18 Jun 2025

 

MAANA YA KIAMBAJENGO KIFUASI.

Besha (1990). kifuasi ni sehemu ya sentensi inayosaidia kuelezea maana ya msingi ya kiambajengo kikuu.

Mfano: "Mwanafunzi anaandika kitabu."

Kiambajengo kikuu: "Mwanafunzi"

Kifuasi: "anaandika kitabu" kinaeleza tendo linalofanywa na kiambajengo kikuu.

Matinde (2015). Matinde anasisitiza kwamba kifuasi ni sehemu inayokamilisha au kuongeza maana ya kiambajengo kikuu. Analeta wazo kwamba bila kifuasi, sentensi inaweza kukosa uwazi wa maana.

Mfano. Mgeni alifika Jana usiku.

Kiambajengo kikuu ni "Mgeni"

Kifuasi . Alifika Jana usiku.

Kamusi la kiswahili fasaha. (2010).Kiambajengo ni kipashio kinachoungana na chengine katika sentensi.

Nida(1949). Kiambajengo kifuasi ni sehemu ya mnyambuliko wa neno inayobeba taarifa za kisarufi zinazohitajika kukamilisha maana ya neno katika muktadha wa sentensi.

Mfano. neno anacheza , kiambajengo kifuasi ni " a" kinaonesha Hali ya wakati uliopo. Katika neno shuleni, kiambajengo kifuasi ni "ni", inaonesha mahali.

Kwa hivyo mkabala wa kiambajengo kifuasi ni mbinu ya uchambuzi wa lugha inayozingatia vipashio vya kisarufi vinavyofuata kiambajengo kikuu kwa lengo la kuelezea maana na uhusiano wa vipas nohio hivyo katika sentensi.

CHIMBUKO LA MKABALA WA KIAMBAJENGO KIFUASI.

Kwa mujibu wa Wana miundo kama vile (Frednand Saussue ) Wanaeleza kuwa istilahi ya kiambajengo kifuasi ilibuniwa na Bloom field (1953). Wanamiundo hawa walitumia mbinu ya uchanganuzi kiambajengo kifuasi ( immidiant constituent analysis.ICA.) na kueleza kuwa bloom field alitambua kwamba sentensi huundwa na mfuatano wa viambajengo ambavyo hupishana kihadhi. Kwa mfano.

a) Mtoto mdogo anacheza mpira.

Kiambajengo kidogo hushirikiana na kiambajengo chenye hadhi sawa katika kuunda kiambajengo kikubwa.

Wazo kuu la mbinu hii ya uchanganuzi ni kwamba, sentensi hugawanywa katika sehemu ndogondogo Hadi kufikia sehemu ambazo haziwezi kugawanywa tena. Kilasehemu hudhihirisha maneno yanayokaribiana na yenye kuhusiana zaidi.

Sehemu ambayo haiwezi kugawanywa zaidi huitwa kiambajengo tamati .

mfano neno " Anacheka" " a" ni kiambajengo tamati.

Katika isimu maumbo kiambajengo kikubwa huwa ni neno , ilhali kiambajengo kidogo ( tamati) ni mofu. Katika sentensi kiambajengo kikubwa ni sentensi na kiambajengo kidogo cha uchanganuzi huwa ni neno.

UTOKEAJI WA DHANA YA UNYAMBUAJI (UPANUZI) KATIKA UCHANGANUZI WAKIAMBAJENGO KIFUASI.

Hii ni sifa ambayo huzipanua na kizipanga sintensi ili kuleta uwiano na kukubalika katika sarufi husika. Kwa mfano

a) mtoto / amepotea .

 b)mtoto mrefu/ amepotea Leo .

c) mtoto mrefu mmnene / amepotea Leo asubuhi.

Unyambuaji huu hudhirisha uhusiano wa maneno kwa mfano Nomino na Kivumishi kuliko Nomino na Kielezi. Kitenzi na kielezi kuliko Kitenzi na Kivumishi.

 Uhusiano wa nafasi zao katika tungo Mfano Kiwakilishi huchukua nafasi ya Nomino ( hii huitwa ubadilishanaji wa nafasi ya utokeaji).Mfano Juma na Ali wameenda msikitini Huwa Wao wameenda msikitini ,

Hadhi yao na mpangilio unaoleta maana na wenye kufuata kaida za kisarufi.  Mfano, Mkulima analima mahindi. Neno Mkulima ambalo ni kiambajengo kikuu ndilo lenye hadhi katika sentensi hii.

Uchanganuzi wa sentensi kwa kutumia matawi hubainisha hadhi ya vipashio katika tungo , kuanzia kipashio kikubwa Hadi kipashio kidogo kabisa. Aidha uchanganuzi huuhutumiwa kuonesha uhusiano wa vipashio katika tungo.


UMUHIMU WA UCHAMBUZI WA KIAMBAJENGO KIFUASI

Kuonyesha viambajengo vya sentensi na kudhihirisha nafasi ya utokeaji na uhusiano wa viambajengo hivyo. Mfano,  Nomino na Kivumishi, Mwanafunzi mnene hapa huonesha uhusiano wa vaimbajengo N+V, Kiwakilishi na Kivumishi, Mfano Wao warefu wamekaa Mbele

Kuonyesha hadhi ya viambajengo katika tungo kutoka kiambajengo kikubwa hadi kiambajengo kidogo.Katika kiambajengo kikubwa ni sentensi na kiambajengo kidogo ni mofu. Mfano, Asha anasoma kitabu

Hapa kiambajengo kikuu ni "Asha" ( mhusika mkuu wa tendo - Nomino).  Pia " anasoma kitabu" ni kiamabjaengo kifuasi

" Amelala" ni kiambajengo kikuu katika neno , ambapo kimbajengo kidogo (mofu) ni " a"  mofu ya nafsi, " me" mofu ya wakati, "Lal" mofu ya mzizi na " a" ni mofu tamati

Huweza kutatua utata katika sentensi mbili au zaidi kwa mfano mama Zakaria amesafiri, sentensi hii ni tata, uchanganuzi kiambajengo kifuasi huondoa utata huu kwa kutenganisha maneno kwa misingi na uhusiano wa viambajengo.                                                                                 Mama/Zakaria amesafiri(kumuarifu Mama kwamba Zakaria amesafiri).                                Mama Zakaria/amesafiri (yaani Mama ake Zakaria amesafiri).

Kiambajengo kifuasi hujibu maswali kama nani? nini? wapi? lini?.Mfano Baba amekwenda sokoni ( sentensi hii imejibu swali la wapi?.)

Mama amepika ( hii inauliza amepika Nini? ) na kuwa mama amepika keki.

 

 

UDAIFU WA MKABALA WA KIAMBAJENGO KIFUASI.

1. Sentensi Zote Kuchukuliwa Kuwa na Muundo wa Kimstari

Uchanganuzi wa kiambajengo kifuasi unadhani kwamba sentensi zote zinafuata mtiririko wa kimstari (maneno yakiungana moja kwa moja). Hii ni changamoto kwani baadhi ya sentensi zina miundo isiyo ya kimstari, kama vile miundo inayojumuisha vipashio vinavyorudiarudia au vifupisho vya maana.

Mfano:

"Aliyekuja jana ndiye aliyenisaidia."

Uchanganuzi wa kimstari utaiona sentensi hii kama muunganiko wa vipashio vilivyopangwa mstari mmoja, lakini kiuhalisia, kuna kipashio cha ndani ("Aliyekuja jana") kilichounganishwa na kipashio kikuu.

2. Kushindwa Kuunganisha na Kuchanganua Sentensi Tofauti

Uchanganuzi wa kiambajengo kifuasi unalenga zaidi lugha maalum badala ya kuweza kuunganisha sentensi kutoka lugha tofauti au hata kuchanganua sentensi zenye muktadha wa lugha mchanganyiko.

Mfano:

Lugha tofauti: "Juma alikwenda sokoni, lakini in the evening he returned late."

Uchanganuzi huu hauwezi kuchanganua kwa ufanisi sehemu ya Kiingereza na Kiswahili kwa pamoja.

3. Kutoweza Kuchanganua Sentensi Zisizo Sahihi Kimuundo

Uchanganuzi huu hauwezi kufasili sentensi ambazo si sahihi kimuundo kwa sababu unategemea muundo wa kawaida wa sarufi.

Mfano:

"Alimkimbilia mwizi mwituni mnene."

Hii ni sentensi isiyo sahihi kimuundo kwani haijulikani kama "mnene" inamhusu mwizi au mwituni. Uchanganuzi wa kiambajengo kifuasi hautoi ufafanuzi wa sintaksia mbadala.

4. Kushindwa Kuonyesha Uhusiano wa Sentensi Zenye Maana Tofauti

Uchanganuzi huu hauwezi kuonyesha uhusiano kati ya aina tofauti za sentensi, kama vile mtenda na mtendewa, au sentensi yakinishi na kanushi.

Mfano:

Sentensi yakinishi: "Mtoto alikula chakula."

Sentensi kanushi: "Mtoto hakula chakula."

Uchanganuzi wa kiambajengo kifuasi hauonyeshi tofauti ya kiuhusiano kati ya sentensi hizi.

5. Kuchanganua Sentensi za Muundo Mmoja Pekee

Uchanganuzi huu hufanya kazi vizuri kwa sentensi rahisi, lakini unatatizika kwenye sentensi changamano au zinazohusisha vipashio vingi.

Mfano:

Sentensi rahisi: "Mama alipika chakula."

Sentensi changamano: "Mama alipika chakula wakati baba alikuwa akifanya kazi ofisini."

Sentensi changamano ina vipashio viwili vinavyotegemeana, hali ambayo uchanganuzi wa kiambajengo kifuasi hauwezi kuichanganua kwa ufanisi.

6. Kutobainisha Uhusiano wa Umbo la Ndani na Umbo la Nje

 

Uchanganuzi huu hauwezi kuonyesha uhusiano kati ya umbo la ndani (maana ya sentensi) na umbo la nje (muundo wa sentensi). Hili linaathiri uchambuzi wa kauli tendi (mtenda) na kauli tendwa (mtendewa).

Mfano:

Kauli tendi: "Juma alikata mti."

Kauli tendwa: "Mti ulikatwa na Juma."

Uchanganuzi wa kiambajengo kifuasi hauonyeshi uhusiano kati ya sentensi hizi mbili, ingawa kiuhalisia zina maana moja.

 

 UDHAIFU WA KIAMBAJENGO KIFUASI

Uchanganuzi wa kiambajengo kifuasi huchukulia kuwa sentensi zote zina muundo wa kimstari, hivi ni kwamba sentensi ni muambatano wa kiambajengo (maneno) wazo ambalo sio sahihi

Uchanganuzi kiambajengo kifuasi hauna uwezo wa kuziunganisha sentensi na kuzichanganua bali huchanganua sentensi ambazo zipo katika lugha husika.

Uchanganuzi huu hauwezi kutumiwa katika kuchanganua sentensi ambazo si sahihi kimuundo.Kwa mfano alimkimbilia mwizi mwituni mnene

Haina uwezo wa kuonyesha uhusiano baina ya baadhi ya sentensi kwa mfano sentensi ambayo kiima ni mtenda na ambayo kiima ni mtendewa,sentensi yakinishi na sentensi kanushi

Huchanganua sentensi za muundo mmoja hivi kwamba ni vigumu kitumia uchanganuzi huu katika kuchanganua sentensi changamano

Wanasarufi miundo hawakubainisha uhusiano wa umbo la ndani na umbo la nje katika muundo wa sentensi, kwa hivyo ilikuwa vigumu katika uchanganuzi wa sentensi zenye kauli tendi na tendwa.

0 maoni:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Wasiliana nami papo kwa papo

Name

Email *

Message *

Ads 468x60px

Breaking News

Top Featured

Featured Posts

Sample text

Sample Text

Recomended

Facebook

Advertise

Most Popular

Connect With Us

Followers

Social Icons

Pages

Pages

BTricks

Pages

Popular posts

Tafuta chochote ukiwa hapahapa

Kategori

Recent Comments

You can replace this text by going to "Layout" and then "Page Elements" section. Edit " About "

recent posts

Video Of Day

TRANSLATE

Instructions

Video

Flickr Images

FURAHIA UWEPO WAKO HAPA

Logo Design by FlamingText.com
Logo Design by FlamingText.com

Imetembelewa mara

NUMBER OF VIEWERS

Popular Posts

SAJIRI

Definition List

premium-wordpress-themes.org