17 Jun 2025

 Imeandaliwa na Mtila Mswahili


 NADHARIA ZA UANDISHI WA KAZI ZA FASIHI.

Maana ya Nadharia,

BAKIZA (2010) Nadharia ni mawazo yanayotumika kuwa ni muongozo wa kutekeleza jambo au kutambulika kwa dhana.

Kwa ujumla nadharia ni mfululizo wa dhana au mtazamo wa kisayansi au falsafa inayokusudiwa kuelezea na kufafanua.

Maana ya nadharia za uandishi wa kazi za fasihi.

Kwa kuangalia muktadha wa uandishi wa kazi za fasihi, nadharia ni mfumo wa mawazo, mitazamo au falsafa zinazomwongoza mwandishi au mhakiki wa kazi ya fasihi katika kutunga, kuchambua au kuelewa maana na madhumuni ya kazi hiyo. Nadharia husaidia kuelewa kwa kina vipengele vya fasihi kama vile dhamira, wahusika, mandhari, lugha, na muundo.

Mambo ambayo humuongoza Mwandishi kutokana na nadharia.

                         Mwongozo katika uandishi.Nadharia humwelekeza mwandishi kuandika kazi ya fasihi kwa kuzingatia mtazamo fulani wa kijamii, kisiasa, kihistoria, au kisaikolojia. Mfano:Mwandishi anayeandika kwa kutumia nadharia ya uhalisia atazingatia maisha halisi ya jamii, matatizo ya kawaida na jinsi watu wanavyoathirika.Mwandishi anayefuata nadharia ya kiisimu anaweza kuandika akizingatia muundo wa lugha, matumizi ya tamathali, na mtindo wa mawasiliano.

                                 Ufunuo wa Maudhui.Kwa kutumia nadharia, mwandishi anaweza kufichua ukweli wa kijamii au kimawazo, kwa mfano:Nadharia ya kikasumba: huonyesha dhuluma za kitabaka.Nadharia ya kifeministi: hufichua ukandamizaji wa wanawake.

                            Uchanganuzi wa wahusika na migogoro.Nadharia huwasaidia waandishi kuchora wahusika na migogoro kwa njia ya kina. Wahusika wanaweza kuwakilisha vikundi vya kijamii, mitazamo ya kifalsafa, au hali ya kisiasa.

                               Ujenzi wa dhamira kwa ujumla.Kila nadharia huleta ujumbe au mafunzo mahsusi. Kwa mfano:Nadharia ya uondoaji (deconstruction) huchanganya au kupindua maana za kawaida.Nadharia ya uhulishaji huonesha jinsi watu huathiriwa na jamii au tamaduni zao Kwa kila jamii husika.

Nadharia ya uandishi wa kazi za fasihi kutokana na Mungu.

                          Nadharia ya uandishi inayotokana na Mungu inahusisha imani kwamba fasihi imeletwa na Mungu, Mungu pia alikuwa muhusika mkuu .Pia, ilikuwa kwamba Mungu alikuwa na matendo mengi aliyafanya huku akiwa ni muhusika mkuu wa matendo na mndirimo wa maisha ya viumbe.Hivyo hapo ilipoibuka uandishi wa kazi za fasihi.

Udhaifu wa nadharia hii.

             Nadharia hii imeibuwa maswali kadhaa wa kadhaa juu ya usanii wa Mungu, maswali yenyewe ni kama ifuatavyo,Ni kuwa Mungu ni kitu kisichoonekana ni kwa namna gani awe mhusika wa matukio?, Dhamira zitafikishwaje na kitu kilichopo Nadharia hii haikubaliki kwa sababu kuna udhaifu mkubwa ndani yake.

Nadharia ya uandishi kutokana na mazingira uhalisia wa mazingira.

                           Nadharia ya uandishi wa kazi za fasihi kupitia uhalisia wa mazingira inahusisha mtindo wa utunzi unaozingatia na kuakisi hali halisi ya maisha ya jamii, mazingira yake, na matukio yanayotokea katika mazingira hayo. 

Udhaifu wa nadharia hii

                            Nadharia hii ya uandishi wa kazi za fasihi kutokana na uhalisia wa mazingira ina udhaifu , Udhaifu wake ni kwamba sio kila wanachoandika waandishi kinatoka kwenye mazingira halisi bali huwaza na kuwazua Kwa namna ya kipekee ambayo hulenga kumfurahisha msomaji,msikilizaji.Pia hutaka kuhifadhi Utamaduni wa mtu binafsi katika maisha yake.

Nadharia hii pia husababisha ugomvi Kwa waandishi wanapoandikia uhalisia wa mazingira bila ya kuficha chochote.

Nadharia ya uandishi wa kazi za fasihi kutokana na wigo.

Maana ya Nadharia ya Wigo

Kwa mujibu wa wataalamu mbalimbali, nadharia ya wigo inafafanuliwa kama ifuatavyo:-

                     Nadharia ya wigo ni Ile hali ambayo mwanaadamu alianza kuwa mbunifu kwa kuiga maumbile mbalimbali yaliyomzunguka pamoja na kuiga vitu vilivyomo katika mazingira yake kama vile miti,sauti za wanyama,watu na kadhalika.

                    Waasisi wa nadharia ya wigo ni Wagiriki ambao ni Plato na Aristotle ambao ni wasambazaji wakuu wa nadharia hii,waasisi wa nadharia hii wanadai kuwa fasihi imetokana na mwigo,uigaji.Hii ni kwamba binaadamu alianza sanaa kwa kuwa muigizaji wa maumbile yaliyomzunguka . Hivyo kazi za fasihi za mwanzo mara nyingi zilijaribu kusawiri vitu vilivyomo katika mazingira kama miti , sauti za wanyama,milio ya vitu mbalimbali.

                     Pia Plato anaendelea kuifananisha dhana ya mwigo na uungu.Anasema " Vyote binaadamu wanavyoona na kuiga ni mwigo wa vitu halisi vilivyopo kwa Mungu.

Katika nadharia hii Kuna vipengele muhimu vya nadharia ya wigo katika fasihi (uandishi)ni hivi ifuatavyo:-

Wigo wa Maana,Mtindo wa mbinu za kifasihi,wigo wa wahusika na wigo wa maudhui.

Udhaifu wa nadharia ya uandishi kutokana na wigo.

        Nadharia hii Ina udhaifu,Sio kweli kwamba mwanaadamu anaiga kutoka kwa Mungu.Pia hudumaza akili ya Mwandishi kwa kutoa kuhangaisha akili yake mwenyewe.

Nadharia ya Uandishi wa kazi za fasihi , Nadharia kipaji.

            Nadharia ya uandishi wa kazi za fasihi kupitia kipaji inazingatia uwezo wa kipekee wa mwandishi katika kuunda na kuwasilisha kazi za fasihi.  Kipaji hiki kinahusisha ubunifu, ufanisi katika matumizi ya lugha, na uwezo wa kuhamasisha hisia na mawazo ya wasomi.

Mfano mzuri ni Waandishi wenye vipaji ni Said Ahmed,Shaaban Robert na wengineo,Mwandishi kama Shaaban Robert anajulikana kwa ustadi wake katika matumizi ya lugha na mbinu za fasihi.  Katika riwaya yake Rosa Mistika, anatumia lugha yenye uzito na mitindo ya kipevu kuwasilisha masuala ya kijamii na kiuchumi, akionyesha ufanisi wa kipaji chake katika uandishi.

Nadharia ya uandishi wa kazi za fasihi kupitia kipaji inasisitiza uzuri ,na ufanisi wa kazi za uandishi wa uwezo wa kipekee wa mwandishi katika kuunda kazi za fasihi.

Udhaifu wa nadharia hii.

                              Udhaifu wa nadharia hii kwamba sio waandishi wote wana kipaji bali walianza kidogo kidogo na baadae kufikia hatua kubwa ya uandishi na mwishowe kujulikana.

Nadharia ya kikasumba .

         Nadharia hii imejikota zaidi kwa mwandishi ambae huendeahwa na hisia zake au za watu Kwa kusikia propaganda zinazoletwa na jamii .

Udhaifu wa nadharia hii

            Nadharia hii Ina udhaifu mkubwa kwani miongoni mwa sifa za msanii ni vizuri kushughulikia maswala yanayoikumba jamii kwa kuyaondosha au kuwaasa watu kwenye mambo hayo na sio kuongeza chuki ndani ya jamii.

                    Hivyo nadharia zote zina umuhimu fulani ambao umechochea kwa namna moja au nyengine ambayo umeweza kuleta faida ambayo imewasaidia wanafunzi wengi katika masuala yao ya kielimu kwenye kada tafauti tafauti.

 

 

MAREJELEO.

Wizara ya Elimu na Utamaduni,(2003).Ufundishaji unaozingatia Ujenzi wa Maana,Chuo cha  Ualimu Morogoro: Ecoprint Ltd.

TUKI, (2004). Kamusi ya Kiswahili sanifu (toleo la pili),Nairobi: Oxford University Press.

Mulokozi,M.M.(2017). Utangulizi wa fasihi ya Kiswahili.Dar es salaam.Tanzania

TET, (2014). Kiswahili,kidato cha nne,Tanzania: Oxford University limited.

Kumar,R.(2021). Research methodology,(4ed).London:SAGE Publications India Pvt ltd.

https://www.msomibora.com/2018/06/Kiswahili -form-one-topic-4-fasihi.html?m=1.

https://learn.farmhub.ag.

https://sw.wikipedia.org.

0 maoni:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Wasiliana nami papo kwa papo

Name

Email *

Message *

Ads 468x60px

Breaking News

Top Featured

Featured Posts

Sample text

Sample Text

Recomended

Facebook

Advertise

Most Popular

Connect With Us

Followers

Social Icons

Pages

Pages

BTricks

Pages

Popular posts

Tafuta chochote ukiwa hapahapa

Kategori

Recent Comments

You can replace this text by going to "Layout" and then "Page Elements" section. Edit " About "

recent posts

Video Of Day

TRANSLATE

Instructions

Video

Flickr Images

FURAHIA UWEPO WAKO HAPA

Logo Design by FlamingText.com
Logo Design by FlamingText.com

Imetembelewa mara

NUMBER OF VIEWERS

Popular Posts

SAJIRI

Definition List

premium-wordpress-themes.org