagua msamiati kulingana na mada. Kwa mfano mada ya masomo inaweza kuibua msamiati kama vile elimu, itifaki.

(iii)       Muktadha wa Mazungumzo

Mazungumzo huathiriwa na miktadha tofauti tofauti muktadha wa mazungumzo unaweza kuwa rasmi au usiwe rasmi, kuna miktadha mbalimbali ambayo wazungumziaji huweza kutumia wakati wa mazungumzo yao. Miktadha kama hiyo ni shuleni, dukani, mjini, barabarani, kijijini n.k . Kwa mfano , lugha anayotumia daktari hospitalini ni tofauti na lugha anayotumia daktari huyohuyo akiwa nyumbani kwake hivyo lugha hutofautisha kulingana na muktadha wazungumzaji wanapaswa kuzingatia muktadha wa mazungumzo yao.

Mfano.

Mazungumzo ya mama na mwanae wakiwa kwenye daladala.

MTOTO:Mama , mbona kila siku baba anakupiga?

MAMA:Chukua andazi mwanangu.

 

Kwa mfano huu, Mama amezingatia muktadha ndio maana hahitaji mazungumzo yaendelee , kwani mada husika haifai kuzungumziwa kwenye daladala

(iv)        Lengo la mazungumzo

Mzungumzaji huwa na lengo la kuzungumza anapokutana na mwenzake ili kukidhi lengo la mazungumzo, mzungumzaji huhitaji kutoa ufafanuzi wa yale anayoyasema ili msikilizaji aelewe kama ilivyokusudiwa . Lengo la mazungumzo linaweza kuwa kutoa taarifa , kuhoji, kukejeli ,kuelimisha ,kuonya au kutia moyo.

(v)          Muda /wakati wa mazungumzo

Mzungumzaji ni lazima ateue msamiati utakaoendana na wakati katika eneo husika . Matumizi mabaya ya muda katika eneo amabalo si rafiki hufanya mazungumzo kuchosha.

(vi)        Utanzu au aina ya mawasiliano

Kabla ya mazungumzo , mzungumziaji ni lazima ajiulize kwamba ujumbe aliokusudia kufikisha kwa hadhira ataufikisha kwa mbinu ipi? Mbinu ya majadiliano, masimulizi, hotuba au nyimbo.

(vii)      Shughuli inayofanyika

Msamiati unaotumika katika mazungumzo huendana na shughuli inayohusika kwa mfano kama shughuli inayofanyika ni ufugaji , uchimbaji madini na msamiati wake utaendana na shughuli husika.

Mifano ifuatayo inaonesha mazungumzo katika miktadha tofauti.

Mfano 1 Mazungumzo ya kanisani

 

MCHUNGAJI: Bwana Yesu apewe sifa

WAUMINI: Amina

MCHUNGAJI: Naomba mfungue biblia zenu.

 

Mfano 2 Mazungumzo ya marafiki.

 

BAHATI: Mambo sanura?

SANURA: Poa tu vipi wewe?

BAHATI :Fresh rafiki yangu, vipi jana mama hakukutia ndimu ulipochelewa kurudi?

SANURA: Loo! Mama Yule na ule mdomo wake, alinichimba biti sana.

 

Mfano 3. Mazungumzo ya shuleni

 

MWANAFUNZI:Shikamoo mwalimu

MWALIMU: Marahaba , hujambo?

MWANAFUNZI: Sijambo

 

 

(viii)    Hali za wahusika wakati wa mazungumzo

Lugha inayotumika inapaswa kuendana na hali za wahusika wakati wa mazungumzo ili kuleta maelewano . kwa mfano kama mzungumzaji ni mgonjwa au amekasirika, lugha inayotumika kuwasiliana naye itaendana na hali hiyo.

Andaa mazungumzo yanayoweza kuzungumzwa katika maeneo yafuatayo;

a)     Hospitalini

b)     stendi ya mabasi

c)     Dukani

d)     Sokoni

e)     Shuleni

 
ZOEZI

 

 

 

 

 

 

Hatua za kufanya mazungumzo katika lugha ya kiswahiliKatika kufanya mazungumzo zipo hatua mbalimbali za kufuata wazungumzaji wanapokutana kuzungumza , Hatua hizo ni hizi zifuatazo;

Salamu

Watu wawili wanapokutana kuzungumza sharti wasalimiane kabla ya kuanza mazungumzo hayo, Jambo la kwanza huwa ni salamu, salamu hii huwa rasmi au isiyo rasmi kutegemea na uhusiano uliopo baina ya wazungumzaji , Salamu rasmi inaweza kuwa kama ifuatavyo; Habari za asubuhi na habari za kazi, Salamu zisizo rasmi inaweza kuwa hujambo? Mambo, vipi hali yako, kumbuka kuwa “kwa heri “ siyo salamu.

Utambulisho

Wazungumzaji wanapokutana wana nafasi ya kutambuana . kipengele hiki hufanyika mara baada ya wahusika kusalimiana katika utambulisho wazungumzaji hutaja majina yao na wasifu wao kwa ujumla. Kwa mfano, unaitwa nani, wewe ni nani?. Hii huwasaidia wazungumzaji kujenga mipaka, uhusiano na mazoea , ukimtambua mtu unayezungumza naye itakupa urahisi wa kuchagua msamiati utakaotumia unapozungumza naye.

 

Mazungumzo mafupi

Mara baada ya utambulisho , wazungumzaji hufanya mazungumzo mafupi kwa nia ya kutaka dhima ya mazungumzo yao.

Mazungumzo kamili

Mazungumzo kamili hutegemea muktadha, lengo la mazungumzo , mada ya mazungmzo na uhusiano uliopo baina ya wazungumzaji . Ni sehemu hii ambayo hutumia muda mrefu wakati wa mazungumzo.

 

Ufafanuzi

Ni kipengele kinachohusu mambo yote ambayo hayakueleweka kwa mmoja kati ya wazungumzaji ,hivyo kurudiwa na kutolewa maelezo ya ziada.

Kukatisha Mazungumzo

Kipengele hiki ni muhimu sana wakati wa mazungumzo, mathalani umetembelewa na ndugu yako ofisini kwako, kwa bahati mbaya ndugu yako huyo anaongea sana kiasi kwamba wageni wengine wanalalamika nje ya ofisi inakupasa ukatishe mazungumzo . zipo njia mbalimbali za kukatisha mazungumzo mfano, kama umekaa kwenye kiti unaweza kusimama kisha kumsogelea na kumpa mkono mtu unayezungumza naye ukaongea naye kwa maneno kama vile “Nitakushukuru, karibu tena, tuonane wakati mwingine n.k

Kuagana

Tumia maneno kulingana na muktadha mfano kama ni ofisini waweza kutumia maneno rasmi kama vile “Nakutakia kazi njema, kila la kheri , tuonane wakati mwingine na unaweza kutumia maneno kama vile baadaye furahia siku yako katika muktadha usio rasmi.

 

 

Lugha fasaha

Lugha fasaha ni ile ambayo inafuata taratibu zote za lugha hiyo ikizingatia maana, matamshi, muundo na mantiki. Lugha inapotumika vibaya huweza kupotosha lengo la mzungumzaji. Makosa haya yanaweza kujitokeza katika msamiati (maana) miundo, matamshi na mantiki. Kwa mfano, Kurara, neno hili si neno fasaha kwa sababu katika lugha ya Kiswahili hutamkwa kulala. Ili mazungumzo yaweze kuwa mazuri, wazungumzaji lazima watumie lugha kwa ufasaha. Angalia makosa mbalimbali ambayo huweza kufanywa na watumiaji wa lugha fasaha katika misingi ya maana, miundo, matamshi, kuacha baadhi ya maneno, kuongeza vitamkwa au silabi, makosa katika matumizi ya nyakati na mantiki.

 

(i)           Makosa ya kimaana / Kimsamiati

Ili lugha iwe fasaha ni sharti neno lililokusudiwa liwe fasaha. Kuna maneno mengi yenye maana zaidi ya moja. Maneno haya ni kama vile, kaa, kata, chungu, mbuzi, kanga, barabara, panda, susa, kanda.

Tazama namna maneno haya yanavyoweza kuleta dhana nyingine:

§  Susa -        Tikisa mti

-           Uchafu utokanao na mabaki ya chakula

-           Kataa kufanya jambo

-           Sehemu ya muwa isiyo tamu

 

§  Kata -        Eneo la kijiografia

-           Gawanyisha kitu katika vipande

-           Chezesha viungo vya mwili kama vile macho,kiuno shingo.

Hapa ndipo maneno kuwakilisha badala ya kuwasilisha, baada badala ya badala hufafanuliwa.

Mfano

l   Mvu imepiga sana usiku  badala ya mvua imenyesha sana usiku

l   Mwalimu alidondoka mlangoni badala ya mwalimu alianguka mlangoni

l   Spika alimwasilisha Rais badala ya spika alimwakilisha Rais

l   Ashura amenona sana badala ya Ashura amenenepa sana

l   Ng’ombe amejifungua badala ya ng’ombe amezaa

Baadhi ya maneno ambayo tofauti zake za kimaana zinatofautishwa na mkazo katika jinsi neno linavyotamkwa.

 

(ii)         Makosa ya kimuundo

Mpangilio mzuri wa maneno katika sentensi hufanya lugha kuwa fasaha. Mfuatano wa maneno husaidia kuleta maana iliyokusudiwa. Kwa mfano “Wanaitwa wanafunzi badala ya Wanafunzi wanaitwa”. “Kizinga anaitwa na Juma” badala ya Kizinga na Juma wanaitwa.

 

(iii)       Makosa ya kimatamshi

Matamshi mazuri ya sauti za lugha hujenga ufasaha wa lugha hiyo. Watu wengine hushindwa kutamka baadhi ya sauti za Kiswahili kwa sababu ya athari za lugha mama na athari za kimaumbile, hususani kithembe, kibogoyo na toinyo. wengine huchanganya na kubadili sauti hizo. Mifano ya maneno haya ni kama yafuatayo:

Ÿ  Ngombe badala ya ng’ombe

Ÿ  Mbusi badala ya mbuzi

Ÿ  Kurara badala ya kulala

Ÿ  Zambi badala ya dhambi

Ÿ  Langi badala ya rangi

Ÿ  Zarura badala ya dharura

Ÿ  Ntu badala ya mtu

Ÿ  Thatha badala ya sasa.

(iv)Makosa ya kimuundo
Haya ni makosa ambayo hutokana na kutokuwa na mpangilio mzuri wa maneno katika sentensi.Mara nyingi sentensi za Kiswahili kimuundo huanza na nomino au kiwakilishi,kisha hufuatiwa na kivumishi,hufuata kitenzi na kisha aina nyingine za maneno.Baadhi ya wazungumzaji hushindwa kufuata utaratibu huu na kujikuta wakikosea kama mifano ifuatavyo inavyoonekana;Kiti mimi nina badala ya mimi nina kiti.
   Mama chakula anapika badala ya Mama anapika chakula
(v)Makosa ya kuongeza vitamkwa.
     Ni makosa ambayo hufanywa na watumiaji wa lugha kwa
     kuongeza vitamkwa au silabi katika maneno sehemu
     ambapo hapatakiwi.Mara nyingi makosa kama haya
     husababishwa na athari za lugha mama.
      Mfano;
      Msichana msafi anaitwa badala ya msichana safi anaitwa.
      Mimi nakuambiaga badala ya mimi huwa nakuambia.
      Mashuleni pawe safi badala ya shuleni pawe safi.

(vi)Makosa ya kuacha maneno
      Ni makosa ambayo watumiaji wa lugha huacha kuyatamka au kuyatumia baadhi ya maneno fulani katika sentensi wakiamini kuwa ujumbe walioukusudia utakuwa umefika kwa hadhira.
Mfano,
Baba amerudi kazini badala ya baba amerudi kutoka kazini.

          

(vii)Makosa ya Mantiki

Ni utaratibu mzuri wa kufikiri ili kupata maana iliyolengwa. Kwa mfano:

-      Mfupa hauna ulimi badala ya ulimi hauna mfupa.

-      Chai imeingia nzi badala ya nzi ameingia kwenye chai.

-      Nimemkuta hayupo badala ya sijamkuta.

-      Kitumbua kimeingia mchanga badala ya mchanga umeingia ndani ya kitumbua.

 

Umuhimu wa kutumia lugha kwa ufasaha

·         Hufikisha ujumbe uliokusudiwa kwa urahisi zaidi.

·         Huifanya lugha kuwa na thamani na hadhi kubwa.

·         Huwavutia watu na kuwafanya kujifunza lugha kirahisi.

·         Huifanya lugha ikubalike ndani na nje ya nchi.

·         Huboresha uhusiano wa watumiaji wa lugha husika.

·         Hufanya lugha iwe na mvuto na yenye kushawishi watumiaji wapya.

·         Hudumisha sarufi ya lugha.

·         Hukuza na kuendeleza utamaduni wa jamii.

Athari za kutotumia lugha kwa ufasaha

(i)           Kupata maana ambayo haijakusudiwa.

(ii)          Watumiaji kutoelewana.

(iii)        Lugha kushuka hadhi yake na kuonekana kama ni lugha ya wahuni.

(iv)         Inaweza kuchochea ugomvi baina ya watumiaji kutokana na kutoelewana hasa wakati wa utumiaji wa msamiati.

(v)          Kuondoa umoja na mshikamano kwa sababu tu lugha ndio kiunganishi cha watu hasa wanaoelewana.

 (vi)Hudumaza utamaduni wa jamii.

 (vii)Husababisha ujumbe ushindwe kufika kama ulivyokusudiwa.                                           

 

 

 

Zoezi la mada

1.   Chagua herufi ya jibu sahihi katika vipengele (i) – (v), kisha andika herufi ya jibu hilo katika sehemu ya kujibia.

(i)           Mawasiliano baina ya wanyama, ndege na wadudu hayawezi kuitwa lugha kwa sababu gani?

A.   Vitamkwa vyao ni hafifu

B.   Lugha ni mali ya wanyama tu

C.   Vitamkwa vyao havina maana

D.  Vitamkwa vyao havina irabu

E.   Vitamkwa vyao ni vya msingi katika utamkaji

(ii)          Kanuni maalumu na taratibu za lugha zinazofuatwa na wazungumzaji katika mawasiliano huitwaje?

A.   Lugha    B. Sarufi   C. Lugha fasaha   D. Utumizi wa lugha   E. Mawasiliano

(iii)        Neno abab halikubaliki lakini neno baba linakubalika kwa sababu gani?

A.   Mpangilio wa neno

B.   Mpangilio wa irabu

C.   Mpangilio wa vitamkwa

D.  Mpangilio wa fonimu

E.   Mpangilio wa mofimu

(iv)         Dhima kuu ya lugha katika mawasiliano ni ipi kati ya hizi zifuatazo?

A.   Kutambulisha utamaduni

B.   Kutunza historia

C.   Kupashana habari

D.  Kuelimisha jamii

E.   Kuburudisha jamii

 

 

 

(v)          Zipi ni aina mbili za fonimu katika lugha ya Kiswahili?

A.   Irabu na konsonanti

B.   Irabu na silabi

C.   Irabu na mofimu

D.  Konsonanti na kiambishi

E.   Foni na alofoni

2.   Oanisha dhana zilizopo safu A na mifano yake iliyopo safu B kwa kujaza herufi ya jibu sahihi kwenye safu A.

 

Safu A

Safu B

(i)           Vokali

(ii)          Haitamkiki bila kuwekewa irabu

(iii)        Huundwa kwa sauti ya konsonanti

(iv)         Huundwa na irabu pamoja na konsonanti

(v)          Huunda lugha

A.   Sauti

B.   Neno

C.   Silabi

D.  Konsonanti

E.   Lugha

F.   Mfumo

G.  Nasibu

 

3.   Panga fonimu hizi kwa utaratibu unaofaa ili kujenga neno la Kiswahili.

(a)  Ambit

(b)  Awsa

(c)  Ynmzaa

(d)  Orsdai

(e)  ngzoao

4.   Eleza kwa kifupi dhima kuu tano za lugha

5.   (a)      Fafanua maana ya lugha fasaha

(b)      Fafanua madhara matano (5) ya kutumia lugha isiyo    fasaha

6.   Eleza tofauti baina ya sauti hizi

(a)  /a/ na /p/

(b)  /g/ na /t/

(c)  /f/ na /ng/

(d)  /th/ na /n/

(e)  /w/ na /y/

7.   Eleza maana ya dhana zifuatazo

(i)           Lugha

(ii)          Lugha fasaha

(iii)        Irabu

(iv)         Konsonanti

(v)          Silabi

8.   Sahihisha sentensi zifuatazo

(a)  Doto ameungama zambi zake

(b)  Watoto walirara sakafuni

(c)  Mzee Kapinga anapaka langi nyumba yote

(d)  Masanja amewasili jana kutoka ngambo

(e)  Mbusi hii inapenda kutoroka sana.

9.   Eleza maana mbili za kila neno

(a)  Paa

(b)  Vua

(c)  Panda

(d)  Randa

(e)  Kanda

10. Fafanua mambo ya kuzingatiwa ili kuwezesha mawasiliano katika mazungumzo.

 

0 maoni:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Wasiliana nami papo kwa papo

Name

Email *

Message *

Ads 468x60px

Breaking News

Top Featured

Featured Posts

Sample text

Sample Text

Recomended

Facebook

Advertise

Most Popular

Connect With Us

Followers

Social Icons

Pages

Pages

BTricks

Pages

Popular posts

Tafuta chochote ukiwa hapahapa

Kategori

Recent Comments

You can replace this text by going to "Layout" and then "Page Elements" section. Edit " About "

recent posts

Video Of Day

TRANSLATE

Instructions

Video

Flickr Images

FURAHIA UWEPO WAKO HAPA

Logo Design by FlamingText.com
Logo Design by FlamingText.com

Imetembelewa mara

NUMBER OF VIEWERS

Popular Posts

SAJIRI

Definition List

premium-wordpress-themes.org