imeandaliwa na Mtila Mswahili.
Kwa mujibu wa Baraza la
Kiswahili la Zanzibar (BAKIZA), (2009)
Lahaja ni tafauti ya
matamshi ya wasemaji wa lugha moja walio katika mazingira tafauti ya ardhi ya
lugha ile.
Kwa ujumla -:
Lahaja
ni vilugha vidogovidogo vya lugha moja ambavyo hubainishwa na jamii au
jiografia. Lahaja za lugha moja zinakaribiana katika matamshi, miundo ya sarufi
na msamiati. Kama lugha hutofautiana katika matamshi tu tofauti hizo huitwa
lafudhi sio lahaja. Ni kweli ya kwamba Kiswahili kinaathiri lahaja za Zanzibar
kupitia hoja zifuatazo-:
Kiswahili
sanifu kinaathiri lahaja za Zanzibar
kupitia msamiati: Kupitishwa kwa maneno mapya lahaja za Zanzibar zimeendelea
kupokea maneno mengi kutoka kwa Kiswahili sanifu hasa yanayohusu dhana mpya, teknolojia,
elimu na masuala ya kitaifa. Mfano badala ya kutumia neno la kienyeji kwa
kompyuta moja kwa moja watu wengi sasa hutumia kompyuta moja kwa moja kutoka
kiswahili sanifu vilevile maneno kama vile televisheni, simu, serikali, rais na
bunge yamepenya sana katika matumizi ya kila siku na kusababisha athari katika
lahaja za Zanzibar.
Kuwepo
kwa utofauti wa matamshi: Kubadilika kwa matamshi ya baadhi ya maneno ingawa
matamshi ndio sehemu inyobaki kuwa tofauti kwa kiasi kikubwa kati ya lahaja na
Kiswahili sanifu kunaweza kua na mabadiliko kadri watu wanavyozidi kusikia na
kutumia Kiswahili sanifu. Mfano sauti fulani ambazo hazipo katika Kiswahili
sanifu zinaweza kuanza kutamkwa kwa namna inayokaribia zaidi matamshi ya
Kiswahili sanifu hasa katika mazingira rasmi au wanapozungumza na watu kutoka
sehemu nyengine.
Miundo
ya sarufi ya Kiswahili: Kurahisishwa kwa miundo ya sarufi Kiswahili sanifu kina
miundo ya kisarufi iliyorahisishwa kwa kiasi Fulani ikilinganishwa na baadhi ya
lahaja.Watumiaji wa lahaja wanaweza kuathiriwa na urahisi huu na kuanza kutumia
miundo hiyo katika mazungumzo yao. Mfano matumizi ya viambishi vya ngeli
yanaweza kua tofauti kidogo kati ya Kiswahili sanifu na baadhi ya lahaja.
Kunaweza kuonekana mwelekeo wa kufuata zaizdi kanuni za Kiswahili sanifu katika
matumizi ya ngeli au uundaji wa sentensi.
Suala
la istilahi na misemo maalumu: Elimu na utawala katika mazingira ya elimu na
utawala, Kiswahili sanifu ndio lugha kuu inayotumika. Hii inasababisha kuenea
kwa istilahi za kielimu na misemo katika matumizi ya kila siku ya wazungumzaji
wa lahaja mbalimbali. Mfano maneno kama mwalimu mkuu, wizara bunge, mahakama
yameingia katika msamiati wa kawaida na kusababishaathari katika lahaja za
Zanzibar.
Uwepo
wa vyombo vya habari: Ushawishi wa vyombo vya habari kama vile redio,
televisheni na magazeti kwa kiasi kikubwa hutumia Kiswahili sanifu. Hii
inawafanya wazungumzaj iwa lahaja kuwa wazi kwa kiasi sanifu na kuiga baadhi ya
maneno, misemo, na hata miundo ya sentensi na kusababisha athari katika lahaja
za Zanzibar.
Kukopa
maneno ya kiteknolojia: Maendeleo ya teknolojia yamefanya maneno mengi kutoka
katika lahaja za Zanzibar na kuingia katika Kiswahili sanifu na kuathiri lahaja
za Zanzibar. Mfano simu, runinga, kompyuta, intanet, ukurasa wa mtandao
yanatumika sana na kuathiri lahaja za Zanzibar.
Ni
dhahiri kuwa Kiswahili sanifu kina ushawishi mkubwa katika lahaja za Zanzibar
zina athari na inaonekana wazi katika msamiati, sarufi, matamshi kwa kiasi
Fulani na hasa katika matumizi ya msimbo mchanganyiko. Ingawa lahaja
zinaendelea kuwa sehemu muhimu ya utambulisho wa jamii za Zanzibar mwingiliano
na Kiswahili sanifu unaendelea kuzibadilisha na kuzifanya zifanane zaidi na
lugha za kitaifa na kusababisha athari katika lahaja za Zanzibar.
MAREJELEO
Khatib M S.(1983),Historia na maendeleo ya Kiswahili
Zanzibar:Lugha ya kiswahili.Makala za semina ya kimataifa ya waandishi wa
Kiswahili I.TUKI.uk19-49.
Horton,M.(1996),Shanga.London.
Temu,C.(1980),Lahaja za Kiswahili.TUKI(mimeo)
Mlacha,S.na A,Hurskainen(Wah)(1995),lugha,lahaja na fasihi ya
simulizi ya kiswahili.TUKI.
0 maoni:
Post a Comment