17 Jun 2025

 Imeandikwa na Mtila Mswahili  




UTANGULIZI

Maana ya utamaduni

Ali M. Rashid (2012)  anaeleza kwamba, neno utamaduni lina asili ya lugha ya kiarabu ambalo maana yake ya msingi ni “dini”; anaeleza kwamba baada ya kutoholewa na kuingizwa katika lugha ya kiswahili lilichukuliwa umbo la utamaduni na baadae kusanifishwa na kuwa utamaduni.

Anahitimisha kwa kusema neno utamaduni lina maana ya mfumo mzima unaofuatwa na mwanadamu katika maisha yake ya kila siku.

Pia  williams (2010) ameeleza kuwa utamaduni ni njia ya maisha, sanaa na nyenzo zenye kutoa maana.

Omar (1981 : 3) akimnukuu Tylor anasema kuwa utamaduni ni maisha ya mwanadamu ambayo yana ufahamu wa elimu, imani, sanaa,maadili, mila, sheria na desturi.

Utamaduni wa mswahili ni utaratibu wa jumla uliowekwa na waswahili ili kuufuata utaratibu huo.

Maana ya mswahili, kwa mujibu wa Kamusi la kiswahili fasaha  lililoandikwa na BAKIZA

Mswahili ni mtu mwenye asili ya mwambao wa Afrika Mashariki na ambae lugha yake ya awali ni kiswahili na hufuata utamaduni wake

Pia Flora Mallema, Mwenyekiti wa Chama Cha Lugha Na Fasihi Ya Kiswahili Tanzania anasema, mswahili ni mtu ambaye anafanya mambo ya kiswahili, anazungumza kiswahili na mambo yafananayo na uswahili.

   MSWAHILI WA ZAMANI AU   MSWAHILI HALISI

Ni mtu mwenye asili ya pwani ya Afrika mashariki ambaye maisha yake yalitawaliwa na mila,desturi na utamaduni wa Mswahili. Huyu ni mtu ambaye maisha yake yalihusiana moja kwa moja na ustaarabu na tamaduni zote za mswahili. Mswahili halisi alikuwepo kabla ya ujio wa wakoloni . Kiswahili  kichotumika na mswahili wa zamani kilikuwa halisi  na kimejaa misemo, methali na maneno ya heshima

MSWAHILI WA LEO;

   Ni mtu wa jamii ya kiswahili anayeishi katika muktadha wa kisasa, akichanganya maisha ya kiutamaduni na athari za maendeleo ya kiuchumi, kijamii, kiteknolojia na kiutandawazi. Huyu ni mtu ambaye bado anaweza kuwa na mizizi ya kiutamaduni ya mswahili,lakini maisha yake yameathiriwa na mabadiliko ya ulimwengu wa sasa.

SIFA ZA UTAMADUNI WA MSWAHILI

Utamaduni wa mswahili  una sifa ya kuwagawa watu katika makundi. Utamaduni wa mswahili huigawa jamii katika makundi mfano wanaume huhusika na masuala ya kutafuta rizki, wanawake shughuli za nyumbani na watoto  madrasa.

TATHMINI

Waswahili wa sasa huingiliana katika majukumu mfano zamani ilikuwa suala la uongozi wa jamii ni la wanaume lakini sasa hata wanawake pia ni viongozi wa jamii. Pia katika shughuli za kutafuta rizki lilikuwa ni la wanaume lakini waswahili wa sasa wanawake pia hujishughulisha na harakati za kutafuta rizki mfano kubeba zege nakadhalika.

kuna matabaka mingi ya kidini ambayo kila siku yanaleta migogoro katika jamii.Na kuhusu mashirikiano ya kijamii hayapo kutokana na  sasa kila mtu na familia yake. Kwa hivyo tunaona ni kwa kiasi kikubwa waswahili wa leo hawafuati utamaduni wa zamani unaoleta mashirikiano na umoja ndani yake.

2) Utamaduni wa Mswahili una sifa ya kubadilika kulingana na mabadiliko ya wakati na kukua kadri nyakati zinavyosonga. Hii ina maana kuwa Mswahili hajafungwa na mila au desturi zisizobadilika

bali huwa na uwezo wa kuchukua vipengele vipya kutoka kwa jamii nyingine au kutokana na maendeleo ya kiteknolojia, ilimradi visiathiri maadili ya msingi ya utamaduni wake kama vile heshima, utu na mshikamano wa jamii.

   mifano kutoka kwa mswahili wa zamani.

Mavazi:  Zamani, Mswahili alivaa khanga, kanzu, na buibui. Alipokutana na Waarabu na Waajemi, mavazi hayo yaliboreshwa – mfano: kanzu ya Kiomani au buibui ya kihijabu.

Lugha: Kiswahili kilianza kama lugha ya jamii ya Pwani, kisha kikachukua maneno kutoka Kiarabu, Kireno, Kiingereza na Kijerumani, na hivyo kuendelea kukua bila kupoteza kiini chake.

 Sanaa: Muziki wa Taarab ulianza kama wa Kiarabu lakini ukaboreshwa na ladha za Kiafrika na Kiswahili

TATHMINI KWA MSWAHILI WA SASA:

Mswahili wa sasa anaendelea kuendana na sifa hii ya kubadilika, lakini kwa kiwango kinachohitaji tahadhari. Mfano: 

Mavazi – Mswahili wa sasa huvaa mavazi ya kisasa kama jeans au t-shirt, lakini wengine bado wanavaa kanzu au khanga katika hafla za heshima.

Teknolojia – Mswahili wa sasa anatumia simu na mitandao ya kijamii kusambaza mashairi, ngoma, au hadithi – njia mpya ya kudumisha sanaa ya zamani kwa mitindo ya kisasa. 

Utamaduni wa Mswahili una sifa ya kurithishana amali za jamani kutoka kizazi  hadi kizazi.  Utamaduni wa mswahili huwawezesha waswahili kurithishana;

Mila na Desturi: Jamii ya Waswahili ina mila nyingi ambazo zimekuwa zikirithiwa, kama vile sherehe za ndoa, maulidi,mazishi, sherehe za jando na unyago ngoma za asili na matukio mengine ya kijamii. Hizi ni sehemu muhimu ya utambulisho wa jamii na husaidia kuimarisha mshikamano

-  Mapishi na chakula: Mapishi kama vile makopa, msambwija, vipopoo wali na vyakula vyengine.  Hii si tu njia ya kuendeleza utamaduni bali pia huonesha utambulisho wa Mswahili.

Sanaa: Sanaa za Waswahili kama vile uchoraji, uchongaji, na muziki ni sehemu muhimu ya utamaduni wao. Waswahili hutumia sanaa hizo ili kuendeleza urithi wao wa kifasihi na kisanaa.

Waswahili wa sasa hurithishana amali za jamii kwa kiwango khafifu sana. Mfano katika mavazi  kwa asilimia ndogo wamerithishana.

Sanaa na miziki. Waswahili wana mziki na sanaa walizozirithi   mfano wa sanaa hizo ni ngoma za msewe, ngoma za kibati nakadhalika

Lakini waswahili wa sasa ni  kwa asilimia ndogo sana wanasikiliza ngoma hizi kutokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia.

4) Utamaduni wa Mswahili una sifa ya kufungamana na dini ya kiislamu. Utamaduni wa mswahili na dini ya kiislamu ni kama sarafu moja, waswahili hufata mila na taratibu za kiislamu kama kuswali, kufunga, kuhiji,kusoma Qur an na pia kuvaa mavazi kama vile shungi, baibui na kofia

   Pia katika taratibu za kula mfano kula kwa mkono wa kulia ni sheria ya kiislamu na ni moja ya taratibu za utamaduni wa mswahili.

TATHMINI

Kutokana na jambo hilo tunaona kwamba waswahili wa sasa bado wanafata utamaduni huu, hivyo wanaendana mno na sifa hii.

5) Utamaduni wa Mswahili una sifa ya kuwa na miiko juu ya mambo fulani. Mfano mwanamke akiwa mjamzito ni mwiko kula mayai,  mtoto akizaliwa  atakuwa hana nywele, ni mwiko kukata kucha usiku, ni mwiko chumvi kuita chumvi kwa wakati wa usiku na iitwe dawa ya jiko au mkubwa wa jiko,pia ni  mwiko kukata nywele usiku nakadhalika.

      TATHMINI

Waswahili wa zamani walikuwa wanafuata vyema na kuheshimu miiko iliyowekwa lakini waswahili wa sasa kwa kiwango kikubwa hawaheshimu miiko mfano suala la kukata nywele usiku, kula mayai kwa wajawazito, kukata kucha usiku na mambo mengi waswahili wa sasa huyafanya licha yakuwa mambo hayo ni miiko

 

6)   Utamaduni wa mswahili una sifa ya kuwafanya waswahili wawe na umoja na ushirikiano. Katika masuala mbalimbali waswahili huwa pamoja kwa kushirikiana kutokana na namna ambavyo utamaduni ulivyo mfano katika chakula familia hukusanyika pamoja na kula, misiba, kushirikiana katika malezi ya watoto nakadhalika

TATHMINI

Waswahili wa leo wana ushirikiano katika baadhi ya sehemu mfano katika msiba, ndoa, na baadhi ya sehemu hawana umoja na ushirikiano mfano katika kula, waswahili wa leo wengi wao hula kila mmoja peke yake

 


0 maoni:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Wasiliana nami papo kwa papo

Name

Email *

Message *

Ads 468x60px

Breaking News

Top Featured

Featured Posts

Sample text

Sample Text

Recomended

Facebook

Advertise

Most Popular

Connect With Us

Followers

Social Icons

Pages

Pages

BTricks

Pages

Popular posts

Tafuta chochote ukiwa hapahapa

Kategori

Recent Comments

You can replace this text by going to "Layout" and then "Page Elements" section. Edit " About "

recent posts

Video Of Day

TRANSLATE

Instructions

Video

Flickr Images

FURAHIA UWEPO WAKO HAPA

Logo Design by FlamingText.com
Logo Design by FlamingText.com

Imetembelewa mara

NUMBER OF VIEWERS

Popular Posts

SAJIRI

Definition List

premium-wordpress-themes.org