17 Jun 2025

 Imeandaliwa na Mtila Mswahili.


UTANGULIZI

Ufundishaji ni dhana pana inayohusisha mchakato wa kuhamisha,  na kuendeleza ujuzi wa lugha na mawazo mapya kwa wanafunzi. Ufundi huu unajumuisha mbinu mbalimbali za kufundisha ili kuyafikia malengo  ya  kielimu, kwa kuzingatia  muktadha wa kijamii na kiutamaduni. Kwa mujibu wa Taasisi ya Elimu Tanzania (TET)(2005), somo la Kiswahili linalenga kumwezesha mwanafunzi kuwasiliana kwa ufasaha katika nyanja na fani mbalimbali za kimaisha kwa kutumia lugha ya Kiswahili kupata maarifa, mielekeo, stadi za kijamii na utamaduni, kiteknolojia na kitaaluma kutoka ndani na nje ya nchi. Ili malengo haya yatimie, mwanafunzi anapaswa kuonesha kuwa maarifa yanayotolewa kwenye somo la Kiswahili ameyapata kwa kufanya mtihani wa kuhitimu elimu ya sekondari. Ufundishaji umekuwa na changamoto mbali mbali katika skuli za Zanzibar kama ifuantavyo:

Changamoto za Lugha: Changamoto hii hujitokeza katika matumizi ya misamiati au maneno magumu katika kufundisha masomo mbali mbali kama kiswahili. Maneno magumu yanaweza kumtatisha mwanafunzi juu ya jambo analojifunza walimu wengi hasa wanzanzibar wamekuwa waliwafundiaha wanafunzi kwa kutumia istilahi mbali mbali tofauti na yenye ugumu ndani jambo ambalo hupelekea wanafunzi wengi kutofikia Lengo linalotakiwa na kwa kiasi kikubwa wanafunzi wanashindwa kuelewa kinachofundishwa. Jambo hili husababisha wanafunzi kuona somo ni gumu kiasi cha kulikatia tamaa.

Changamoto za Zana za Kufundishia na Kujifunzia: kuwapo kwa upungufu wa vitabu vya kufundishia na kujifunzia, hasa vya kiada na ziada. Pia, hakuna vitabu vya kumungoza mwalimu kama vile kamusi, majarida, karatasi ngumu za kuchorea michoro, chatipindu, vifaa vya kurekodi kama tepurekoda au kinyonyi (flashi) na redio, ambavyo vingetumika kwaajili ya kufundishia pia kupelekea kutofikia lengo la kufikisha ujuzi wowote kwa mwanafunzi, skuli nyingi za Zanzibar zimekuwa zikipiga kelele juu ya kutokuwepo kwa vifaa vya kufundishia na kujifunzia jambo hili hupelekea changamoto kubw kwa wanafunzi. Na wanafunzi wengi wazanzibar wamekuwa wakijifunza kwa kukariri kuliko kwa Vitendo hii ni kutokana vifaa havipatikani maskulini.

Changamoto ya walimu wenye sifa: Katika kufikia lengo la ufundishaji huhitajika mwalimu aliebobea na mwenye sifa juu ya ufundishaji lakini kumekuwa na changamoto kubwa ya walimu wenye sifa ya kufundisha kwa sasa katika visiwa vya Zanzibar hii nikutokana na walimu wengi kutokuwa na elimu ya kutosha katika ufundishaji na walimu wengi Zanzibar waliajiriwa bila ya kuzingatia vigezo muhimu anavyopaswa kuwa navyo mwalimu kama wa sanaa na pia wasayansi hivyo jambo hili hupelekea kutofikiwa lengo la ufundishaji.

Changamoto ya muda mdogo wa kujifunzia: Ufinyu wa muda wa masomo ni changamoto nyingine inayokabili ufundishaji Katika shule nyingo za Zanzibar muda wa masomo ni mfupi, na hii inamaanisha kuwa walimu hawana muda wa kutosha kufundisha kwa kina. Hali hii inasababisha kukosa uelewa wa kina wanafunzi wanapokuwa na muda mfupi wa kujifunza, wanakosa fursa ya kuelewa kwa kina dhana na kanuni za masomo mbali mbali yanayotolewa kama vile kiswahili. Hii inawafanya wanafunzi kutokuwa wamahiri kwa kile wanachofundishwa.

Changamoto za Taaluma/Ujuzi: Changamoto zinazohusiana na taaluma/ujuzi ni kikwazo katika ufundishaji wa   Kiswahili .Kuna baadhi ya walimu  wana elimu ya vyeti ila umahiri ni sifuri hivyo kuna changamoto ya uwezo wa kufundisha kwa walimu na tatizo hili husababishwa na changamoto za walimu kitaaluma.pia tatizo jengine linasabishwa na walimu kutofundisha vizuri vitabu vya fasihi kama vile tamthiliya na diwani .Walimu wengi, hasa waliosoma zamani bado wanashikilia misimamo yao ikiwa kuna jambo jipya hawalijui, huishia kupinga kwa kutumia mifano ya vitabu vya zamani ambavyo hata kwenye mtaala havitumiki. Hawataki kujifunza mambo mapya kwa kujisomea na kufuatilia tafiti.

Mtazamo Hasi kuhusu Kiswahili: Zanzibar kuna changamoto ya mtazamo hasi kuhusu lugha ya Kiswahili ambapo Changamoto hii inahusisha wazazi, wanajamii na wanafunzi. Wazazi huwahimiza watoto kujifunza na kuwekeza nguvu kwenye masomo yanayofundishwa kwa Kiingereza. Jamii imeweka mtazamo kwamba somo la Kiswahili linaeleweka; pia, halimsaidii mwanafunzi kupata ajira akihitimu likilinganishwa na masomo ya Kiingereza. Mtazamo huu huathiri ufundishaji.

            Hivyo changamoto hizi zinahitaji mikakati madhubuti na ushirikiaono kati ya serikali, walimu, wazazi pamoja na wadau wengine wa elimu,  ili kuhakikisha Kiswahili kinapata muamko mzuri wenye kuleta mafanikio kwa kuboresha miundo mbinu ya skuli, kuongeza muda wa kufundisha kwa somo la Kiswahili, kutoa elimu kwa walimu wa zamani ili kuendana na mitaala mipya  na  kutoa elimu kwa wanafunzi na wazazi pamoja na wanaja ii kuhusiana  na mafanikio yanayopatikana  kwenye lugha ya Kiswahili baada ya kuhitimu.


MAREJEO

BAMITA (2022): Mwongozo wa Upimaji Katika Shule za Msingi. Dar es salaam.

Juma, H.K (2017): Tathmini ya Mitaala ya Ufundishaji wa Kiswahili Ngazi ya Sekondari katika Matumizi ya Nadharia Nchini Tanzania.

Akaka, L. (2013): Changamoto zinazowakabili Walimu katika Ufundishaji wa Kiswahili katika Shule za Upili nchini Kenya. Kioo cha Lugha.

0 maoni:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Wasiliana nami papo kwa papo

Name

Email *

Message *

Ads 468x60px

Breaking News

Top Featured

Featured Posts

Sample text

Sample Text

Recomended

Facebook

Advertise

Most Popular

Connect With Us

Followers

Social Icons

Pages

Pages

BTricks

Pages

Popular posts

Tafuta chochote ukiwa hapahapa

Kategori

Recent Comments

You can replace this text by going to "Layout" and then "Page Elements" section. Edit " About "

recent posts

Video Of Day

TRANSLATE

Instructions

Video

Flickr Images

FURAHIA UWEPO WAKO HAPA

Logo Design by FlamingText.com
Logo Design by FlamingText.com

Imetembelewa mara

NUMBER OF VIEWERS

Popular Posts

SAJIRI

Definition List

premium-wordpress-themes.org