18 Jun 2025

 Imeandaliwa na Mtila Mswahili


1.0 UTANGULIZI.

Kwa mujibu wa kamusi la Kiswahili Sanifu (TUKI). (2004). Utamaduni ni mila, asili, jadi, na desturi za kundi Fulani.

Loliyong. (1972). Utamaduni ni jumla ya shughuli kumbukumbu na mipango ya baadae ya jamii fulani zikiwemo pia ndoto na maono ya jamii hizo.

Ibrahim, H. (2005). Jumla ya mambo yote yanayobuniwa na jamii ili kukidhi utashi na maendeleo ya jamii.

Ni mwenendo wa maisha ya jamii na mtazamo wao, na mambo na taratibu zao za kuendesha maisha ambazo huwatofautisha na jamii nyingine. Kutokana na maelezo hayo ni wazi kuwa utamaduni huipa upekee na kuifanya kutambuliwa kwa njia maalumu. Jamii yoyote inayotaka kuendelea kutambulika na kuenziwa ni sharti iwe na upekee katika vipengele mbalimbali vya kiutamaduni. Tunatambua kuwa, mila na desturi hujengwa kutokana na kurithishwa kutoka kizazi kimoja hadi kingine. Iwapo jambo hili halitotekelezwa kuna uwezekano mkubwa wa kufifia kwa utamaduni uliopo katika jamii hiyo na hata kupotea kabisa kwa wazanzibar.

Vipindi mbalimbali vilivyopitia utamaduni wa Zanzibar. Baada ya mapinduzi ya Zanzibar 1964/01/12 utamaduni wa Zanzibar ulianza kubadilika.

Kuanzia Mwaka 1964 mpaka 1979: Utamaduni wa Zanzibar ulijionesha katika vipengele mbali mbali kama vinavoelzwa hapo chini.

1.1 MALENGO

1.1.1 Lengo kuu.

Ni kuonesha mabadiliko ya kiutamaduni katika vipindi mbali mbali baada ya mapinduzi matukufu ya Zanzibar hadi sasa.

1.1.2 Malengo madogo

  1. Kuonesha historia ya utamaduni wa mswahili Zanzibar baada ya uhuru
  2. Kuonesha maendeleo ya kiutamaduni wa mswahili hapa Zanzibar.
  3. Kuonesha mabadiliko ya utamaduni wa mswahili hapa Zanzibar.
  4. Kuonesha ushahidi kutokana na utamaduni wa mswahili halisi.

2.1 HISTORIA YA ZANZIBAR.

Zanzibar ni muunganiko wa visiwa viwili ambavyo ni Unguja na Pemba, ambapo ndani yake muna visiwa vingine vidogo vidogo vilivyozungukwa na bahari ya Hindi katika pande zake zote, Zanzibar pamoja na visiwa hivyo vina historia ya kweli ya muda mrefu sana kutokana na matokeo na mambo mbalimbali yaliyoijenga historia hiyo. Zanzibar ilikuwa imetawaliwa na wakoloni mbalimbali wakiwemo Waengereza, Wajerumani, Waarabu, Wapashia, na Wareno. Kila koloni lilikuwa na tamaduni zake walizotoka nazo kutoka katika nchi zao na kuziendeleza katika visiwa vya Zanzibar kurithisha kizazi hadi kizazi.

Wakoloni hawa waliitawala Zanzibar kwa muda mrefu na kuanzisha mambo mbalimbali ya kiuchumi kwa manufaa yao. Wakati mapinduzi ya Zanzibar 12/01/1964. Yaliyoongozwa na Muasisi wa mapinduzi hayo Shekhe Abed Aman Karume.

Tayari tamaduni zote walizokuja nazo wakoloni zilikuwa zilishaenea na kuendelezwa na

wazanzibar waliowengi.


Picha.na 1.0. inaonesha wanafunzi wa chuo kikuu SUZA wakiongea na mwanahistoria wa mambo ya kale na utamaduni katika eneo la Dunga.

 

 

3.1 UTAMADUNI WA ZAMANI

Utamaduni wa mzanzibari kuanzia mapinduzi ya Zanzibar 1964 ulidhihirika katika vipengele mbalimbali.

3.1.1 MAVAZI

Ni sehemu muhimu ya utamaduni wa mswahili wa Zanzibar, yalikuwepo mavazi maalumu ya kike na ya kiume, Wanaume walikua wakivaa nguo tofauti na wanawake vile vile wanawake wakivaa nguo tofauti na Wanaume, Pia watu wazima wakitifautiana mavazi yao na vijana. Kwa ujumla watu wa Zanzibar baada ya mapinduzi walikua wanapenda kuvaa mavazi ya heshima kulingana na jinsia zao na utamaduni wao.

Mavazi ni muhimu katika utamaduni, Mfano:-

Vazi la kanga: Vazi la kanga lilikua ni muhimu katika kuonesha utamaduni wa Zanzibar. Kanga ilipendelewa zaidi kuvaliwa na wanawake katika shughuli tofauti na kuzivaa hasa wanapokuwa majumbani mwao na kutembelea sehemu za karibu na sio katika safari za mbali. Japokuwa Wanaume walizitumia kujifunga wakiwa nyumbani lakini haikuwa mavazi yao rasmi.

Vazi la kanzu:

Kanzu ni miongoni mwa mavazi ambayo yalitumika katika kuonesha utamaduni wa kizanzibar. Vazi hili lilikua likivaliwa na Wanaume wakati walipokua wakienda misikitini au madrasa, maeneo mbali mbali ya visiwa vya Zanzibar. Pemba na Unguja walikua wakivaa vazi hili mfano: mjini Unguja kwa upande wa Unguja na Chake chake Kwa upande wa kisiwani Pemb

Vazi la baibui

Baibui ni vazi ambalo lilikuwa likivaliwa na Wanawake tangu hapo mwanzo kabla ya mapinduzi mpaka sasa. Vazi hili lilikuwa likivaliwa na kila namna ya uvaaji wake basi lilikuwa likitoa maana yake. Lakini baibui lilikuwa likivaliwa hapo mwanzo lilikuwa likiitwa baibui la kamba(kizero) na maana hizo ni kama zifuatazo:-

a.        mwanamke akivaa baibui kawaida, hivyo inamaanisha kwamba anaenda dukani kutafuta vitu vya skukuu au vitambaa. Au anavaa baibui akiwa amefunga kamba au hajafunga kizero katupia nyuma pia hiyo maana yake anaenda dukani.

b.      Mwanamke akiwa amelivaa baibui akalishika kutoka chini mpaka kwenye mabega, kifua kikawa wazi maana yake anaenda ugomvini kugombana na mtu mengine.

c.       Ikiwa mwanamke amelivaa baibui moja kwa moja na kizero akikifunika lakini unyuzi hajaufunga maana yake huyo ni kizuka.

d.      Ikiwa kizero akikifunika usoni na akafunga na kamba maana yake huyo ni biharusi.

e.       Mwanamke akivaa baibui kifua wazi huku amelikamata maana yake huyo ni mjane.

f.       Mwanamke ikiwa amelivaa baibui na akalikamata kwa mkono basi maana ni anamgonjwa.

g.      Mwanamke ikiwa amevaa baibui, kizero amekipeleka nyuma nyuzi hajafunga na viatu mkononi maana yake anaenda mazikoni.

h.      Mwanamke ikiwa amelivaa baibui na mkoba kavaa ndani ya baibui maane yake anaenda Kwa bwana wake.

                                        

 Picha na 1.2. inaonesha baibui la kizero

 

Vazi la kofia

Ni vazi ambalo lilikuwa likivaliwa tangu mapinduzi na hata sasa bado vazi hili limekiwa likivaliwa, pia vazi hili lilikuwa lina namna mbalimbali ambazo pia zilikuwa zikitoa maana zake.kofia ambazo zilikuwa zikivaliwa hapo tangu mwazo ni kama vile; tarbushi, kofia ya kiuwa shumbulele(ilikuwa sana ikivaliwa na wavuvi).

                                                  

Vazi la kanga

Vazi hili lilikuwa sana likivaliwa na Wanawake na ilikuwa ikipendelewa sana Kwa vijana na watu wazima kulivaa vazi hilo kama sehemu mojawapo ya kujistiri.

        

       Picha .1.4. Vazi la heshima la kanga

Pia kuna mavazi mengine ambayo yalikuwa yakivaliwa na waswahili wa hapa Zanzibar tangu mapinduzi kama njiani mojawapo ya kukuza na kuuendeleza utamaduni wao. kama kikoi,shuka, kanzu na koti ,viatu vya matarawanda na viatu vya biharusi.

 

4.1 VYAKULA

Wazanzibar pia walikuwa wakitumia vyakula vyao kama kuuenzi na kuuendeleza utamaduni wao. Ambapo wanajamii wengi wamekuwa wakitumia vyakula hivyo na hupendelea sana kutumia vyakula hivyo katika kukuza utamaduni wao na kuvirithisha kizazi hadi kizazi. Vyakula hivyo ni kama vile; Manda, bobwe, mseto, kipote, tapo, muhogo, makopa, tuwale, matonge, vwevwe, kirugu (ugali wa muhogo), ndizi, uwele, mtama, ugali wa macho macho, vikuku, bokoboko (uji wa nazi wa uwanga), zarubia, mabwabwata, pia katika mbogamboga kuna mnavu, mungunye, na makunga.

                 

 

      

                    

Picha.2.0. vyakula vya alili.

5.1 VINYWAJI

Hivi pia ni vimiminika ambavyo vilikuwa vikitumiwa na watu kama sehemu ya kiburudisho chao ama kinywaji chao cha asili ambavyo hutumika katika kuuendeleza utamaduni wa kizanzibar mfano wa vinywaji hivyo ni kama vile, potelo, togwa, uji wa mtama, uji wa mapunje, uji wa uwele.

6.1 SANAA

6.1.1 Sanaa ya muziki

Sanaa ya muziki nayo ni miongoni mwa sanaa chachu ya utamaduni wa mswahili wa Zanzibar. Sanaa ya muziki ni sanaa pendwa, pia ni kitambulisho cha utamaduni wa mswahili kwani walikuwa wakitumia mambo ya asili katika muziki huo katika kuuenzi utamaduni wao. Miziki ya kipindi hicho ilikuwa ni kama taarabu asilia, dumbaki, Ngoma ya msondo na nyengine. Wanamuziki waliutangaza sana utamaduni wa mswahili wa Zanzibar kupitia nyimbo zao ndani na nje ya nchi kama vile India na ulaya, ambapo zilienea zaidi nyimbo za Bi Siti bint Saad na Bi Kidude bint Baraka, pamoja na Mzee Makame Faki. Miongoni mwa nyimbo walizoimba ni kama vile, Nifanye nini, Kijiti, Ahmada na Mpewa hapokonyeki.

 

 

 

 

 

 

 

                                Picha n.3.0. inonesha wasanii wa zamani.

Katika mwaka 1990 sanaa ya muziki ilikuwa zaidi Hadi kuchipukia kwa muziki wa zenji fleva. miongoni mwa wasanii hao na nyimbo zao ni kama vile, AT na Berry Black, wimbo ni Kama Nimekosea.

 

         

 

 

                                Picha.3.1 Msanii wa zenji fleva

 

 

 

 

6.1.2 Sanaa ya maonesho

Hii ni sanaa inayooneshwa katika kundi la watu kwa ajili ya kutoa ujumbe na kuelimisha jamii katika nyanja nyingi. Sanaa hizi ziliweza kuibua hisia za watazamaji na wasikilizaji pamoja na kuimarisha utamaduni. Sanaa hii ilihitaji upeo mkubwa wa kifikiri na kuangalia yaliyomo katika jamii za waswahili. Miongoni mwa maonesho hayo ni kama vile, maigizo, mashairi, ngonjera, Ngoma na maonesho mengine yenye kuibua hisia. Wanamichezo hao wakongwe ni kama vile, Mzee Halikuniki, Mzee sekembuke, walioogoza michezo kama vile, Kituko, Maraka tuu na Ugomvi wa mke.

    

Picha.3.2. Inaonesha wanavichekeasho wa zamani wa Zanzibar

6..1.3 Michezo

Waswahili wa zanzibar pia walikuwa wakicheza michezo mbalimbali katika kuuendeleza utamaduni na kuuendeleza hadi sasa mfano wa michezo hiyo ni kama vile; mchezo wa ng'ombe, kurumbizi, Ngoma ya msewe, kidumbaki, kuvuta kamba, mashindano ya vidau, mchezo wa kujisuka na charanga.

a. Mchezo wa kamba: ni mchezo ambao ulikuwa ni wa kushindana kuvuta kamba baina ya pande mbili ili kupimana nguvu. hususani maeneo ya pujini.

Kurumbizi/ngwale: ni mchezo wa kuangushana hususani maeneo ya pemba.

 

 

b. Kidumbaki: hizi ni ngoma ambazo zilikuwa zikipigwa katika sherehe za harusi.

Ngoma ya msewe: Ngoma hizi zilikuwa zikipigwa sana kwenye sherehe za mavuno na sherehe za siasa.

c.Charanga: ni Ngoma ambazo zilikuwa zikipigwa kwenye mikutano na hata katika mashindano ya mpira kama kusherehekea. Ngoma hii sana ilikuwa ikipigwa maeneo ya kojani

Ngoma ya umundi: ni ngoma ambayo ilikuwa ikipigwa katika sherehe za uganga hususani katika maeneo ya wingwi na kiuyu (pemba)

iii. Sherehe

Waswahili wa Zanzibar walikuwa wakifanya sherehe katika kusherehekea, kufurahi na kujumuika kwa pamoja. Mfano wa sherehe hizo ni kama vile:-

Sherehe za maulidi yaliyokuwa yakifanyika maeneo ya Tumbatu (Gomani), Pemba (kojani), Fundo na Micheweni

a. Sherehe za mavuno, hizi zilikuwa zikifanyika kila baada ya mavuno na kusherehekea mavuno yao sehemu hizo ni kama vile Makunduchi

b. Sherehe za harusi, ni sherehe zilizokuwa zikifanywa siku za harusi katika jamii zao ambapo walikuwa wakipiga Dufu, Ngoma za vibati na Kidumbaku. Watu walikuwa wakivaa mavazi yao mazuri. Kwa upande wa biharusi alikuwa akichaguliwa mume na mzee wake pia alikuwa akiwekwa ndani mwezi kabla ya harusi na kupewa mafunzo ya ndoa. Na baada ya ndoa wote mke na mume hawaruhusiwi kutoka ndani mpaka wiki ifike huku wakihudumiwa.

Mavazi ya bibi harusi wa zamani alikuwa akivaa buibui la nyuzi (kizoro) na kanga na mitarawanda. Na Kwa upande wa bwana harusi alikuwa akivaa kanzu koti na kofia au kanzu kofia na joho na viatu vya makubadhi.

c. Sherehe za mwaka kogwa; ni sherehe ambazo zilikuwa zikifanywa haswa baada ya mavuno ambapo paliandaliwa mapigano ya vigongo baina ya makundi mawili kwa ajili ya kupimana nguvu zao na pamoja na kutumia mavuno yao katika skukuu. Lakini baadae rais wa kwanza wa Zanzibar aliamrisha watu kupigana kwa kutumia makoa (magomba). Sherehe hizo zilikuwa maarufu sana Makunduchi na Kojani.

d. Sherehe za skukuu ya Iddil fitri na Iddi lhaji. Sherehe hizo zilikuwa maarufu sana Zanzibar, zilikuwa zikifanywa katika mfunguo mosi na mfunguo tatu. Siku hizo watu walikuwa wakivaa vizuri na kunywa vizuri pamoja na kutembeleana.

Skukuu ya Iddil fitri (mfunguo mosi) ilifanyika baada ya waisilamu kumaliza kufunga Ramadhani

Skukuu ya Iddil hajji (mfunguo tatu). Hii hufanyika baada ya waisilamu kumaliza kufanya hija huko Makka. Hapa waisilamu hufunga siku Tisa kama kuwakilisha waliokwenda hijja

6.5 UONGOZI NA SIASA.

Zanzibar ni moja ya maeneo muhimu sana katika historia ya Tanzania. Kuanzia mwaka 1964 hadi sasa, kumekuwa na viongozi kadhaa walioongoza Zanzibar. Hapa nitataja baadhi ya viongozi muhimu wa Zanzibar tangu mwaka 1964:

1. Shekh Abeid Amani Karume. (1964-1972) - Alikuwa Rais wa kwanza wa Zanzibar baada ya muungano wa Zanzibar na Tanganyika. Alikuwa kiongozi wa Mapinduzi ya Zanzibar ya 1964 na alikuwa rais hadi kifo chake mwaka 1972.

2.Ali Hassan Mwinyi. (1972-1984) - Alichukua madaraka baada ya kifo cha Abeid Amani Karume mwaka 1972 na akahudumu kama Rais hadi mwaka 1984.

3.Idris Abdul Wakil.(1984-1988) - Alikuwa Makamu wa Rais chini ya Ali Hassan Mwinyi, na aliteuliwa kuwa Rais wa Zanzibar baada ya Mwinyi kuhamia Tanganyika kama Rais.

4. Aboud Jumbe. (1988-1990) - Alichukua madaraka baada ya kujiuzulu kwa Idris Abdul Wakil mwaka 1988.

5. Salmin Amour. (1990-2000) - Alikuwa Rais wa Zanzibar kuanzia mwaka 1990 hadi mwaka 2000.

Baada ya mapinduzi, yaliongozwa na Mzee KARUME."1964" Zanzibar ilianza kufuata sera za kiongozi mpya, ambaye kwa muda mrefu alikuwa mstari wa mbele katika kutetea haki za Wazanzibari na kusukuma mbele malengo ya uhuru na maendeleo ya taifa.

Baada ya Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964, uchumi wa Zanzibar ulibadilika sana. Mapinduzi hayo yalikuwa ya kisiasa na kijamii na yalilenga kubadilisha mfumo wa serikali na uchumi wa Zanzibar. Baada ya mapinduzi, sera za serikali ya Zanzibar zililenga kujenga uchumi wa kijamaa na kufanya mageuzi katika mfumo wa umiliki wa mali na rasilimali za nchi.

Umiliki wa Ardhi na Viwanda; Baada ya mapinduzi, ardhi na viwanda vilivyokuwa vikitawaliwa na wakoloni na wakulima wakubwa vilinaswa na serikali au kugawiwa kwa wananchi. Hii ililenga kusambaza mali na rasilimali kwa usawa miongoni mwa wananchi. Kwa mfano makunduchi serikali ilipanga mkakati maalumu katika kukuza uzalishaji wa mazao. Wanajamii walipatiwa mbegu kuziatika na kuangalia mbegu gani imeota vizuri na kuichagua hiyo katika mwaka huo kama zao la kuotesha.

i. Uchaguzi wa Taifa. Baada ya mapinduzi wazanzibari walikuwa wanaendesha masuala ya siasa katika kuchagua kiongozi atakaewaongoza wananchi kwa utaratibu maalumu.  Ili uwempiga kura halali lazima uwe na meno kumi na nane (18). Yani (gego la mwisho liwe limeota). Serikali ilioshika madaraka iliwafanya raia kuwa na mapenzi na viongozi wake na kudhibiti machafuko kutotokezea. Hivyo, watu waliishi kwa amani na furaha na viongozi wao.

                           

                        Picha na .4.0. Picha inaonesha uchaguzi wa taifa.

 

 

 

7.1 UCHUMI WA WAZANZIBARI BAADA YA MAPINDUZI.

7.1 Biashara.

Biashara baada ya mapinduzi ilikuwa ni wachache wanaojihusisha na biashara, kwa sababu ilitangazwa rasmi kuwa kila mmoja afanye biashara anayoitaka. Ispokuwa wale waliopewa mamlaka na serikali, mfano Pemba watu walikuwa wanakwenda kupanga msongo maeneo ya wete kununua kilo ya Mchele, na inawezekana asiupate kwa siku ile. Baada ya miaka michache ikatangazwa kuwa kila mmoja afanye biashara anayoipenda mahali popote, watu wakafungua maduka ya vyakula kama vile mchele, maharage, nguo, vyombo vya baskeli za rali nakadhaalika.

Picha na 5.0. inaonesha biashara.

 

 

7.2 Kilimo

Baada ya Mapinduzi, serikali mpya ya Zanzibar ilianzisha sera ambazo zililenga kuendeleza kilimo na kuinua hali ya maisha ya wakulima. Miongoni mwa hatua zilizochukuliwa ni pamoja na:

Serikali ilichukua hatua ya kutaifisha mashamba makubwa yaliyokuwa chini ya umiliki wa wakoloni au wenyeji matajiri na kugawa ardhi hiyo kwa wakulima maskini. Hatua hii ililenga kuhakikisha usambazaji wa ardhi kwa wakulima wengi ili waweze kufaidika moja kwa moja na kilimo.

Kuwepo kwa vyama vya Ushirika.Serikali ilianzisha vyama vya ushirika ambavyo vilisaidia wakulima kuungana pamoja na kunufaika kutokana na nguvu ya pamoja. Vyama hivi vilisaidia katika usambazaji wa pembejeo za kilimo, mafunzo kuhusu mbinu bora za kilimo, pamoja na soko la mazao yao.

Kilimo cha mazao ya biashara. Kuanzia 1964 biashara ilikuwa na kusababisha waswahili kuwa na utamaduni wa kujipandia mazao ya biashara kama vile karafuu. Minazi. miembe. Wakati wa karafuu watu wakiambizana wote wenye uwezo wa kuchuma waende katika mashamba kwa ajili ya kuchuma zao hilo.

           Description: C:\Users\IBRAHIM\Pictures\image\FFFFFF.jpg

           Picha na.5.1 inaonesha mazao ya biashara yanayolimwa Zanzibar.

Shuhuli za uvuvi. Uvuvi ilikuwa ni shuhuli maarufu iliyo ikifanya na waswahili baada ya mapinduzi kwa ajili ya kupata kipato cha kujikimu kimaisha. Waswahili walikwenda baharini kutafuta samaki, pweza, chaza, kome, korong'onjo, choe, Tondo na kadhalika. Waliitumia bahari kupata kitoweo na pia kupata kipato cha pesa. Vilevile walikamata samaki kutoka katika mito na maziwa kama vile perege, kambare na aina nyengine za samaki.

7.3 MSIBA.

Misiba ya wazanzibari ilipo kuwa ikitokea, walizingatia zaidi dini zao walizo kuwa nazo na hasa dini ya kiislamu na wakiristo.

Katika msiba wa waislamu, ulipokuwa unatokea watu wakikusanyika katika eneo la tukio na kushirikiana kwa hali na mali katika kumstiri marehemu. Hutolewa watu katika kila Kona ya kijiji ili kila chochoro angalau mtu mmoja aweze kushiriki katika uchimbaji wa kaburi. Watu wa karibu walikuwa na utaratibu wa kuleta chakula ili wale na wafiwa kwa pamoja. Na walikuwa na utaratibu wa kupeana mkono wa pole pia kulala matangani siku tatu.

Pia walisoma hitima ikifika siku ya tatu na siku ya arobaini wakisoma halili.

Picha na 6.0. inaonesha misiba wa waswahili

Kwa upande wa wakiristo. Walikuwa anapokufa mtu wanakusanyika na kumuombea kuuwaga mwili na baadae kwenda kumzika akiwa ndani ya jeneza.

 

8.1 UONGOZI NA SIASA YA SASA.

Viongozi waliongoza kuanzia 2000 hadi 2024 nikama wafuatao:

1.Amani Abeid Karume. (2000-2010) - Alikuwa rais wa Zanzibar kuanzia mwaka 2000 hadi mwaka 2010.

2. Ali Mohamed Shein. (2010-2020) - Alikuwa rais wa Zanzibar kuanzia mwaka 2010 hadi mwaka 2020.

3. Hussein Mwinyi. (2020-hadi sasa) - Alichaguliwa kuwa rais wa Zanzibar.

Siasa za sasa zimekuwa za kiuhasama, kiuadui na kujengeana chuki baina ya watu. Hii ni kutokana na kuwa viongozi wanaochaguliwa hawana huruma na wafuasi wao, hujali kitu kuliko utu. Huwajaza Imani wafuasi wao na matokezeo yake watu huanza kupigana, kudhulumiana, kutosalimiana, kutohudhuria katika misiba ya kundi au watu wengine na hata kupoteza uhai wa wengine. Utamaduni huu ulianza kukua kuanzia" 2000" Hadi sasa.

Mikutano

Siasa za sasa hufanyika kwa ushindano mkubwa baina ya vyama tofauti. Kila kundi linajiona limekamilika kutokana na muamko wa watu wanaohudhuria katika mikutano mbalimbali ya kisiasa. Watu hupiga ngoma na matarumbeta pia husoma utenzi unaowapa moyo wafuasi, na kiongozi hupanda jukwaani na kuhutubia hadhira iliomzunguka.

Uchaguzi mkuu.

Siku ya uchaguzi Wazanzibar hujitokeza kwa wingi katika vituo vilivyopangwa kwa ajili ya kupiga kura. Siku ya kura kila mmoja huacha kila kitu ilimradi afike katika maeneo ya kupiga kura na kutekeleza zoezi hilo. Utamaduni uliopo nikwamba , mpiga kura atakaefika mapema huanzisha foleni bila kuzingatia vyeo vyao, vyama vyao , rangi zao , masikini wala tajiri ispokuwa wote siku hiyo wanakuwa sawa , wala huwezi kumbagua mtu kutokana na mavazi aliovaa ispokuwa viongozi katika chama fulani.

Picha na 6.1. inaonesha mahojiano juu ya chaguzi za kisiasa

8.2  MILA.

Katika utamaduni wa mswahili wa Zanzibar pia waswahili hawa walikuwa na mila zao ambazo walikuwa wakizifuata kutoka kwa mabibi na mababu zao. Mila hizo walikuwa wakiziendeleza kwa kuzitekeleza kama zinavyotakiwa..Mila hizo zilikuwa zikifanywa ima kwa siku kadhaa katika mwaka na ni lazima zitekelezwe katika jamii husika.mfano wa mila hizo ni sherehe za mwaka kogwa ( kutoka katika jamii ya makunduchi) , sherehe ya kuoga mwaka (kutoka katika jamii ya pemba- kojani).

Description: C:\Users\RM\Pictures\babu na bibi.jpeg

Picha n.6.2 inaonesha mila za waswahili katika eneo la makunduchi

 

8.3 ITIKADI

Hii hufungamana sana na Imani ambapo wanajamii huamini katika jambo fulani kwa kuomba shida na matatizo yao ili yaweze kutatulika. Katika itikadi hizo waswahili wa zanzibar walikuwa wakiomba katika mizimu ya mababu na mabibi zao, kuomba katika mapango na hata katika miti mikubwa. lakini ingawa dini ilikuwa imeshaingia nchini lakini walikuwa wakiabudu kwa misingi ya dini hizo na itikadi zao zilikuwa zikifuatwa vilevile pasi na kuharibu au kuathiri utamaduni wao. Vilevile kutokana na itikadi hizo nyengine zilikuwa zikiwekwa mipaka na kuwa jinsia hii itafanya na nyengine isifanye juu ya kile wanachokiamini. Waswahili hawa huamini sana katika masuala haya hata kama wakawa na mgonjwa au ugomvi katika familia zao basi hufuata itikadi zao. mfano wa itikadi hizo ni;

wanawake pekee kuruhusiwa kuoga mwaka kogwa pasi na kuonekana ama kushiriki na mwanaume yeyote na ikitokea mwanaume ataenda kuwaona wanawake hao basi atahukumiwa kesi juu yake.

Wanawake wajawazito kutoruhusiwa kula yai kwa kuhofia kuharibu ujauzito au kumuathiri mtoto wake. Mwanamke alie katika ada yake haruhusiwi kuchuma mboga kwa kuamini kuwa ikiwa atachuma mboga hizo basi zote hufa.

Kiti au kibanda kilichojengwa Kwa ajili ya kiongozi au mkubwa wa kijiji basi katika sherehe zao za kiitikadi ilikuwa haruhusiwi yeyote kukitumia kifaa hicho hata kama mwenyewe hayupo .ila katika siku za kawaida basi huruhusiwa kutumia bila hata ya idhini ya mwenyewe na ikitokezea mtu katika sherehe zao akatumia vifaa hivyo pasi na mwenyewe basi vilikuwa vikimdhuru.

Description: C:\Users\RM\AppData\Local\Microsoft\Windows\INetCache\Content.Word\Screenshot_20240504-140709_1.png

                       Picha na.6.3. inaonesha herehe za mwakakogwa

8.4 JADI ILIVYOKUWA INATUMIKA BAADA TU YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR 1964

Jadi ni miongoni mwa mila, maarifa pamoja na imani ambayo hurithishwa kutoka kizazi hadi kizazi na ni sehemu ya utamaduni wa jamii ya wanaadamu. Jadi huhusisha urithi wa kitamaduni unaotambulisha jamii fulani na kuendeleza utambulisho wake kwa njia ya shughuli, fikra na maadili yaliyomo katika utamaduni huo. Kwa kiasi fulani jadi ilivyokuwa ikitumika kabla ya mapinduzi ya Zanzibar na baada ya mapinduzi mnamo miaka ya 1964 imegawika katika vipengele.

I.Ngoma za jadi:

Ngoma za jadi zilizokuwa zinatumika tangu enzi na enzi na mara tu baada ya mapinduzi ya Zanzibar ni kama vile Ngoma ya Pungwa ambayo katika visiwa vya Zanzibar inafanyika Bumbwini Unguja na kwa upande wa Pemba ngoma hii hujuilikana kama Umundi, pia ngoma ya Rubamba ambayo hujumuisha mavazi meusi, Ngoma ya Somali au Ruhani, ngoma ya kibuki ambayo asili yake ni Komoro. Ngoma hizi zimekuwa zikitumika sana tu katika kipindi cha miaka ya nyuma na zilikuwa zikitiliwa maanani sana.

II.Vyakula vya jadi

 Jadi ina muingiliano mkubwa na mila ambayo imehusisha vyakula mbali mbali vya kijadi. Vyakula vya kijadi ni vyakula vya asili lakini si kila vyakula vyote vya asili vinaweza kuingizwa katika jadi. Mfano wa vyakula vya kijadi ni Bumbwi, Manda, Makopa yanayotengezwa kwa Muhogo, Nyama ya kuchoma na venginevyo. Kimsingi vyakula hivi ndivyo vinavyotumika katika jadi na vilikuwa vikipewa kipaombele sana katika ulaji wao. Vyakula hivyo vya jadi vinatumika kuliwa katika sherehe za kijadi vilevile hutumika kupikiwa mashetani pamoja na mizimu ili watu kuweza kuendeleza jadi yao ambayo walirithi kutoka kwa mababu zao na mabibi zao na ndiyo maana ya kuwa jadi hurithishwa kizazi hadi kizazi.

III.Matibabu ya jadi

Katika upande wa matibabu ya kijadi hapo miaka ya nyuma kidogo baada ya mapinduzi ya Zanzibar miaka ya 1964 watu walikuwa wakitumia sana dawa za mitishamba yaani dawa za asili pamoja na kujitibu kupitia njia za kuomba mashetani. Matibabu haya yalikuwa na utaratibu maalumu, Kwa upande wa matibabu ya kutumia dawa za asili yaani mitishamba watu walikuwa wakiingia maporini na kujikatia miti inayofaa kwa kutibu maradhi yao. Kwa upande wa matibabu kupitia njia za mashetani watu huenda kwa mafundi (waganga wa kienyeji) ambao wao hutumia mashetani katika kutibu watu na wagonjwa huambiwa wapeleke aidha kuku wa aina pamoja na rangi fulani, Ng'ombe, Mbuzi, Kondoo pamoja na masharti mengine ili kuweza kupona maradhi waliokuwa nayo. Pia kwa upande wa familia inakuwa na jadi yao ambayo wamerithi kutoka kwa wazazi wao, kwahiyo mtu anapoumwa katika familia kiongoz ambae ameibeba jadi ya familia hiyo ndiyo hutoa dawa. Na ikiwa familia hiyo kila mtu ana matatizo basi hupewa kipaombele sana jadi kwa kuamua kuchicha mnyama yoyote ili familia hiyo iweze kuepukwa na mikosi pamoja na nuksi. Matibabu mengine ya kijadi ni kuomba kwenye mizimu au mashetani kwa ajili ya kutafuta tiba. Watu huenda sehemu za mapango, kwenye mijiti mikubwa na sehemu maalumu zilizotengenezwa kwa ajili ya kuomba mizimu pamoja na mashetani ili kuweza kupata tiba. Zifuatazo ni picha zinazoonesha sehemu ambazo watu huenda kuomba ili kupata tiba na kutatuliwa matatizo yao waliokuwa nayo.

      Description: C:\Users\RM\AppData\Local\Microsoft\Windows\INetCache\Content.Word\20240504_233809.jpegDescription: C:\Users\RM\AppData\Local\Microsoft\Windows\INetCache\Content.Word\20240504_233804.jpeg                                                                   

Picha.na 7.2 inayonesha jadi za waswahili.

   

Picha na.6.4 inaonesha wanafunzi wakifanya mahojiano na Mzee Mwita wa Makunduchi katika eneo la mwaka kogwa.

8.5 MAADILI YA KALE

Maadili ni tabia ya mtu, watu au jamii Fulani. maadili hayo yanaweza kuwa mabaya au mazuri. Baada ya uhuru yalikuwa katika hali nzuri na ya kuridhisha kutokana na kushirikiana kwa wazee katika kulea watoto waona kuwarithisha tabia njema ili kuwalindia utu na heshima za wazazi wao, watoto walikuwa na adabu kwa wakubwa na wadogo zao, wakifuata mila na itikadi zao kwa kufuatiwa na msemo usemao usiache mbachao kwa msala upitao. Kwa wakati huon watoto walifundishwa mambo mengi kama kupata elimu, kujilinda na vishawishi jambo ambalo limepelekea kutokuwepo kwa ukatili, ubakaji, na udhalilishaji kwa vile jamii ilileana katika maadili mema mpaka kufikia kipindi cha (1999). maadili yalipewa kipao mbele sana kwasababu kila mzazi alikuwa hayupo tayari kumuona mtoto wake anapoteza na anaenda kinyume na maadili ya utamaduni wa mswahili. Hivyo ikapelekea wazazi kujifunga kibwebwe kuepukana na kwenda kinyume na na maadili kwasababu waliamini kwamba maadili ndio kitu muhimu kwa mwanadamu katika harakati tofauti tofauti za kijamii na kimaisha. Endapo mtu atakosa maadili alionekana kuwa haifai kuigwa katika jamii hiyo. Mifano ya maadili ni kama vile watoto kuwasaidia wazee wanapokuwa na mizigo, kuongea kauli nzuri unapoongea na watu wazima, kuwasalimia kwa kutumia utamaduni wa mswahili, kuwa na mavazi yenye heshima na stara nakadhalika.

Vilevile maadili yaliongozwa na wanajamii wote na ikafikia hatua kwamba mzazi yoyote anauwezo wa kumkanya na kumpa maadili mema mtoto wa mzazi mwenzake. Na waliamini msemo wa wahenga waliosema " Samaki akioza mmoja huoza wote" hivyo kutokana na msemo huo waliondoa tofauti zao kama wazazi na waliona mtoto mmoja ni wa wanajamii mzima kwahio walikuwa hawako tayari kuona mtoto mmoja katika jamii yao anaenda kinyume na maadili yao.

Pia waliamini kwamba "umoja ni nguvu utengano ni udhaifu" jambo hilo liliwapelekea kuwa kitu kimoja na endapo mmoja miongoni mwao katika jamii atapata matatizo wanaona kwamba tatizo hilo ni lao wote hivyo watashirikiana kwa hali na mali kutafuta njia mbadala wa kulitatua tatizo hilo kwa pamoja na kuendeleza maadili yao.

Vilevile waliamini kwamba maadili yanaleta faida katika jamii miongoni mwa faida hizo ni kama zifuatazo:

a) Kuwepo kwa umoja na mashirikiano miongoni mwa wanajamii:  Hii ina maana kwamba wanajamii wanapokuwa wameshikilia maadili yao fulani kutapelekea umoja na mashirikiano katika harakati zao za maisha. Kwa mfano wakulima hupeana mijima ya kusaidiana kulima kwa pamoja pindi wanapomuona mwenziwao akiwa katika harakati hizo hivyo huungana kwa pamoja kulitekeleza jambo hilo.

b) Huzidisha mapenzi kwa wanajamii: Hali hii hutokea pindi endapo wanajamii katika jamii fulani wanapoishi kwa kuzingatia maadili yao hivyo hupelekea mapenzi na kuoneana huruma baina yao kutokana na maadili yao ambayo wanayatumilia katika shughuli zao za Kila siku.

c) Huondosha migogoro katika jamii:  Hii ni kwamba endapo jamii itaamua kuwa na maadili fulani mazuri husaidia kwa kiwango kikubwa kuondosha migogoro katika jamii hiyo kwa sababu wanajamii wote wanafuata maadili ambayo yamewekwa na wanajamii wote katika jamii hizo.

                 Description: C:\Users\RM\AppData\Local\Microsoft\Windows\INetCache\Content.Word\IMG-20240504-WA0018_010510.jpg

Picha.na 7.0 inaonesha maadili ya watoto wa zamani.

Vile zamani ilikuwa kuna maadili ambayo bibi au babu wanakaa na wajukuu zao na kuanza kuwatolea hadithi katika usiku wa mbalamwezi mfano:

 

Description: C:\Users\RM\AppData\Local\Microsoft\Windows\INetCache\Content.Word\IMG-20240504-WA0017_010505.jpg

 

 

 

 

 

 

Picha.na7.1 inaonesha wazazi walivyo wakiwahadithia watoto wao.

  Maadili ni kitu kizuri katika maisha ya mwanadamu katika jamii kwasababu husaidia wanajamii kuishi na maadili mema na mchakato mzuri katika maisha.

10.1 ELIMU

Hiki ni kipengele muhimu sana ambacho watu walikuwa wakipata ujuzi na maarifa hapo mwanzo waswahili wengi wa Zanzibar walikuwa wakipatiwa elimu katika mfumo wa usemaji na utendaji jambo ambalo limepelekea watu kuwa na weledi zaidi katika taaluma hizo, lakini waswahili hao walikuwa wakipatiwa elimu kutokana na dini na jamii inavyowazunguka mpaka tulivyotawaliwa na wakoloni ndipo elimu yetu ikaanza kubadilika na kuwa na mfumo wa usemaji hadi tulipopata mapinduzi ukaendelea kutumika mfumo huo huo.

Vilevile elimu ya hapo mwanzo ilikuwa tofauti sana na hii ya sasa katika maeneo na mbinu za kujifunzia mfano; vifaa au zana zilikuwa ni dhaifu, maeneo ya kujifunzia nk.  Hapo mwanzo wanafunzi wengi walikuwa wakijifunza chini ya miti.

 

 

 

Description: C:\Users\RM\AppData\Local\Microsoft\Windows\INetCache\Content.Word\IMG-20240505-WA0007.jpg Description: C:\Users\RM\AppData\Local\Microsoft\Windows\INetCache\Content.Word\IMG-20240505-WA0006.jpg

Picha.8.0.inaonesha elimu ilivyo ikisomeshwa.

10. 2 UTAMADUNI WA WASWAHILI WA ZANZIBAR KUANZIA 2000 HADI SASA

Kuanzia mwaka 2000 hadi kuendelea hivi sasa utamaduni wa mswahili umeweza kupokea mabadiliko katika kila kiepengele cha utamaduni wa mzanzibar. Na mabadiliko hayo ni kama vinavyoelezwa:-

11.1 UTAMADUNI WA SANAA

Utamaduni wa sanaa wa kipindi cha Mheshimiwa Rais Amani Abeid Karume (2000) hadi sasa umezidi kuimarika bali pia kubadilika kutokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia pamoja na muingiliano wa watu na mabadiliko ya tabia ya nchi. Hivi sasa sanaa imezidi kukua na kuendelea kuchangia maendeleo hapa Zanzibar.

i.Sanaa ya muziki ya sasa.

Katika kipindi hiki sanaa ya muziki wa Zanzibar ni tofauti kabisa na wa kale kutokana na maendeleo ya sayansi na Teknolojia. Hivyo muziki wa sasa ni mkubwa na umejigawa. Miziki hiyo ni zenji fleva na zile za taarabu asilia ( rusha roho) beni na mengine. Kwa sasa taarabu ndiyo pekee ambayo bado inaonesha utamaduni wa Zanzibar kwa kiwango cha juu ukilinganisha na hii ya fleva ambayo kiuhalisia imebadilika haswa kimavazi, chakula, na hata lugha inyotumika. Ambapo jambo hili linapelekea kuharibu na kudumaza utamaduni wa mswahili wa Zanzibar.pamoja na kuibua migogoro mingi yenye kuhatarisha na kupelekea mifarakano baina ya wanajamii.

Miongoni mwa wasanii hao ni kama vile Dogo fany mwenye wimbo wa Naumwa.

Tamaduni huo wa sanaa katika kipindi hiki unajionesha wazi kama vile ifuatavyo:-

Picha.8.1. ikimuonesha msanii Dogo fany: wimbo' Naumwa'             

ii. Sanaa ya maonesho

Kwa sasa sanaa hii imekuwa sana. Sanaa hii imebadilika sana na zamani na hata ubunifu wake umekuwa ni mkubwa na wenye mawanda mapana. Sanaa hizi zinafanywa maeneo mengi sana kwa sasa. Pia wapo wanaoendeleza na kukuza utamaduni kutokana na kuonesha ama kiwasilishabyale mambo yanayofanywa juu ya utamaduni wetu. pia wanaudumaza kutokana na maonesho ya tasnia zao zisizozingatia utamaduni wa waswahili kama vile; lugha, Mila, mavazi wala vyakula vya kiutamaduni.

 

 

Picha.n.8.2 ikionesha Sanaa ya muziki.

iii.Sanaa ya ususi

Katika sanaa hii watu wa Zanzibar husuka nywele na vitu mbali mbali kwa umaridadi ambapo vitu hivyo vikiwa na asili ya utamaduni wa mswahili hapa Zanzibar. Miongoni mwa misusi hiyo kwa upande wa wanawake ni kama misuko ya nywele ya mitindo tofauti kama vile boga (rocket), jicho la mkwe mwenza, usinionee wivu, ambapo misuko hii ilikuwa ikisukwa kwa muundo wa mbinjuo ama mnyoosho. Pia katika utamaduni wa ususi umeelekea kubadilika kwa watu kuanza kuweka madawa kichwani, kusuka rasta na pia kukata mikato kwa wanawake hao wa Kiswahili. Na kwa namna hiyo hata watoto wa kiumbe hivi sasa wameonekana wakisukana mikato yao ya ajabu kama kiduku. Jambo ambalo linapelekea kuharibu na kupoteza utamaduni wa kwetu na kuendeleza utamaduni wa wageni.

Pia kwa upande wa sanaa ya ususi wa vitu umeweza kukua na kuendelea na kuchangia kiasi fulani kibiashara kutokana na bidhaa hizo zenye asili na utamaduni wa Zanzibar. Baadhi ya bidhaa hizo ni kama vile vipepeo vya makuti na ukindu, mokoba ya ukili, makuti ya kujengea ingawa yamepungua kwa sasa kimatumizi, usukaji wa matenga, madema na masusu ya kubebea vitu. Vitu hivi watu husuka kwa mitindo mbali mbali ili kupendezesha na kuvutia wateja wake. Ingawa pia watu wanaojishugulisha na sanaa hii si wengi kutokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia ambayo inawaletea vitu mithili ya hivi kutoka nje.

iv.Sanaa ya ushoni

Katika utamaduni wa sanaa ya ushoni bado inaendelea kuonesha utamaduni wa mswahili kwa kushona mishono tofauti ya kiasili kama vile dira, suti, vitenge, shati, baibui na shungi ( abaya kwa sasa), mshazari, sketi na panjabi. Lakini pia wakati huu mishono hio umeweza kubadilika sana. Wengi wao kwa sasa wanashona mishono kwa kuiga mitindo ya watu wa nje yautamaduni wao jambo linalopelekea vizazi hivi vya sasa kuvaa nguo zisizostara. Mfano wa mishono hiyo ni kama vile sketi fupi suruali za kubana (pedo), kitentemente, madira ya mpasuo, Modo, Nguva na mengineyo.

Description: C:\Users\RM\AppData\Local\Microsoft\Windows\INetCache\Content.Word\Screenshot_20240504-123521.pngDescription: C:\Users\RM\AppData\Local\Microsoft\Windows\INetCache\Content.Word\Screenshot_20240504-122514_1.png

     Picha.n.8.3. ikionesha Sanaa ya ushonaji.

v. Sanaa ya uchongaji

Sanaa hii nayo imeweza kukua kwa ustadi mkubwa na wenye faida kwa wakati huu kuliko zamani. Michongo ya kisasa inavutia sana na inafanya kuvutia wateja kutokana na mapambo wanayoweka katika vitu hivyo. Kwa kipindi hiki seremala wengi huchonga michongo mikubwa na mizuri mno, Vitu hivyo vinavochongwa sana kwa wakati huu ni kama vile milango, kabati, meza na vitu, vyetezo, henga za viatu na mapazia, dressing table, shokesti, vitanda, stuli na vibao vya mikate na vya kukalia. Vitu hivyo ni bidhaa nzuri na pia  hutokana na asili ya utamaduni wa mswahili pia ni vyenye kuendana na wakati tulionao.

Description: C:\Users\RM\AppData\Local\Microsoft\Windows\INetCache\Content.Word\Screenshot_20240504-124240_1.pngDescription: C:\Users\RM\Pictures\vitanda.png

 

 

 

 

 

 Picha n.8.4. uchongoji wa samani.             

vi. Sanaa ya uchoraji

Sanaa hii ya uchoraji imepamba moto kwa sasa na kuwapa vijana ajira kwa kuchora michoro mbali mbali na Kuingiza kipato katika kazi hizo, watu hao hujishughulisha na kuchora michoro tofauti kwa maandishi na picha. Huchora katika maduka nguo hasa shati za skuli na mpirani na hata shati za sherehe za serikalini, pia huchora katika mahoteli na mikoba.

Pia kuna uchoraji wa piko ambao huchorwa watu wenye shughuli, maharusi na watoto katika kusherehekea skukuu za iddi. Ambapo michoro hio ni tofauti na michoro ya zamani. Pià katika zama hizi watu huchora tatuu katika mwili ambapo tatuu hizo hukaa kwa muda mrefu au hata maisha yote katika ngozi bila kufutika ambapo suala hili ni tofauti na utamaduni wa Zanzibar.

Description: C:\Users\RM\AppData\Local\Microsoft\Windows\INetCache\Content.Word\IMG-20240504-WA0066.jpg       Description: C:\Users\RM\AppData\Local\Microsoft\Windows\INetCache\Content.Word\IMG-20240505-WA0028.jpg

                  Picha.n.8.5 mikoba iliyochorwa picha

 

vii.Sanaa ya ufundi

Katika sanaa ya ufundi watu hutengeneza vitu vingi sana vikiwemo ufundi wa umeme, ufundi wa simu, majiko ya umeme. taa na mafeni, ufundi wa vyombo vya usafiri pamoja na ujenzi.

Description: C:\Users\RM\AppData\Local\Microsoft\Windows\INetCache\Content.Word\IMG-20240504-WA0068.jpg  Description: C:\Users\RM\AppData\Local\Microsoft\Windows\INetCache\Content.Word\IMG-20240504-WA0069.jpg  

                               Picha.8.6. inaonesha ufundi seremala                                                                                                                  

viii. Sanaa ya upambaji

Upambaji ni nyenzo ya sanaa inayofanywa na jamii ya watu wa Zanzibar. Upambaji hufanyika katika kupambamaharusi, kupamba nyumba, maholi na masteji katika shughuli. Upambaji wa kipindi hiki ni tofauti na upambaji wa miaka ya nyuma (1964-1999). Hivi sasa upambaji umetanuka sana kutokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia, ambapo hata dhana hizo za kupambia zimebadilika.

Description: C:\Users\RM\AppData\Local\Microsoft\Windows\INetCache\Content.Word\Screenshot_20240504-124000_2.png         Description: C:\Users\RM\AppData\Local\Microsoft\Windows\INetCache\Content.Word\Screenshot_20240504-123810_2.png

                                 Picha.n.9.0.inonesha mapambo ya harusi.

 

 

ix.Sanaa ya ufinyanzi

Ni sanaa ambayo hutengeneza vitu kwa kutumia udongo. Sanaa hii hadi leo bado inafanyika hasa katika vijiji kama Muyuni na Muungoni. Watu hao hutengeneza vitu kama vile mikungu, vyetezo, mitungi, vyungu na hata majiko ya mkaa yenye asili ya vyombo vya uswahilini. Ingawa kutokana na sayansi na teknolojia sanaa hii imepungua kutokana na kuwepo kwa uingiaji wa vyombo vya bati, kaure na vya kisasa.

Description: C:\Users\RM\AppData\Local\Microsoft\Windows\INetCache\Content.Word\Screenshot_20240504-123011_2.pngDescription: C:\Users\RM\Pictures\ufinyz.png

                         Picha.n.9.1. vyombo vya ufinyanzi.

x. Sanaa ya udarizi

Pia katika kipindi hiki utamaduni wa mswahili wa Zanzibar umeweza kuimarika kupitia udarizi wa vitu na mitindo tofauti ambayo watu wakiibuni. Miongoni mwa udarizi huo ni mashuka, mapazia, kanzu, kofia na mazulia.

Description: C:\Users\RM\Pictures\shuka.pngDescription: C:\Users\RM\AppData\Local\Microsoft\Windows\INetCache\Content.Word\Screenshot_20240504-122514_1.png 

Picha.9.2. inaonesha udarizi mashuka

12.1 MAVAZI YA SASA

Mavazi ni miongoni mwa stara ambazo waswahili wa sasa wanayatumilia kuvaa kwa lengo la kujistiri milli yao. Mavazi hayo ni jambo la kawaida sana kumkuta mwanamke na mwanamme wa zama hizi kuvaa ukilinganisha zama zilizopita kwasababu mavazi hayo yanatofautiana sana katika mionekano yao namna inavyoonekana.  Japo kuwa mavazi ya sasa ni yenye gharama sana lakini wanajamii wanayatafuta kwa hali na mali ili kuyavaa katika harakati zao za kila siku. Hivyo na kupelekea mavazi hayo kubadilika mionekano yake siku hadi siku zinavyoenda katika ulimwengu.

 Pia mavazi hayo kubadilika kulingana na wakati namna unavyokwenda na humpa taswira mtu tofauti pindi anapoyavaa.  Kwasababu kila vazi linapovaliwa linaleta taswira yake na umuhimu wake katika jambo fulani inaweza kuwa vazi hilo mtu akivaa ikawa naenda harusini, mazikoni hospitalini, mashuleni, kondeni, kazini na kadhalika kulingana na mtu vazi alilovaa hivyo humtambulisha namna kitu anachokifanya.

Vilevile mavazi ni moja ya njia wapo ambayo humtambulisha mtu sehemu anayotoka kwasababu ya tofauti ya mavazi hayo. Kuna aina mbali mbali za mavazi katika ulimwengu mavazi hayo ni kama vile mavazi ya kihindi, mavazi ya kiarabu kama vile kanzu na kofia , mavazi ya kichina , mavazi ya kizungu ambao mara nyingi huvaa suruali na flana katika harakati zao mbali mbali za kila siku pia kuna mavazi ambayo wanavaa waswahili ambayo yameletwa na wageni mbalimbali ambao walikuja kitawala katika upwa wa Afrika Mashariki ambapo walipoondoka wakatuachia mavazi hayo ambayo waswahili wa sasa wanayatumilia kuvaa katika shuguli zao mbali mbali kama vile makazini , mashuleni , maharusini , mikutanoni katika mambo ya kisiasa , misikitini ambapo mavazi yake ni kanzu na kofia ambazo zimeletwa na waarabu walipokuja katika upwa wa Afrika Mashariki na mavazi hayo huvaliwa kwaajili ya kuabudu na kujifunza elimu na pia hutumika katika shughuli za kindoa kwa waisalamu na sherehe kama za kusherehekea Eid elfitr ambapo waislamu takribani wote huvaa wakubwa kwa wadogo kwaajili ya sherehe hizo.

Kwa upande wa wakristo wao hupendelea kuvaa vazi la suti ambalo limeletwa na Waengereza wakati walipokuja kutawala katika mwambao wa Afrika Mashariki ambapo vazi hilo hutumika katika shughuli zao za kindoa na sherehe mbali mbali kama vile krismasi , siku za kwenda kuabudu na kadhalika.

.   

Picha.n.9.3.inaonesha mavazi ya sasa.

Huu ni mfano mmoja wapo ambao wanajamii wa wakati huu wanavaa katika harakati zao za kila siku kabla ya hapo zamani kulikuwa hakuna mavazi haya ispokuwa walikuwa wanavaa makaniki pamoja na mabaibui ya nyuzi katika shughuli zao tofauti.

    

       Picha.n.9.4.inaonesha baibui la sasa.

Kutokana utandawazi ulioingia ulimwenguni umepelekea watu sasa hivi kutokuvaa mabaibui yao kiasili ya kiutamaduni waswahili na kuvaa mabaibui ambayo yameletwa na wageni mbalibali kama vile waarabu, wazungu na hata wachina.

 Pia mavazi ya sasa yako mengi sana ukilinganisha na ya zamani ambayo yapo ya kitoto na ya kijitukizima mbali mbali kama vile:

Mfano wa mavazi wanayovaa wanaume wakati wa sherehe kama vile harusi au sherehe za Eid ni kama yafuatayo:

   

   Picha.n.9.5.mavazi ya ulimwengu mpya.              

Pia Kuna mavazi tofauti tofauti ambayo sasa yanavaliwa lakini zamani ilikuwa hayapo kutokana utandawazi ulioingia ulimwenguni umepelekea watu sasa wanayatumilia kuvaa kwa ajili ya malengo yao tofauti tofauti ambayo huvaliwa na wanawake wanapokwenda maharusini, makazini, maofisini nakadhalika mfano wa mavazi hayo ni kama yafuatayo:

 

 

 

 

 

 

 

      Picha.n.9.6.mavazi ya kizazi kipya.

Pia kuna mavazi ya kisasa mbayo huvaliwa na watoto katika harakati tofauti tofauti za kijamii lakini zamani ilikuwa mavazi hayo hayatumiki. Mfano wa mavazi hayo ni kama yafuatayo,   

     

         Picha.n.9.7. inaonesha mishono ya sasa.                

 Vile vile watoto wa kiume wa sasa yapo mavazi ambayo wanayatumilia kuvaa lakini zamani pia yalikuwa hayatumiki. Mfano wa mavazi hayo ni kama yafuatayo;

           

               

     Picha.n.9.8.inaonesha mavazi ya kizazi cha sasa.

 Kutokana utandawazi uliyongia ulimwenguni sasa umepelekea wanajamii kuyaacha mavazi yao ya kiasili na kufuata utamaduni wa kigeni na kuacha mavazi ya tamaduni zao za kiswahili ambapo japo kuwa mavazi kuonekana kuwa na ubora zaidi kuliko na ya kale lakini mavazi hayo ni ya gharama zaidi ukilinganisha na ya zamani ambayo ndio ya kiasili zaidi.

 Hivyo mavazi pia yamepelekea kudumaza kwa kiwango kikubwa utamaduni wa mswahili baada ya kuja utandawazi ambao umedhoofisha utamaduni wa mswahili hivyo hatuna budi kuyaenzi mavazi ya zamani ili kuudimisha utamaduni wetu wa mswahili vijijini na hata mijini

12.2 ELIMU

Elimu ni ujuzi fulani ambao mtu hupata ujuzi huo kwa kusomea au kujifundishia. Utamaduni wa kupata elimu umekua ukitofautiana kwa kiasi kikubwa ukilinganisha na miaka ya nyuma iliopita. Elimu kwa sasa imekua ikitolewa kwa njia moja tu ukilinganisha na utamaduni wa zamani ambao ulikua ukitolewa kwa njia tofauti; mfano wa njia zilizozikitumika zamani ilikua ni njia ilio rasmi na njia iliokua sio rasmi. Njia iliokua sio rasmi watoto walikua wakikusanywa kwa ajili ya kupewa elimu kwa vikundi kama vile elimu ya kijinsia, mila, utamaduni nakadhalika.

Njia ilyokua rasmi. Hii ni njia ambayo watoto walikuwa wakipelekwa mashuleni kwa ajili ya kupatiwa elimu itakayoenda kuwakomboa katika maisha yao ya kila siku. Idadi ndogo sana ya wanafunzi ilonekana katika mashule hii ni kutokana na kukosa hadhi kwa wakati huo kulingana na utamaduni wao.

Kwa sasa utamaduni wa kupatiwa elimu umekuwa ukitumia njia moja tu ambayo ni njia rasmi. Utamduni wa kupata elimu kwa sasa umekuwa suala la msingi kwa sasa ambapo watoto huanzia ngazi ya maandalizi mpaka kufika kidato cha nne kama ni elimu ya lazima kwa zanzibar. Vile vile ongezeko la wanafunzi limekua kwa sasa ukilinganisha na miaka iliopita nyuma; hii ni kutokana kwa kuonekana elimu ni kitu muhimu katika maisha ya kila siku. Pia katika elimu ya Zanzibar somo la kiswahili limekua kama ni somo moja wapo ambalo ni la lazima katika masomo yake ili kuendeleza na kukuza utamaduni wa Kiswahili.

Pia uboreshaji wa miundo mbinu ya kielimu imekua kwa kiasi kikubwa kulinga na idadi ya wanafunzi maskulni, skuli tofauti kubwa za ghorofa kama ni maskuli ya kisasa kumekuwa na ongezeko kubwa la madarasa ya kujifunzia, vikalio, madaftari ya kujisomea, n.k

Pia idadi ya vyuo vikuu vimeongezeka kutoka idadi chache na kufikia idadi kubwa ya vyuo hivo , jambo hili la kuenda vyuo vikuu limefika idadi kubwa ya wanafunzi ambao wanajiunga na vyuo hivyo kama ni utamaduni wao wa zanzibar. Vile vile idadi ya wafundishaji katika sehemu za kutolea elimu ukilinganisha na hapo awali. Ubora wa elimu uinayopatika kwa sasa imekua na hadhi kubwa na kuzalisha watu walio bora na ufanisi mkubwa wa kazi.                             

Mfano wa wanafunzi wa sasa wanavopata elimu wakiwa katika maeneo ya kujifunzia.

 Description: C:\Users\RM\AppData\Local\Microsoft\Windows\INetCache\Content.Word\IMG-20240504-WA0022.jpgDescription: C:\Users\RM\AppData\Local\Microsoft\Windows\INetCache\Content.Word\IMG-20240505-WA0009.jpg

Description: C:\Users\RM\AppData\Local\Microsoft\Windows\INetCache\Content.Word\IMG-20240505-WA0004.jpg Description: C:\Users\RM\AppData\Local\Microsoft\Windows\INetCache\Content.Word\IMG-20240505-WA0003.jpg

Picha.1.0. inaonesha elimu ya sasa.

 13.1 MILA NA ITIKADI ZA SASA.

Waswahili wengi wa Zanzibar wamekuwa ni wenye kuzitupa mkono mila na desturi zao walizokuwa nazo jambo ambalo limepelekea kuharibu utamaduni wao. Mfano kuoga mwaka katika jamii nyingi za wazanzibari mila hii wameziacha kabisa na kutokutekelezwa haswa na kupelekea kudhorota kwa tamaduni zetu.

Vilevile kutokana na Zanzibari kuendelea kukua na kuongezeka kwa idadi ya watu wake basi waswahili wa zanzibar wamekuwa si wenye kuzifuata tena itikadi zao na zengine kupotea kabisa. Ingawa kabla na tangu mapinduzi waswahili wa zanzibar walikuwa ni wenye kufuata itikadi za jamii zao pamoja na zile za dini ya kiislamu na kikristo lakini kila miaka inavyozidi kwenda ndipo mambo hubadilika na kwenda na wakati huo.

Tangu Karne ya 20 mpaka sasa waswahili wa zanzibar wameziacha itikadi zao walizorithi kutoka kwa mababu zao na wengine ndio haswa imani za kidini pia kuzipuuzia. Na sasa wengine wao wamekuwa ni wenye kuishi kulingana na mfumo wa utandawazi na maendeleo ya sayansi

 

na teknolojia jambo ambalo limezidi sana kukandamiza itikadi na utamaduni wa waswahili kwa ujumla, hivyo kufuata mfumo kutokana na wakati na wageni katika nchi ya Zanzibar.

13.2 VYAKULA

Utamaduni wa mswahili katika ulaji hapo awali kulikua na vykula vingi vya asili ambavyo walikua wakitumia ikiwemo mabobwe, manda nk. Utamaduni huu wa ulaji wa vyakula vya asili umekua tofauti na sasa kutokana na maendeleo na makuzi ya nchi na kupelekea waswahili kula vykula vya kisasa ambavyo ni tofauti na vya zamani. Mfano utamaduni wa sasa wa ulaji kwa waswahili umejikita zaidi katika vyakula vya aina ya protini na mafuta ukilinganisha zamani ambapo wakitumia sana nafaka, majani na kadhalika.

Katika utamaduni wa mswahili umepekea madiliko makubwa katika upishi na ulaji wa vyakula na kupelekea kuacha kutumia mbinu za upishi na ulaji wa vyakula ambavyo huwatambulisha waswahili, hali hii hutokezea kutokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia. Mfano kutumia nyama za kutengeneza kama vile peduu badala ya vitoweo vya baharini, kutumia mafuta kwa wingi badala ya nazi kama vile wali wa mafuta, mchuzi wa mafuta na nyama kwa wingi.

Kutokana na hali hii imepelekea kupotea kwa utamaduni wa zamani wa vykula kwa Waswahili.

Picha hapo chini inaonesha jinsi utamaduni wa sasa wa Waswahili katika vyakula vyao ambapo sana hutumia mafuta kuliko nazi ambayo ni asili kwa Waswahili. 

                      

 

 

 

 

 

Description: C:\Users\RM\AppData\Local\Microsoft\Windows\INetCache\Content.Word\IMG-20240505-WA0022.jpg

                                                         

                                                                    

 

 

 

 

Picha.10.1.inaonesha vyakula.

i.Vyakula vya kisasa

Hata hivyo Waswahili katika utamaduni wa chakula kwa kipindi hichi cha sasa hupendelea zaidi kutumia vitoweo vya kisasa ukitoa vile vya asili vya baharini na kutumia zaidi vinavyotengenezwa viwandani kutokana na maendeleo ya kisayansi na teknolojia kama vile kuku aina peduu, nyama za kutengeneza viwandani na kadhalika.

13.4 MAADILI YA SASA

 Kuanzia Karne ya ishrini (20) maadili yalianza kutoweka kidogo mpaka kufikia sasa Karne ya ishrini na moja (21) ambapo maadili hayo ya utamaduni wa mswahili yalibadilika kutokana na maingiliano ya sayansi na teknolojia.  Jambo hilo kupelekea maadili hayo kupotea kwa kiwango kikubwa. Na kutokana na maingiliano ya sayansi na teknolojia watu wa sasa katika zama hizi kuiga maadili ya kigeni ambapo wanaenda kinyume na maadili yao na kusababisha maadili kupotea. Mfano ni watu kuvaa nguo ambazo hazina maadili na utamaduni wa mswahili

Description: C:\Users\RM\AppData\Local\Microsoft\Windows\INetCache\Content.Word\IMG-20240504-WA0016_010510.jpg

Picha.10.2.mavazi ya vijana wa sasa.

Vile vile Kuna mitindo mbali mbali ya mikato ya nywele ambayo mitindo hiyo hapo zamani ilikuwa haitumiki lakini kutokana na utandawazi ulioingia ulimwenguni sasa vijana wakiume wanakata mitindo hiyo ambayo ni kinyume na maadili yao ya mswahili. Mfano wa mitindo hiyo ni kama ifuatayo:

Description: C:\Users\RM\AppData\Local\Microsoft\Windows\INetCache\Content.Word\Screenshot_20240505-133338_013908.jpg

 

 

                                     

Picha.10.3.inaonesha mikato ya vija wa sasa.

Pia wanawake wanasuka mitindo mbali mbali ambayo imeletwa na wageni mbalimbali na kutokana na utandawazi ulioingia ulimwenguni umepelekea wanawake hao kuacha maadili ya misuko yao ya utamaduni wa msw ahili. Mfano wa mitindo hiyo ni kama ifuatayo:

Description: C:\Users\RM\AppData\Local\Microsoft\Windows\INetCache\Content.Word\Screenshot_20240505-133538_013859.jpg

 

 

 

                                              

Picha.n.10.4.mitindo tofauti ya misuko ya wanawake.

Pia wanawake wanaenda kinyume na maadili ya mavazi ya zamani ambayo yana stara na heshima kwasababu una uwezo wa kuvaa popote lakini kutokana na utandawazi uloingia ulimwenguni sasa vijana wa kike wanavaa nguo za mibano ambayo haziendani na utamaduni wa maadili ya mswahili.

14.1 UCHUMI WA WATU WA ZANZIBAR WASASA.

Uchumi wa Zanzibar umekuwa ukibadilika na kuendelea kukua kutokana na maendeleo ya sayansi katika njia kadhaa. Matumizi ya teknolojia, mawasiliano, na mifumo ya usafirishaji yamechochea mabadiliko makubwa. Hapa chini ni baadhi ya mambo yanayo pelekea mabadiliko na maendeleo ya uchumi wa Zanzibar:

i.Mawasiliano

 Kuongezeka kwa upatikanaji wa simu za mkononi na intaneti Zanzibar kumeleta mapinduzi katika jinsi biashara inavyofanyika. Wafanyabiashara sasa wanaweza kuwasiliana kwa urahisi na wateja wao, kufanya biashara mtandaoni, na kufuatilia mwenendo wa soko la kimataifa.

ii.Teknolojia ya Kilimo

Maendeleo katika teknolojia ya kilimo kama vile matumizi ya mbolea za kisasa, mifumo ya umwagiliaji, mbinu za kilimo endelevu zimeboresha uzalishaji na ubora wa mazao Zanzibar, hivyo kuongeza fursa mbalimbali kupitia mazao ya kilimo na kusababisha uchumi kukua.

iii.Usafirishaji.

Uboreshaji wa miundombinu ya usafirishaji kama vile bandari, barabara, na viwanja vya ndege umefungua fursa za uzalishaji kwa watu wa Zanzibar. Usafirishaji wa haraka na salama unarahisisha uagizaji na usafirishaji wa bidhaa, hivyo kukuza kipato cha nchi.

Picha.n.10.5.inaonesha usafiri wa sasa waswahili.

vi.Ufugaji na viwanda.

Sayansi imechangia sana katika kuboresha sekta ya ufugaji na viwanda Zanzibar. Kupitia matumizi ya mbinu za kisayansi, wafugaji na wawekezaji wa viwanda wamefaidika na maendeleo makubwa katika uzalishaji na ubora wa bidhaa zao. Katika sekta ya ufugaji, sayansi imesaidia kuboresha mifugo iliyopo na kuongeza uzalishaji wake. Kwa mfano, kuzaa kwa njia ya kisayansi imesaidia kuzalisha mifugo yenye sifa nzuri za utumiaji, uzalishaji wa maziwa, na nyama. Wanasayansi pia wamefanya utafiti wa lishe bora na mifumo ya usimamizi wa afya ya mifugo ili kuongeza uzalishaji wao.

Picha.10.6.inaonesha ufugaji wa sasa wa waswahili.

Kwa upande wa viwanda, sayansi imeongeza ufanisi na ubora wa bidhaa. Mbinu za kisayansi zimeboresha mchakato wa uzalishaji kwa kufanya tafiti za kisayansi na kuweka mazingira bora ya utengenezaji wa bidhaa. Pia, teknolojia za kisasa zimekuzwa na kutumika katika viwanda vya Zanzibar, kama vile teknolojia ya usindikaji wa chakula na utengenezaji wa vifaa vya kisasa.

14.2 MSIBA WA SASA.

Mzee MWITA MASEMO MAKUNGU wa makunduchi tarehe 25/4/2024 katika mahojiano ya Waswahili wa sasa wakati wa msiba alisema kuwa waswahili wasasa wanaonekana kwa kiasi kikubwa kuwa na mabadiliko ya utamaduni waliokuwa nao na kujiingiza katika utamaduni unaotokana na wageni katika suala la misiba. Waswahili wa leo wakati mtu anapofariki, hukusanyika kama kawaida, lakini kuna mambo kiutamaduni yamebadilika kama yafuatayo:

Kulipishana wakati wa kuchimba kaburi la maiti; Uchimbaji wa makaburi kwa sasa kuna watu maalumu wanaohusika na masuala hayo, hivyo watu hulipishwa ili wachimbiwe kaburi kwa ajili ya kumstiri maiti wao.

Hitima na dua baada ya mazishi kwasasa jamii nyingi za waswahili zimeacha utamaduni huo. Hivyo, baada ya watu kumzika maiti hutawanyika.

Wanaofanya matanga hujikusanya na kuona kuwa katika siku tatu zile wamepata sehemu ya  kujistiri ( Yani kupata chakula).

15.1 SHEREHE NA MICHEZO YA SASA KATIKA TAMADUNI ZA KIZANZIBAR.

Wazanzibar wanatekeleza sherehe mbali mbali ambazo zinatekelezwa katika kuudumisha na kuuwenzi utamaduni wao, miongoni mwa sherehe ambazo zinatekelezwa na wana jamii wa Zanzibar ni pamoja na hizi zifuatazo.

i.Sherehe za Harusi. Harusi ni miongoni mwa sherehe ambayo ndani yake imeonekana kwa kiasi kikubwa kuwa inaendeshwa Katika jamii zetu za Zanzibar, sherehe hizi za Harusi zinaambatana na tamaduni nyingi za sasa au za wakati huu wa muelekeo wa sayansi na teknolojia miongoni mwa tamaduni hizo ni pamoja na.

Wazanzibari wa sasa wana tamaduni ya kuwaalika watu katika sherehe zao kwa kutumia kadi maalumu; Kadi ambazo zitawatambulisha kuwa wao ni watu halali walioalikwa katika sherehe hiyo hiyo ya harusi. Kwa namna hii watu hupewa mualiko ili wahudhurie katika shughuli hiyo, Jambo ambalo lina sababisha mgawanyiko wa wana jamii kwa kiasi kikubwa kwa sababu inakuwa na ubaguzi ndani yake kwani hasa hasa kadi hupatiwa watu wa tabaka la juu na kuachwa watu wa tabaka la chini jambo ambalo kiuhalisia hasa watu wa tabaka la chini ndio wenye shida na mahitaji mengi katika maisha yao.

 Pia sherehe za Harusi za wakati huu zinaambatana na vazi maalumu lenye kufanana kwa wanawake (VIJORA). Vazi hilo kwa upande mwengine linaitwa sare ambazo huamuliwa na upande wa kike kwa kila mmoja anatakiwa awe amepata sare hiyo ya kijora kama wanavyo iita kutokana na mazoweya yao. Hii ni miongoni mwa tamaduni zilizo anza hivi karibuni unaoonekana kutekelezwa katika sherehe nyingi za harusi za Zanzibar.Wanawake wanakuwa na umoja na mshikamano katika hilo, kutokana na umoja wao wanasababisha harusi kuwa na sura yenye mafanikio kwao. Vazi hilo la kijora linakuwa na mtandio ambao unakuwa na rangi iliyofanana sawa na kijora.

Description: C:\Users\IBRAHIM\AppData\Local\Microsoft\Windows\INetCache\Content.Word\Screenshot_20240506-165632.png               Description: C:\Users\IBRAHIM\AppData\Local\Microsoft\Windows\INetCache\Content.Word\Screenshot_20240506-165639.png

                                  Picha.10.7.inaonesha vazi la vijora wanavyo vaa waswahili.

Aina ya kwanza ya vazi hilo la kijora na wakati linaspovaliwa.

 Aina hii wanawake wanavaa wakati wa Asubuhi wa siku ya Harusi; Wanavaa kwa ajili ya kazi ndogo ndogo za nyumbani ambako Harusi inafanyika kutokana na kazi hizo zinazochukuwa nafasi wakati huo ni lazima kwa baadhi ya Harusi pawepo na vazi maalumu litakalotawala wakati huo ili iwe rahisi kwa wakati huo kujuwa wanao husika na shughuli hio.

Vazi la pili huvaliwa wakati wa kuchukuwa Harusi; Huu ni wakati muhimu kwa wenye shughuli hii watu wanakuwa na sare maalumu inayowekwa kwa ajili ya uchukuwaji wa Harusi. Mara nyingi unakuwa ni wa masafa marefu kiasi kwamba haiwezekani kuvaa vijora ambavyo wameshinda navyo (kuvivaa) tokea asubuhi hivyo basi wanabadilisha vazi hilo ili waweze kuwa na sura nyengine pale wanpokwenda ugenini; Ambako wanakwenda kuchukuwa Harusi na pia kwa Harusi ya kike inakuwa na hali hiyo hiyo ilimuradi tu waweze kuikamilisha sherehe yao walioifanya.

Vazi la tatu linavaliwa wakati wa kwenda holini; Kwa tamaduni nyingi za kizanzibar wanavaa nguo nyengine wakati wa kwenda holini wakiwemo Harusi wa kike na Harusi wa kiume. Wanafanya hivyo pia ili kuuenzi na kuendeleza utamaduni wao walionao sasa wakiachana tamaduni za zaman zilizopitiwa na wakati.

Mashirikiano katika uchukuwaji wa harusi; Tamaduni za sasa za kizanzibar zimekuwa zimekuwa zikifanywa na watu wenyewe kwa kushirikiana wakati wa uchukuwaji wa harusi kwa wanaume na wanawake wanakodi magari maalumu ambayo yanaweza kutumika wakati wa safari hizo. Mashirikiano hayo yanaendelezwa kwa watu wote wa kinzanzibar, Hali hii ya mashirikiano inapotekelezwa kikamilifu inapelekea kuuwenzi utamaduni wasasa wa kinzanzibar ili uweze kubakia na kurithishwa kutoka kizazi hadi kizazi kwa namna hii, Na kwa upande wa wanawake wanaambatanisha  safari hizo wakiwa na nyimbo za taarabu kwenye magari yao wanayopanda kwenda kuchukuwa Harusi ambapo pia ndani yake wanakuwa na furaha kupitiliza kiasi ambacho wanacheza muziki ndani ya gari huku gari ikiwa kwenye mwendo mkubwa bila kukumbuka athari ambazo zinaweza kutokezea kwa kufanya hayo; Hali hii hasa hasa kwa sehemu za mjini  inaonekana kwa kiasi kikubwa kuliko sehemu za vijijini.

Maharusi kupelekwa maholini; pia tamaduni za Sasa za kizanzibari kwa baadhi ya wanajamii wanawapeleka maharusi wao katika holi ambako wanafanya hivyo ili kuweza kufanya sherehe ya Harusi hiyo, inaweza kuwa baada ya kurudi kuchukuwa Harusi au siku nyengine yeyote ya mbele kutoka siku Ile ya Harusi, Wanakwenda huko, Sherehe hiyo ya holini inakuwa na waalikwa mbali mbali, pia inajumuisha Wanaume, Wanawake, Wazee, Vijana na Watoto. Shughuli hio pia inaambatana na muziki na baadhi ya kasida zinazoendana na sherehe za harusi.

ii.Sherehe za Maulidi, Maulidi pia ni sherehe zilizomo katika visiwa vya Zanzibar Hivyo maulidi ni sherehe zinazoendelezwa kwa muda mrefu sana na Hivyo sasa kwa kiasi kikubwa inaonekana kuwa, zimeshika hatamu kwa namna ambavyo zinatekelezwa katika jamii zetu za sasa sherehe hizo zinaambatana na mambo mengi yakitamaduni yakiwemo.

 Maulidi ya Harusi

Upigaji wa madufu: Wanajamii wa Sasa kwa kiasi kikubwa wanaendeleza utamaduni wa kisasa hii inaendeshwa hasa katika sherehe za harusi za wakati huu ambapo kuwa wanawake wanakuwa wanacheza uwanjani wakiwa na sare zao walizozianda kwa ajili ya sherehe hiyo huku wakicheza kwa msongo na furaha juu.

Maulidi ya kuzaliwa kwa mtume.

Pia katika tamaduni za sasa kuna fanyika Maulidi ya kuzaliwa kwa Bwana Mtume Muhammad (S.A.W.) Maulidi hufanyika kila siku ya mwezi 12 mfunguo sita kila mwaka ambako watu wanashereheka kwa hali ya juu Maulidi haya yanaweza kufanywa na watu wa mji na hata madrasa zilizomo ndani ya Zanzibar na kuweza kufanya Maulidi hayo. Watu wa Miji wanafanya Maulidi ya Mji kwa lengo la kuenzi utamaduni wa kizanzibar, Miji mbali mbali ambayo ni marufu kwa ufanyaji wa Maulidi haya kwa kila mwaka ni pamoja na Kisiwa cha TUMBATU, CHAANI, CHARAWE kwa UNGUJA, na CHAMBANI, MUAMBE, KOJANI, MAKANGALE, OLE KIANGA, KIUYU MBUYUNI, MAZIWA NG'OMBE kwa upande wa PEMBA.

Na pia Madrasa mbali mbali zinaendeleza tamaduni hii ya Maulidi mfano wa madrasa hizo ni madrasaat Kamaria, Al madrasaat Anuar ddin Islamiyya, Al madrasaat Nnur islamila, zote hizo zinawaika watu vyuo mbali mbali ili kusherehekea katika Maulidi ya kuzaliwa kwa Mtume Muhammad (S.A.W.) katika sherehe hii ya Maulidi, inaambatana na ratiba maalumu ambao unakuwa ni muongozo mzima wa shughuli hii. Ratiba hii inakuwa na ufunguzi wa Qur'an Tukufu, nasaha za Mwalimu Mkuu kwa wageni na wenyeji waliohidhuria katika shughuli hio, Usomaji wa Kassida,Usomaji wa milango ya Maulidi, Usomaji wa hadithi za Mtume (S.A.W) Mwisho ni ugawaji wa dhifa kwa wageni na wenyeji na mwisho wa shughuli Dua ili kuomba kheir kwa Maulid hayo na baada ya hapo watu wanarudi majumbani  kwao kwa ajili kuendelea na shughuli zao za kimaisha.

15.2 MICHEZO

 Kwa upande wa michezo pia ni tofauti kati ya ile ya kizamani na ya tamaduni za sasa; Michezo ya kisasa ni kama vile:

Mchezo wa mpira wa miguu wa kisasa; Huu ni aina ya mchezo ambao inajumuisha timu mbili na kwa kila timu moja inakuwa na Jumla ya wachezaji kamili kumi na moja, wanakuwa na Jezi maalumu zinazowatofautisha Wachezaji wa timu hizo mbili hii inawasaidia Wachezaji hao pamoja na washabiki katika kujuwa wachezaji wake anaocheza nao katika mchezo na washabiki kujuwa wachezaji wa timu anayoshabikia wakati wa mchezo huo. Mchezo huu unakuwa alama tatu kwa kila mchezo atakapo funga goli, Lakini pia unakuwa na mabadiliko ya wachezaji wakati ambapo mchezaji itatokea kachoka au kutokufanya vyema ndani ya uwanja wakati mchezo unaendelea, Pia mchezo huu unakuwa na muda wa mapumziko, Mapumziko ambayo yanawapa wachezaji kupata fursa ya kujipanga upya

kwa ajili ya mapambano ya awamu ya pili, Kwa sababu viongozi wa timu wanatoa mafunzo ya kutosha dhidi ya wachezaji waweze kupata mafanikio yalio mazuri katika mchezo mafanikio yenyewe ni kupata ushindi na kuchukua alama tatu katika mchezo huo.

Mchezo wa riadha; Riadha ni mchezo ambao unachezwa kwa kushindana wale wanao shiriki katika mchezo huo, mara nyingi mchezo huu unakuwa na makundi wakati wa mshindano ambapo washiriki wanatakiwa kupanga mstari uliosawa kwa ajili ya kuanza riadha, unachezwa katika viwanja vya mpira wa miguu, makundi hayo yanazunguruka uwanja kulingana na makubaliano yao waliokubaliana wenyewe ikiwa ni mizunguruko mitano au kumi itategemea na wenyewe walivokubakiana.

Mashindano ya Baskeli; Mchezo huu unahusisha washiriki mbali mbali ambao Wana uwezo wa kuendesha baskeli maeneo marefu. Hivyo huekewa sehemu maalumu ambayo itatumika kwa ajili ya kuanzia safari ya mashindano hayo na kuwekewa sehemu maalumu ya kufikia ili aweze kujulikana mshindi ni nani na alieshindwa ni nani.

16.1 MAMBO YANAYO PELEKEA KUBADILIKA KWA UTAMADUNI:

Elimu.

Elimu ni moja kati ya mambo makubwa yaliosababisha kupotea au kuachwa baadhi ya tamaduni. Kabla ya kuja kwa elimu watu walikuwa na tamaduni zao, ambazo walikuwa wakizifuata, kwamfano kuabudia mizimu lakini kwasasa asilimia tisiini Mungu ambae wanamuabudia kulingana na Imani zao. Waislamu wao kwa Imani zao wanaamini kuwa mungu wakuabudiwa ni mmoja kwa viumbe wote wala hana anaeshikiana nae katika mambo yake.

Vilevile wanaamini kuwa elimu au kitabu kilichobora ni Qur’ani tukufu. Ambayo iliteremshwa kuja kwao kama nimuongozo wao. Kwaupande wa wakristo wanaamini kitabu cha Bibilia ambacho aliteremshiwa yesu. Na hawa wako wanoamini mungu mmoja na mungu watatu.

Pia elimu ya kisaikolojia ilichangia kwa kiasi kikubwa kubadilika kwa utamaduni. Waswahili waliowengi wanajihusisha na masuala ya kutafuta elimu na kuacha utamaduni wa kupeana hadithi za kale elimu zisizo rasmi. Elimu hii iliwabadilisha waswahili katika masuala mbalimbali kama vile:-

                                i.            Namna gani wanatakikana walime katika mashamba yao ili kuweza kuzalisha kwa kuwango chajuu na kupata mazao yalio bora kwa afya zao.

                              ii.            Vipi wanyama wanatakikana wafugwe ili waweze kupatikana wakati wowote kwa matumizi ya wanaadamu.

Teknolojia. 

Teknologia ilipoingia katika miji ya waswahili hususan Zanzibar imeathiri sana utamaduni wa mzanzibari. Teknolojia tunaweza kusema kuwa nibaba wa mabadiliko ya haraka kutokana nakuwa watu wengi wanatumia teknolojia katika mambo yao na maisha yao ya kila siku. Mambo yafuatayo yanaonesha kuwa tekknolojia imeharibu ama kubadilisha utamaduni wa mswahili:-

                                i.            Matumizi makubwa ya vyakula vya kisasa kama vile peduu. Teknolojia imekuja na mfumo wa kuzalisha kuku kwa haraka na kutumika kama chakula. Waswahli kwa kiasi kikubwa wanatumia aina hii ya chakula.

                              ii.            Teknolojia imebadilisha namna ya uvaaji. Waswahili wasasa wameacha mavazi na namna ya uvaaji wao wa asili. Na hii nikutokana na muingiliano wa sayansi na teknolojia.

                            iii.            Teknolojia imesababisha kubadilika kwa mikato ya nywele. Ukiangalia vijana wasasa wanamikato tofauti ukilinganisha na utamaduni wao.

Mahusiano ya kimataifa.

Mahusiano ya waswahili na nchi nyengine yanachangia kubadilika kwa utamaduni wa waswahili. Katika uhusiano kuna namna mbalimbali, kama vile:-

                                i.            Kukubaliana kuingiza bidhaa yoyote katika nchi. Kwa mfano uingizwaji wa madawa ya kulevya , hii husababisha kubadilika kwa utamaduni. Zanzibar ni nchi ilio na mahusiano na nchi nyingi hivyo kulingana na makubaliano yanapelekea kuharibika kwa utamaduni wa wazanzibar na kuingia utamaduni mwengine.

17.1 FAIDA ZA UTAMADUNI

Utamaduni wa watu wa zamani ulikua na faida nyingi kama vile:

  1. Umoja na ushirikiano; Utamaduni ulikua na nguvu katika Kuimarisha ushirikiano na umoja kati ya watu wa jamii moja
  2. Heshima kwa wazee; Utamaduni unafanya watu kuweka heshima kubwa kwa wazee na maarifa Yao.Wazee waliheshimiwa kama viongozi na walikua na jukumu muhimu katika kusimamia jamii.
  3. Ulinzi wa mazingira; Utamaduni ulikua na mifumo ya kuhifadhi mazingira na rasilimali za asili.

18.1 HASARA ZA UTAMADUNI

Miongoni mwa hasara za utamaduni ni kama zifuatazo:

  1. Kupotea kwa lugha na Mila; Utamaduni unakabiliwa na hatari ya kupotea kwa lugha za asili na Mila kutokana na mabadiliko ya kijamii na kiuchumi.
  2. Kuathiriwa kwa teknolojia; Maendeleo ya teknolojia yameathiri utamaduni kwa njia nyingi ikiwa ni pamoja na kusababisha kupotea kwa mazoea ya kiutamaduni na kuleta mabadiliko katika mawasiliano na mahusiano ya kijamii.
  3. Mmonyoko wa maadili; Utamaduni unakabiliwa na changamoto ya mmonyoko wa maadili kwa jamii ambao unaweza kusababisha migogoro na vitendo viovu katika jamii.

 

 

 

 

HITIMISHO

Makala hii imelezea kwa kina kihusiana na utamaduni wa mswahili baada ya mapinduzi ya 1964 hadi 2024.katika kipindi hichi utamaduni wa watu wa Zanzibar ulipitia katika vipindi mbalimbali. Vipindi hivo ni kipindi cha mwanzo wakati Mzee Abeid Amani karume baada ya mapinduzi matukufu 1964 alipowaelekeza waswahli waendeleze utamaduni wao na kuuboresha katika vipengele mbalimbali kwa mfano Maadili, vyakula, Elimu,Siasa nakadhalika. Kipindi cha pili niwakati teknolojia iliposambaa zaid ndani ya Zanzibar.Hapa Utamaduni ulibadilika kwa kiasi kikubwa, mila, desturi, maadili, vyakula, mavazi, Sanaa, na hata tabia za watu zimebadilika kwa asilimia 80% ,licha ya kuwa baadhi ya sehemu bado watu wanayaendeleza.

Cha muhimu ni kuwa waswahili wasiwe niwenye kukubali kirahisi kupokea utamadu ambao unaharibu heshima na maadili ya wazanzibari.kwani kwa kufuata mambo yanayoletwa na watu wengine ndio sababu inayopelekea kupotea kwa utamaduni wetu. “usiache mbachao kwa masala upitao” na tukumbuke “mkataa kwao mtumwa”.

 

 

MAREJELEO

Baraza la kiswahi la Zanzibar. (BAKIZA). (2008).Utamaduni wa mzanzibar. Zanzibar.Baraza la Kiswahili la Zanzibar.

Kamisheni ya utamaduni na michezo. (2012).hazina inayopotea :bodi ya sensa ya filamu na sanaa mchezo. Chukwani Zanzibar.

Ministry of information, culture, tourism and sport. (2013).commition of culture:inventory of intangible cultural heritage .Zanzibar ,UNESCO; Zanzibar Tanzania.

Mzee Mwita M asebo Makungu. (2024). Historia ya Utamaduni wa Makunduchi. (Mahojiano ya ana kwa ana). Makunduchi, Zanzibar.

Wizara ya elimu utamaduni na michezo. (2005).Sera utamaduni wa Zanzibar .serikali ya mapinduzi ya Zanzibar .Zanzibar.

 

            

0 maoni:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Wasiliana nami papo kwa papo

Name

Email *

Message *

Ads 468x60px

Breaking News

Top Featured

Featured Posts

Sample text

Sample Text

Recomended

Facebook

Advertise

Most Popular

Connect With Us

Followers

Social Icons

Pages

Pages

BTricks

Pages

Popular posts

Tafuta chochote ukiwa hapahapa

Kategori

Recent Comments

You can replace this text by going to "Layout" and then "Page Elements" section. Edit " About "

recent posts

Video Of Day

TRANSLATE

Instructions

Video

Flickr Images

FURAHIA UWEPO WAKO HAPA

Logo Design by FlamingText.com
Logo Design by FlamingText.com

Imetembelewa mara

NUMBER OF VIEWERS

Popular Posts

SAJIRI

Definition List

premium-wordpress-themes.org