21 Sept 2019


SWALI
1. Dadavua maana ya dhana mawasiliano kwa kurejelea nadharia mbalimbali.
2. Istilahi stadi za mawasiliano hufafanuliwa kwa kuzingatia nadharia mbalimbali.  
    Jadili

1. Dadavua maana ya dhana mawasiliano kwa kurejelea nadharia mbalimbali.
Kwa mujibu wa Kavoi na Wanjala (2013) wametafasili dhana  mawasiliano ni kitendo cha uwasilishaji  na ung’amuaji  wa maana kati ya watu au jamii kwa kutumia mfumo  wa ishara na miondoko iliyokubalika  katika  jamii mahusisi.
Dhana  mawasiliano imejaribu kuelezwa katika  kitabu cha “stadi za mawasiliano” katika nadharia kuu tatu kwa namna tofautitofauti kwa mujibu wa vijenzi pamoja  na uchangaano wake.Nadharia  hizo zinazojaribu kuelezea maana ya dhana mawasiliano finyu,mawasiliano mauluti na mawasiliano mihamala.
Nadharia  ya mawasiliano fingu; iliyoasisiwa na  Shampon,C.E na Weaver,W(1949).walitafasili mawasiliano  kwa upande mmoja tu yaani mawasiliano na simu.Aina hii ya mawasiliano fingu inahusu vipengele vitatu ambavyo ni mtoa ujumbe,ujumbe na mlengwa.Nadharia hii hutuumiza zaidi katika  shghuli za utawala.waasisi  hawa pia walibainisha  kuwa kelele  ndio chanzo kikubwa  kinachokwamisha mawasiliano.vilevile nadharia hii imeshindwa kuonyesha marejeo ya ujumbe anaotumia  mtoa ujumbe kwenda  kwa mlengwa.
Pia waitifaki wameweza kuelezea dhana ya mawasiliano kwa kutumia nadharia ya mawasiliano mahuluti waitifaki wameichukulia aina hii ya mawasiliano kuwa kwa kiasi fulani ni kamilifu,mawasiliano mahuluti huhusisha vipengele vitano ambavyo ni mtoa ujumbe,ujumbe,nyenzo,mpokea ujumbe na jibu.Aina hii ya mawasiliano huonyesha namna mtoa ujumbe  anavyogusana  na kuingilia  na mpokea ujumbe kupitia majibu yanavyotolewa,ili kuwa na mawasiliano timilifu katika uhusiano wa mtagusano mtoa ujumbe na mpokeaji  ujumbe  hubadilishana  nafasi.Nadharia hii ni mari zaidi ila hainyooshi uhalisia wa uchangamani  wa mchakato  wa mawasiliano.
Waitifaki wa nadharia hii ya mawasiliano mhamala wanadai kuwa wahusika katika mchakato wa mawasiliano huwa hawapeani zamu ya kutoa ujumbe,kuupokea ujumbe wala kutoa jibu.Waasisi hawa wanaamini  kuwa hutokea kwa wakati mmoja wao huchukulia mawasiliano kama mfumo wenye hatua madhubuti na unaojengwa  kwa mihimili inayotegemea,mihimili hiyo ni ujumbe,nyenzo,mtoa ujumbe,mlingwa,jibu,muktadha wa mawasiliano, idadi ya wahusika tajriba(utamaduni) ya wahusika na hali ya upokeaji na wawasilishaji.
Kwa ujumla mchakato wa mawasiliano unahusisha hatua saba ambazo zimefumwa katika shuka  la muktadha na wahusika .ujumbe,nyenzo,mtoa ujumbe,usimbaji,mpokeaji ujumbe,usimbuaji na jibu kwa hiyo stadi za mawasiliano zinahitajika  muda wote wa mchakato wa mawasiliano.



2. Istilahi stadi za mawasiliano hufafanuliwa kwa kuzingatia nadharia mbalimbali. Jadili
Istilahi” Stadi za mawasiliano” imetokana  na tafsiri  ya istilahi “Communicaion skills” ya kiingereza ,Baaadhi ya watu wameitafasili kama “Mbinu  za mawasiliano”Kimakosa.Istihali za “Stadi za mawasiliano” imeweza kufafanuliwa  au kutafasiliwa katika  nadharia  tatu kuu zinazojaribu kuitafasisi istilahi hii ambozo ni nadharia ya umilisi, nadharia ya ujaminishaji na nadharia ya utawala taarifa na mawasiliano.
Katika kitabu cha Stadi za mawasiliano waitifaki walioweza kuielezea  nadharia ya umilisi,  ni pamoja na Smith,Caput,Cupach,Spitznerg,Crettenden na Rawstone wao wanashikilia  kuwa Stadi za mawasiliano humwezesha mwasilianaji kuchajua mbinu stahili ya mawasiliano ili aitumie kuwasilisha  ujumbe  kwa mujibu wa muktadha husika.Nadharia hii inashikilia kuwa mwasilianaji anayemudu Stadi za mawasiliano  anafaa kuwa na hekima,maarifa na motisha inayomwezesha kuteua  nyenzo  tatu za kubeba ujumbe katika muktadha unaofaa,Pia nadharia hii imejengwa katika nguzo kuu nne ambazo ni hekima,motisha,maarifa na muktadha ambozo mwasilianaji anapaswa kuzizingatia  ili aweze kufikisha ujumbe ilivyokusudiwa
Nadharia ya ujiaminishaji; nadharia hii iliasisiwa na  William Gudykunst mwaka 1985,Waitifaki  wake wanadai kuwa maingiliano ya wawasilianaji  wakiwa katika  mchakato wa mawasiliano  hugubikwa na hali ya wasiwasi,uoga na mashaka hususani katika hatua za mwanzo.Hali hii hutokea  zaidi iwapo  wahusika hawafahamiani au wanatofautiana kihadhi,kiumri na kielimu au kikabila,Nadharia  hii hudai kuwa mwasilianaji ambaye anamudu Stadi za mawasiliano anapaswa kuwa na uwezo wa kudhibiti na kushinda hali ya mashaka udhibiti huo huwajengea  wawasilianaji hali ya kujiamini.
Nadharia ya utawalaji taarifa na mawasiliano; waasisi  wa nadharia hii ni pamoja  na De Ridder,Ballinger na De sai. Waitifaki wa nadharia hii wanashiliki kuwa  Stadi za mawasiliano huwawezesha wawasilianaji kubadilishana,kushilikishana na kutumia ujumbe husika pamoja na kuzalisha taarifa mpiga kwa hiari katika mchakato wa mawasiliano.
Kwa ujumla majumuisho ya nadharia hizi yanapatikana katika maoni ya mwanaisimu Cooper (1980) anyesema kuwa mtu anayezimudu  Stadi za mawasiliano ni Yule anayeweza kusema kile anachotaka kukisema na kumaanisha  kile  anachosema bila kupoteza  maana au kuleta utata wowote ule.
MAREJELEO
Wanjala, F.S na Kavoi, J. M. (2013). Stadi za Mawasiliano na Mbinu za Kufundishia  Kiswahili.
               Mwanza: Serengeti Educational Publishers  Ltd
Kiura, M. K. & Munga, E. C. (2010). Communication Skills. Mwanza: Serengeti Educational
                  Publishers Ltd.

   


0 maoni:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Wasiliana nami papo kwa papo

Name

Email *

Message *

Ads 468x60px

Breaking News

Top Featured

Featured Posts

Sample text

Sample Text

Recomended

Facebook

Advertise

Most Popular

Connect With Us

Followers

Social Icons

Pages

Pages

BTricks

Pages

Popular posts

Tafuta chochote ukiwa hapahapa

Kategori

Recent Comments

You can replace this text by going to "Layout" and then "Page Elements" section. Edit " About "

recent posts

Video Of Day

TRANSLATE

Instructions

Video

Flickr Images

FURAHIA UWEPO WAKO HAPA

Logo Design by FlamingText.com
Logo Design by FlamingText.com

Imetembelewa mara

TAKWIMU ZA WATEMBELEAJI

Popular Posts

SAJIRI

Definition List

premium-wordpress-themes.org