KIMOJA
i.
Nyumba hujengwa kwa mawe, Nawe umenijengea,
Ukaipamba
vigawe, Izidi kunivutia,
Huduma
zako na wewe, pesa mimi kutumia,
Kimoja
umesahau, ngoja leo nikwambie.
ii.
Ukanipatia gari, nipate kutembelea,
Ikawa
kwangu fahari, kwa wazazi salimia,
Mikufu
pia bangiri, mapambo kunipambia,
Kimoja
umesahau,Ngoja leo nikuambie.
iii.
Ukachimba na kisima, shida ya maji kuua,
Ukasahau
heshima, na dhima ya kunioa,
Ndiyo
nakupa lawama, Hujajua nini ndoa,
Kimoja
umesahau, ngoja leo nikwambie.
iv.
Ukanipa na madini, ukajua ndiyo penzi,
Ukaivaa
miwani, ukadhani mwisho kazi,
Kumbe
tatozo chumbani, mficho na nyingi tenzi,
Kimoja
umesahau, ngoja leo nikwambie
v.
Ukafungua mradi, nipate kuendeleza,
Imani
na Itikadi, matatizo kupwekeza,
Maisha
ninafaidi, kimoja nakipoteza,
Kimoja
umesahau, ngoja leo nikwambie.
vi.
Sasa ngoja nikwambie, hicho ulichosahau,
Usahihi
jifanyie, nami nipate walau,
Nami
ndani nitulie, kazi yako we mdau,
Kimoja
umesahau, ngoja leo nikwambie.
vii.
“HUBA” hujenga mahaba, ndicho ulichosahau,
Nimekosa
mi kushiba, ndiyo kisa cha dharau,
Sahihisha
mara saba, kwangu iwe angalau,
Kimoja
umesahau, ngoja leo nikwambie.
viii.
Pesa hujenga majumba, wala hajengi mapenzi,
Pesa hununua shamba, kwenye
penzi si mjenzi,
HUBA ndiyo vunja mwamba, kama
nazi na mkwezi,
Kimoja
umesahau, ngoja leo nikwambie.
ix.
Wewe tajiri wa mali, maskini wa mahaba,
Mali
kwangu siyo dili, Dil kubwa lako huba,
Kazi
kwako kufasiri, nipatie pate shiba,
Kimoja
umesahau, ngoja leo nikwambie
x.
Kingine mkono wako, umeshindwa
kukazana
Kwangu
machache mashiko, zana zinapokutana,
Kubwa
tatizo ni lako, mkono kutokazana,
Kimoja
umesahau, ngoje nikwambie.
xi.
Nimeshasema machache, jaribu kuyatatua,
Taki
toka nikuache, wewe ni wangu wa ndoa,
Ya
zamani tuyaache, jenga yetu familia,
Sasa
nimeshakwambia, kitu ulichosahau.shairi kimoja