17 Jun 2025

 Imeandaliwa na Mtila Mswahili 

Mbinu za ufundishaji ni njia au mbinu ambazo walimu wanazitumia katika mchakato wa kutoa elimu kwa wanafunzi. Zinatoa ramani jinsi mwalimu anavyopanga, kutekeleza na kusimamia mchakato wa kufikisha maarifa, ujuzi na mitazamo kwa wanafunzi. Lengo kuu la mbinu za ufundishaji ni kuwasaidia wanafunzi kufikia malengo ya kujifunza yaliyowekwa.

Mbinu zisizoshirikishi ni mbinu ambazo huweka msisitizo kwa walimu kama mtoaji mkuu wa maarifa, huku mwanafunzi akiwa mpokeaji zaidi. Hizi zinaweza kujumuisha matumizi ya data zilizokusanywa awali,tafiti za maktaba na uchambuzi wa takwimu.

Sifa za mbinu zisizoshirikishi                                      

v  Mwalimu ni kituo kikuu cha maarifa na habari: Jukumu lake ni kusambaza taarifa huku wanafunzi wakitegemea yeye kwa kila kitu wanachojifunza.

Mfano-:                                        

Mwalimu akitoa mhadhara darasani kuhusu sifa za sayari huku wanafunzi wakibaki kimya na kuandika maelezo tu.

v  Ufanisi katika kusambaa kwa tarifa nyingi: Mbinu hizi huruhusu kwa kiasi kikubwa cha habari kusambazwa kwa wanafunzi wengi kwa muda mfupijambo linalofaa kwa mada pana au darasa kubwa.

Mfano-:

Mhadhara wa utangulizi wa somo jipya katika chuo kikuu, ambapo profesa anatoa muhtasari wa kozi nzima kwa muda mfupi.

v  Msisitizo kwenye kukariri ukweli na dhana: Lengo kuu mara nyingi ni kuhakikisha wanafunzi wanakariri ukweli, kanuni au fomula.Uelewa wa kina au matumizi ya maarifa hayapewi kipao mbele.

Mfano-:

Mwalimu akirudia mara kwa mara fomula za fizikia na kutaka wanafunzi wazikariri kwa ajili ya mitihani, bila ya kuwapa matatizo ya vitendo ya kuvitumia.

v  Udhibiti kamili wa walimu: Mwalimu ana udhibiti kamili wa mtaala, kasi ya ufundishaji na shuguli zote za darasani. Anaamua nini kifundishwe, linin a jinsi gani.

Mfano-:

Mwalimu anapanha darasa lake lote na kufuata kitabu cha kiada kwa ukamilifu, akitoa maelekezo ya moja kwa moja bila ya kutoa nafasi au shughuli za hiari za wanafunzi.

v  Mpangilio maalumu wa kimya kimya darasani: Mazingira ya darasani mara nyingi huwa tulivu na yamepangwa ambapo wanafunzi wanakaa kimya na kumsikiliza mwalimu, kelele na mijadala isiyo na mpangilio hupunguzwa.

Mfano-:

Darasa likiwa kimya kabisa wakati mwalimu anaandika maelezo muhimu kwenye ubao ,  huku wanafunzi wakinakili tu.

Ubora wa mbinu zisizoshirikishi

v  Kujifunza kwa kutazama bila ya kujaribu chochote: Mbinu hii wanafunzi wanatazama maonyesho au video bila ya kushiriki moja kwa moja na kike mwalimu anachokionesha na kukifundisha.

Mfano-:

Wanafunzi wanaweza kutazama maonyesho ya majaribio ya kisayansi bila ya kufanya majaribio wenyewe.

v  Usambazaji wa haraka wa taarifa nyingi: Mbinu zisizoshirikishi kama vile mihadhara huruhusu mwalimu kusambaza kiasi kikubwa cha tarifa kwa wanafunzi weni kwa muda mfupi.

Mfano-:

Katika chuo kikuu Profesa anaweza kutoa mhadhara wa saa mbili unaofunika mada nzima ya Hisroria ya uchumi wa Dunia akiwasilisha matukio muhimu na nadharia bila ya kusitisha na mijadala mingi.

v  Rahisi kutekeleza na rasilimali chache: Mbinu hizi hazihitaji rasilimali nyingi za ziada kama vile vifaa maalumu, vitabu vingi vya rejea au teknolojia ya hali ya juu na kutekelezwa hata katika rasilimali chache.

Mfano-:

Skuli iliyo na rasilimali chache inaweza kutumia mbinu ya walimu kutoa maelezo kwa kutumia chaki na ubao pekee bila kuhitaji vitabu vya ziada au kompyuta nabado kufikisha ujumbe muhimu.

v  Rahisi kwa wanafunzi wenye mahitaji maalumu ya utulivu: Baadhi ya wanafunzi hasa wenye mahitaji maalum kama vile tawahudi, wanaweza kustawi vizuri zaidi katika mazingira tulivu na wenye mpangilio wa moja kwa moja unaopatikana katika mbinu zisizoshirikishi.

Mfano-;

Mwanafunzi mwenye tawahudi anaweza kunufaika zaidi na maelezo ya moja kwa moja kutoka kwa mwalimu bila ya usumbufu wa shughuli za kikundi kwani inamruhusu kujikita kikamilifu kwenye maelezo.

v  Kutoa msingi wa maarifa kwa haraka kwa mada mpya au changamoto ambazo wanafunzi hawana ufahamu wowote:Mbinu hizi zinaweza kutoa msingi wa maarifa kwa haraka kabla ya kuanza shuguli shirikishi zenye kina zaidi.

Mfano-:

Kabla ya kuanza mradi wa kikundi kuhusu mfumo wa juu mwalimu anaweza kutoa mhadhara mfupi wa kueleza dhana za msingi za sayari, nyota, galaksi ili wanafunzi waw na msingi wa kuanzia.

Udhaifu wa mbinu zisizoshirikishi

v  Ukosefu wa ushiriki na uchochezi kwa wanafunzi: Wanafunzi hukaa kimya wakisikiliza au kuandika tu hawapati fursa ya kuuliza maswali, kujadili au kuunganisha mada na maisha yao na kupunguza umakini wa kujifunza.

Mfano-:

Mwalimu anatoa hutuba ndefu kuhusu historia bila ya kuwapa wanafunzi nafasi ya kujadili au kutoa maoni, wanafunzi wengi hupoteza umakini na hawaelewi kikamilifu.

v  Kutoweza kugundua udhaifu wa kujifunza kwa haraka: Mwalimu huwa na ugumu wa kujua mapema wapi wanafunzi wanashindwakuelewa, makosa yanaweza kujengeka nbila ya kushughulikiwa na kuacha mapengo makubwa katika ujifunzaji.

Mfano-:

Mwalimu anaeleza sheria za sarufi bila ya kuwapa wanafunzi mazoezi au maswali ya haraka. Wakati wa mitihani matokeo mabaya hufichuo mapengo ambayo yangekuwa yamegundulika mapema kwa ushiriki.

 

v  Ukosefu wa ustadi wa mawasiliano na ushirikiano: Mbinu hizi hazitoi fursa kwa wanafunzi kukuza ustadi muhimu wa mawasiliano na kufanya kazi kwa pamoja.

Mfano-:Mwalimu anafanya jaribio la sayansi mbele ya darasa na kueleza matokeo bila ya kuwapa wanafunzi fursa ya kujadili jinsi ya kupanga jaribio au kuchambua data kwa pamoja na husababisha kuwanyima wanafunzi ustadi wa ushirikiano.

v  Kuchosha na kupunguza hamu ya kujifunza: Ukosefu wa shughuli za vitendo, mijadala na mwingiliano hufanya masomo yawe kavu na yasiyovutia na kupunguza hamu ya wanafunzi kujifunza.

Mfano-:

Mwalimu anasoma hadithi nzima ya fasihi kwa sauti bila ya kuruhusu wanafunzi kujadili wausika au ujumbe wa hadithi, hii inaweza kufanya somo lionekane lenye kuchosha na lisilo na ubunifu.

v  Kukosa kukuza uwezo wa kufikiri kwa makini: Mbinu hizi hazichochei wanafunzi kufikiri kwa kina, kudadisi, au kuhoji taarifa wanazopokea.Wanakumbuka tu kile wanachofundishwa bila ya kuchambua.

Mfano-:

Katika somo la uraia mwalimu anasoma katiba bila ya kuwaruhusu wanafunzi kujadili vifungu vyake au kuunganisha na changamoto za jamii, wanafunzi hawawezi kukuza uwezo wa kuchambua sharia au sera.

Mbinu shirikishi ni mbinu ambazo zinawahusisha wanafunzi kikamilifu katik mchakato wa kujifunza, badala ya kuwa wapokeaji tu wa taarifa. Mbinu hizi zinaweza kujumuisha mahojiano, makundi ya kujadili na tafiti za uwanjani.

Sifa za mbinu shirikishi

v  Mwalimu ni kituo cha kujifunza badala ya mwalimu kuwa chanzo pekee cha maarifa: Mwanafunzi anakuwa mjenzi na mtafiti wa maarifa yake mwenyewe, akiongozwa na mwalimu.

Mfano-:

Badala ya mwalimu kueleza tu mzunguko wa maji wanafunzi hupewa mradi wa kuchunguza mzunguko huo kwa kutumia vifaa rahisi na kasha kuwasilisha matokeo yao.

v  Kukuza ustadi wa mawasiliano na ushirikiano: Wanafunzi hufanya kazi kwa pamoja, wakijadiliana na kusaidiana, hii inawajenga uwezo wa kuwasiliana kwa ufanisi, kusikiliza na kushirikiana.

Mfano-:

Kazi za vikundi zenye lengo la kutatua matatizo ya kisayansi au kuandaa mada ya kuwasilisha, huwalazimisha wanafunzi kuwasiliana na kushirikiana.

v  Mwalimu kama mwezeshaji na mshauri: Jukumu la mwalimu hubadilika kutoka kuwa mtoaji wa maarifa na kuwa mwezeshaji anayeongoza, Iushauri, na kuhamasisha wanafunzi katika safari yao ya kujifunza.

Mfano-:

Mwalimu anasimamia mijadala, anatoa muongozo, na anahakikisha wanafunzi wanapata rasilimali sahihi wanapofanya mradi wa utafiti, badala ya kuwapa majibu moja kwa moja.

v  Kuongeza morali na kujiamini: Wanafunzi wanaposhiriki na kufanikiwa kayika shughuli sirikishi, morali yao huongezeka na kujiamini kwao katika uwezo wao wa kujifunza na kutatua matatizo huimarika.

Mfano-:

Mwanafunzi anapomaliza mradi mgumu wa kikundi na kuuwasilisha kwa mafanikio darasani, anajisikia mwenye uwezo na mwenye kujiamini zaidi.

v  Kutumia uzoefu na maarifa ya awali ya mwanafunzi: Mbinu shirikishi huthamini uzoefu na maarifa ambayo mwanafunzi tayari anayo na kuyafanya kama msingi wa kujifunza mada mpya.

Mfano-:

Kabla ya kuanza somo la biashara mwalimu anaweza kuwauliza wanafunzi watoe mifano ya biashara ndogondogo wanazozifahamu katika maeneo yao na kasha kuunganisha na dhana ya kifedha.

Ubora wa mbinu shirikishi

v  Hujenga uhusiano bora kati ya mwalimu na mwanafunzi: Katika mazingira shirikishi mwalimu huwa kama mwezeshaji na mshauri bala ya mtoaji tu wa taarifa. Hii hujenga uhusiano mzuri wa kirafiki na wenye kuaminiana kati ya mwalimu na mwanafunzi.

Mfano-:

Mwalimu anayechangamana na wanafunzi katika shughuli za kikundi na kutoa msaada wa kibinafsi huwafanya wanafunzi wajiskie huru kuuliza maswali na kutafuta msaada wanapohitaji.

v  Huwaandaa wanafunzi kwa maisha halisi  na soko la ajira: Ujuzi kama vile mawasiliano, ushirikiano, utatuzi wa matatizo na kufikiri kwa makiniunaosisitizwa katika mbinu shirikishi nimuhimu sana katika maisha ya kila siku na soko la ajira la kisasa.

Mfano-:

Skuli inayotumia miradi ya kikundi na uwasilishaji wa mada mara kwa mara inawaandaa wanafunzi kwa mazingira ya kazi ambapo wanatakiwa kufanya kazi kwa wenzao, kuwasilisha mawazo na kutatua changamoto za pamoja.

v  Huwajenga wanafunzi kujiamini na kujitegemea: Wanapopata fursa ya kutoa maoni, kufanya makosa na kujifunza kutokana nayo na kutatua matatizo wenyewe, wanafunzi hujenga kujiamini katika uwezo wao na kujifunza kujitegemea.

Mfano-:

Mwanafunzi anayewakilisha mradi wake binafsi mbele ya darasa na kupokea maswali na maoni huongeza kujiamini kwake katika kueleza mawazo yake na kusimamia ujifunzaji wake.

v  Huongeza uhifadhi wa maarifa: Wanafunzi wanaposhiriki kikamilifu katika kujifunza wanashughulikia taarifa kwa njia nyingi tofauti (kusikia, kuona, kufanya na kujadili) na hivyo kuongeza uwezekano wa kukumbuka na kuhifadhi maarifa kwa muda mrefu.

Mfano-:

Badala ya kukariri matukio ya kihistoria wanafunzi wanaweza kuunda ramani za dhana au kuwasilisha matukio hayo kupitia sanaa au tamthilia, jambo linalowasaidia kukumbuka habari kwa ufanisi zaidi.

v  Kuboresha ustadi wa mawasiliano na ushirikiano: Shughuli shirikishi kama kazi za vikundi, mijadala na miradi ya pamoja huwapa wanafunzi fursa ya kujifunza jinsi ya kuwasiliana kwa ufanisi, kusikiliza wengine na kufanya kazi kwa kushirikiana.

Mfano-:

Kuwaweka wanafunzi katika vikundi kujadili na kutatua tatizo tata la hisabati kunawafundisha kushirikiana, kueleza mawazo yao na kujifunza kutoka kwa mawazo ya wenzao.

Udhaifu wa mbinu shirikishi

v  Zinachukua muda mrefu: Mbinu hizi huhitaji muda mwingi wa kupanga, kutekeleza na kusimamia. Hii ni cangamoto katika mitaala ya iliyojaa au yenye muda mfupi.

Mfano-:

Kupanga mjadala wa kikundi au mradi wa utafiti kunaweza kuchukua saa nyingi za maandalizi na utekelezaji na hivyo kupunguza muda wa kufundisha mada nyengine muhimu zilizo kwenye mtaala.

v  Ugumu wa kusimamia darasa kubwa: Katika madarasa yenye wanafunzi wengi kusimamia shughuli shirikishi kunaweza kuwa changamoto kubwa na vigumu kutoa umakini wa kutosha.

Mfano-:

Katika darasa la wanafunzi 80 mwalimu anaweza kupata ugumu kusimamia mijadala ya vikundi vidogo na kuhakikisha kila mwanafunzi anapata fursa ya kutoa mchango wake.

v  Baadhi ya wanafunzi kutoshiriki kikamilifu: Sio wanafunzi wote wanajisikia huru kushiriki katika shughuli za kikundi au mijadala. Baadhi wanaweza kuwa waoga, wanyamavu, au hawana uhakika na uwezo wao na hivyo kubaki nyuma.

Mfano-:

Katika mjadala wa darasa mwanafunzi mmoja mwenye aibu anaweza kutochangia chochote hata kama ana mawazo mazuri akihofia kuchekwa au kukosea.

v  Mahitaji makubwa kwa mwalimu: Mwalimu anahitaji kuwa na ujuzi wa ziada katika kupanga,  kuwezesha, na kutathmini mbinu shirikishi.

Mfano-:

Mwalimu ambae hajafunzwakutosha katika kusimamia miradi ya vikundi anaweza kujikuta akihangaika kutatua migogoro kati ya wanafunzi au kuhakikisha kazi inafanyika kwa urahisi.

v  Huweza kulea mazingira ya kelele na fujo: Hujumuisha muingiliano mwingi na harakati darasani, jambo ambalo linaweza kusababisha harakati na fujo endapo halitasimamiwa vizuri na kuathiri mkusanyiko.

Mfano-:

Wakati wa mijadala ya vikundi, darasa linaweza kuwa na kelele nyingi kiasi cha kuvuruga madarasa mengine jirani au kupunguza uwezo wa wanafunzi kujikita kwenye mada.

       Katika kuchagua kati ya mbinu zisizoshirikishii na shirikishi watafiti wanapaswa kuzingatia malengo ya utafiti wao, aina ya data wanayohitaji,na rasilimali zilizopo. Kila mbinu ina faida na changamoto zake hivyo ni muhimu kufahamu sifa hizi ili kufanya maamuzi bora katika mchakato wa utafiti, mara nyingi matumizi ya mbinu mchanganyiko yanawza kutoa matokeoo mazuri na yaliyo bora zaidi kwasababu huleta pamoja faida za mbinu zote mbili.

MAREJELEO

Magare, Y, D.(2011)Matumizi ya majadiliano ya vikundi katika kufunza stadi ya kuzungumza katika shule za upili katika tarafa za Masocho, Kaunti ya kisii, Kenya. Nairobi:Kenyatta University.

Ndege,J.,Kea,P.,Osoro,E.,Waititu,F.,Mucheria,Z.naWafula,W.(2020).Kiswahili Dadisi:Mwongozo wa Mwalimu Gredi ya 4.Nairobi:Oxford University Press.

Wasike,M.W.(2015).Tathmini ya marumizi ya nyimbo za kizazi kipya kama mbinu za kufundishia masuala ibuka katika Kiswahili kwenye shule za upili nchini Kenya.Kibabii University.Bungoma:Kibabii University.

0 maoni:

Post a Comment

Powered by Blogger.

Wasiliana nami papo kwa papo

Name

Email *

Message *

Ads 468x60px

Breaking News

Top Featured

Featured Posts

Sample text

Sample Text

Recomended

Facebook

Advertise

Most Popular

Connect With Us

Followers

Social Icons

Pages

Pages

BTricks

Pages

Popular posts

Tafuta chochote ukiwa hapahapa

Kategori

Recent Comments

You can replace this text by going to "Layout" and then "Page Elements" section. Edit " About "

recent posts

Video Of Day

TRANSLATE

Instructions

Video

Flickr Images

FURAHIA UWEPO WAKO HAPA

Logo Design by FlamingText.com
Logo Design by FlamingText.com

Imetembelewa mara

NUMBER OF VIEWERS

Popular Posts

SAJIRI

Definition List

premium-wordpress-themes.org